Hakuna uchawi wala baba yake ushirikina.
Kilichopo ni mambo ya kufikirika tu.
Lakini hata wewe hujachelewa.
Kama kweli uchawi upo nitolee mimi mfano.
Niroge.
unabishana tu au unafikir neno uchawi limetoka wap? Na huwez ukagundua kama umerogwa unaweza ukakuta wewe unamrahisishia mtu mambo yake bila kujijua kurogwa sio lazima ulale au uwe chizi.
Uchawi ni story tu haupo. Wengi wanaishi kwa story tu za kusadikika ukimuuliza atakwambia ndugu yangu lilimtokea hili au lile ila wao binafsi hawajawahi kuona zaidi ya kusikia. Hakuna uchawi
Uchawi upo 100%.
Nimeamini baada ya kumuuguza ndg yangu mpaka nikapoteza matumaini na maombi yalifanywa usiku na mchana ila haikusaidia.
Bwana mmoja aliweza kumtibu ndg yangu kwa usiku mmoja tena bila kuonana (wakiwa mikoa tofauti).
Ni sababu zile zile mtu hata msomi wa PHD anaamini kuna Mungu. Ukristo na Uslamu unazungumzia uchawi na shetani. Hivyo huwezi ukachagua super natural power moja ukaiamini na nyingine usiiamini. But again the key word is AMINI hivyo si sayansi kwamba utaprove. My bro has 2 PHD and he is a Priest (Catholic). So anaamini uwepo wa shetani na uchawi. Cardinal Pengo ktk makala yake moja alizungumzia mbinu za shetani. 1) Ni kufanya watu wasiamini presence yake na 2) Kufanya watu waamini nguvu zake hata kama hana hizo nguvu. Sasa 'wasomi' wengi mmenaswa kwenye hilo la kwanza. Washirikina wengi wamenaswa kwenye la pili.Ni kitu gani haswa kinamfanya mtu aamini kwamba kuna guvu za uchawi?
NI kwamba watu hawana elimu ya kutosha au zilikuwa mila za Kiafrika kabla ya
dini nyingine kuingia?
Nashindwa kuelewa maana tukisema elimu mbona kuna watu na ma PHD ya TZ bado
wanaenda kwa waganga?
Maana inasikitisha karne hii ya 21 bado watu wana ng'ang'ania mambo ya kishirikina.
Nashindwa kuelewa.
watu hawaamini lakin uchawi upo mfano katika familia yetu nina mdogo wangu yamemkuta
Mwaka 2010 aliamka asubuhi ghafla tu anapepesuka hawezi kusimama vizuri ikabdi mshua ampeleke hosptali wakampiga sindano lakin wapi
akapata transfer aende Temeke hospital,temeke wamepima kila ugonjwa,temeke wakapima hawakukuta chochote ikabidi wampeleke muhimbili nako ikawa hvyo hvyo,pima polio,chukua maji ya uti wa mgongo,piga ultrasound,piga x ray vyote hakukutwa na tatizo ikabdi aruhusiwe
aliporudi nyumbani mzee ikabidi ampeleke temeke kuna msikiti mmoja wakamsomea kisomo cha qur an kwa muda wa masaa mawili,wakati wanamsomea dogo alianza kulia ghafla na akajikojolea pale pale,kisomo kilipoisha tukarudi nae hom kesho yake asubuhi akapandisha jini bwana na kuanza kusema kuwa ametumwa na mtu,tulipojaribu kumuliza nan kamtuma hakutka kumtaja ikabdi tumuanzishie tiba ya kumtoa yule jini mpka leo hii jini limet oka lakin dogo hajasimama tena
hii ni stori ya kwel kwa asie amin haya mambo namuonea huruma tena asiseme kabsa.
Una kiuno kizuri jamaniNN unajua kuniita kwenye uzi kama huu unanitaka nini lakin??
afu kusema wateja wakubwa awa hao wanaovuta wapenzi ni wanawake you are very wrong.
for sure its a two way. there are women who go for the service as well as men.
kuna wanawake wanalia kabisa kisa aina ya ndoa walizoolewa nikimaanisha waliolewa na wanaume ambao waliwavuta hao wanawake kichawi hadi mwanamke kukubali kuolewa nae.
wapo wanawake waliopata waume kwa njia hizo hizo. siku hizi biashara ya kuvuta wapenzi na yenyewe haina mashiko biashara yao kubwa imebaki kuwa kuvuta watu kwenda kwenye ufreemason na kutoa pesa za bahati ama kuwapa hela za majini.
Bila Mungu mjin hapa hukawii kulishwa kinyesi cha mbuzi ukidhan ni korosho za mtwara
hamisi una mastory siku hizi
hahahahah!!! endelea kutuburudisha bana. naenjoy. naomba nikuroge. lolAcha hizo Mwajuma...
Naapa leo mwisho...hakuna tena stori toka kwangu.