Balqior
JF-Expert Member
- Jun 8, 2021
- 1,709
- 5,699
Hii habari nimeiona Millard Ayo, wazee baada ya hili tukio Shivaz, kuna usalama kweli sasa hivi hapo, si patakuwa panawaka moto. Doria za 24 hours za polisi plus malaya wengine kuhama hiyo sehemu
Inakuaje unamnyonga mtu halafu unakimbia, story doesn't add up.
---
Wakizungumzia tukio hilo lililotokea juzi mchana, baadhi ya wakazi wa eneo hilo, akiwamo Saidi Salum, walidai waliona watu wamejaa katika nyumba hiyo ya kulala wageni.
Salum alidai kuwa alipokwenda kushuhudia kilichokuwa kinaendelea baada ya kuona idadi kubwa ya watu, alipata taarifa za mwanamke huyo kuuawa kwa kunyongwa.
“Huyu mwanamke si mgeni, tunamfahamu, maana hili ni eneo lake la kazi. Alikuwa ana... (alitaja neno lenye maana ya biashara isiyoruhusiwa kisheria) kila siku. Hata hapa Shivers ni mwenyeji, tunasikitika sana,” alisema.
Shuhuda mwingine aliyejitambulisha kwa jina moja la Kiu, alisema matukio kama hayo kwa Arusha ni mengi kwa sasa, hivyo aliomba serikali kuyafanyia kazi, ili wahusika wachukuliwe hatua kali na kuyakomesha.
Anna John alisema amepokea kwa masikitiko kifo cha mwenzao kwa kuwa hakuwa na ugomvi na mtu na alikuwa kazini.
Alidai kuwa kuna kijana alifika nyumba hiyo ya kulala wageni asubuhi na ilipofika mchana, alishangaa kumwona kijana huyo anakimbia akiwa na nguo ya ndani tu.
“Baada ya kuona amekimbia, waendesha pikipiki na vijana wengine waliopo eneo hili walishirikiana kumkimbiza na kumkamata eneo la Mnara wa Mwenge, mita chache kutoka hapa kisha kumkabidhi kwa polisi waliokuwa tayari wamefika eneo la tukio,” alidai.
Anna aliendelea kusimulia kuwa polisi walipofika katika nyumba hiyo ya wageni, waliingia katika chumba alimokuwa mwanamke huyo na kukuta haja kubwa imetapakaa kitandani na umauti ulikuwa umeshamkuta mwanamke huyo. Walibeba mwili wake na kuondoka nao.
Hassan Hamis alidai alimwona kijana huyo akiingia katika nyumba hiyo na baada ya muda alisikia kelele ndani ya chumba hicho zilizoashiria mzozo na ilipofika mchana, aliona kijana huyo anatoka kwa kukimbia akiwa amevaa nguo ya ndani tu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo, alithibitishwa kuwa na taarifa za tukio hilo katika nyumba ya kulala wageni ya Shivers.
“Kwa sasa wataalamu wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa (Mount Meru) wanaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo ili tujue kwa hatua zaidi,” alisema.
Kamanda Masejo alisema hawawezi kutaja jina la marehemu na mtuhumiwa kwa sasa mpaka uchunguzi utakapokamilika.
Chanzo: Nipashe
Inakuaje unamnyonga mtu halafu unakimbia, story doesn't add up.
---
Wakizungumzia tukio hilo lililotokea juzi mchana, baadhi ya wakazi wa eneo hilo, akiwamo Saidi Salum, walidai waliona watu wamejaa katika nyumba hiyo ya kulala wageni.
Salum alidai kuwa alipokwenda kushuhudia kilichokuwa kinaendelea baada ya kuona idadi kubwa ya watu, alipata taarifa za mwanamke huyo kuuawa kwa kunyongwa.
“Huyu mwanamke si mgeni, tunamfahamu, maana hili ni eneo lake la kazi. Alikuwa ana... (alitaja neno lenye maana ya biashara isiyoruhusiwa kisheria) kila siku. Hata hapa Shivers ni mwenyeji, tunasikitika sana,” alisema.
Shuhuda mwingine aliyejitambulisha kwa jina moja la Kiu, alisema matukio kama hayo kwa Arusha ni mengi kwa sasa, hivyo aliomba serikali kuyafanyia kazi, ili wahusika wachukuliwe hatua kali na kuyakomesha.
Anna John alisema amepokea kwa masikitiko kifo cha mwenzao kwa kuwa hakuwa na ugomvi na mtu na alikuwa kazini.
Alidai kuwa kuna kijana alifika nyumba hiyo ya kulala wageni asubuhi na ilipofika mchana, alishangaa kumwona kijana huyo anakimbia akiwa na nguo ya ndani tu.
“Baada ya kuona amekimbia, waendesha pikipiki na vijana wengine waliopo eneo hili walishirikiana kumkimbiza na kumkamata eneo la Mnara wa Mwenge, mita chache kutoka hapa kisha kumkabidhi kwa polisi waliokuwa tayari wamefika eneo la tukio,” alidai.
Anna aliendelea kusimulia kuwa polisi walipofika katika nyumba hiyo ya wageni, waliingia katika chumba alimokuwa mwanamke huyo na kukuta haja kubwa imetapakaa kitandani na umauti ulikuwa umeshamkuta mwanamke huyo. Walibeba mwili wake na kuondoka nao.
Hassan Hamis alidai alimwona kijana huyo akiingia katika nyumba hiyo na baada ya muda alisikia kelele ndani ya chumba hicho zilizoashiria mzozo na ilipofika mchana, aliona kijana huyo anatoka kwa kukimbia akiwa amevaa nguo ya ndani tu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo, alithibitishwa kuwa na taarifa za tukio hilo katika nyumba ya kulala wageni ya Shivers.
“Kwa sasa wataalamu wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa (Mount Meru) wanaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo ili tujue kwa hatua zaidi,” alisema.
Kamanda Masejo alisema hawawezi kutaja jina la marehemu na mtuhumiwa kwa sasa mpaka uchunguzi utakapokamilika.
Chanzo: Nipashe