Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,155
- 137,168
- Thread starter
- #21
NN unajua kuniita kwenye uzi kama huu unanitaka nini lakin??
Kwa sababu wewe ndo rejea yangu ya watu na vitisho vyao vya kuniroga.
Halafu, hivi hilo la majina ya mwana na mama mzazi ndo huwa sharti kuu la wachawi?
Manake huyo naye kaja kama ulivyokuja wewe 😀.
afu kusema wateja wakubwa awa hao wanaovuta wapenzi ni wanawake you are very wrong.
for sure its a two way. there are women who go for the service as well as men.
Sawa, nakubali kwamba sina takwimu lakini nikitumia anecdotes bado naona kuwa wateja wakubwa wa hao waganga ni wanawake.
Sasa kusema wateja wakubwa ni wanawake haimaanishi kwamba hakuna wanaume waendao huko.
Lakini kusema kweli mpaka sasa bado nadhani wanawake wanawapiku wanaume kwenye hilo.
Sijawahi kukutana na mwanaume aliyeenda kwa mganga kwenda kutafuta mitishamba ya mapenzi. We ushawahi?
kuna wanawake wanalia kabisa kisa aina ya ndoa walizoolewa nikimaanisha waliolewa na wanaume ambao waliwavuta hao wanawake kichawi hadi mwanamke kukubali kuolewa nae.
Nah...mimi nakataa aisee. Kwani mtu huwezi tu ukampenda mtu haraka haraka au hata taratibu halafu baadae penzi likachuja? Kwa nini likichuja sababu iwe uchawi na si tu kwamba upendo umepungua kwa hali ya kawaida tu?
wapo wanawake waliopata waume kwa njia hizo hizo. siku hizi biashara ya kuvuta wapenzi na yenyewe haina mashiko biashara yao kubwa imebaki kuwa kuvuta watu kwenda kwenye ufreemason na kutoa pesa za bahati ama kuwapa hela za majini.
Hapa inabidi nichecke tu kwa kweli 😀😀😀.
Ati pesa za nini? Au kujiunga na nini? Mbona umesahau kuongeza akili za darasani..?
Bila Mungu mjin hapa hukawii kulishwa kinyesi cha mbuzi ukidhan ni korosho za mtwara
Hakika maana kwa upumbavu wa kuamini upuuzi kama uchawi mtu akili [kama hata unayo] utaiweka kando ili kutimiza masharti ya mganga wako.
Mganga hakawii kukwambia ule maharage ya Mbeya na mayai ya kuchemsha halafu umvizie mumeo akiwa amelala umjambie mdomoni ili penzi lake likolee!