Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Nilichojifunza kutoka kwa Bushite, ni mtu mwenye nia na jambo ila ni mtu ajiyejua namna bora ya kukamilisha nia yake. Ajitahidi sasa kujifunza namna bora ya kukamilisha nia. Hata vita alizokua anazianzisha kila mtu alikua anaziunga mkono lakini naamna alivyokua anazitekeleza ndo hakuna mtu anayemuunga mkono.
 
Hivi kusema ukweli ndio kulipa kisasi kaka ? alafu Gwajima sio level ya bashite,bashite ni level ndogo tu,alichosema Gwajima ni kuweka ukweli hadharani mjue kwamba mtu alipewa ukuu huo analevel ghani ya kufikiri
Ukweli upi? Si aweke vyeti hadharani aache maneno? Then na yeye aweke vyeti vyake vya uchungaji sheinzi type, atuambie alisomea wapi uchungaji
 
Wanataka awakamilishie jengo lao haraka kabla hajatumbuliwa
 
Nimeona hyo kamvua nguo zote walalh huyu dogo imekula kwake sujui atagombea nn na vyeti vyake feki ni pingamizi tu atendelea kuteuliwa viti maaluum tu na sizonje wake
Lakini huyu jamaa ni kichwa kama haya ni ya kweli, maana nasikia nafasi aliyonayo kachukua chake mapema hata akiwekwa pembeni ameisha jipanga sana ni suala la tu la kutumia kile alichokichuma kusonga mbele, usawa huu ukiwa na majumba kadhaa katika miji mikubwa tayali una mahala pa kuanzia
 
nafikiri ni aibu kubwa kwa taasisi kama itathibitika kwamba huyu tuliyemuamini na kumpa wadhifa mkubwa namna ile anatumia vyeti vya kununua.

Ni aibu kubwa kwa taifa letu sio jambo la kufurahia hata kidogo ,kumbe siku moja tunaweza kuja kuwakabithi wageni Nchi yetu kwa kutofanya vetting ya kutosha.

Ni aibu kubwa ni aibu aibu aibu kama itathibitika kwamba huyu mtu amenunua vyeti na tumeshindwa kumbaini na tukamwamini na kumpa wadhifa mkubwa kiasi hicho.

Hii ni dharau kubwa kwa wizara ya elimu na zoezi zima la kukagua vyeti lilikua upotevu wa muda na matumizi mabaya ya fedha za serikali kama itathibitishwa kwamba vyeti ni vya kununua ni hatari sana kwa sifa na mustakabali wa Taifa letu.
 
Raha utam raha utam! Namsihi JPM kama kweli alikuwa na nia thabiti ya kuwafukuza watumishi wenye vyeti kanjanja hii ndiyo nafasi nzuri amtumbue kwanza huyu Daudi kisha akamatwe na kupelekwa Mahakamani
 
Hapa hata mimi nashindwa kumuelewa Makonda ............ si atoe tu hivyo vyeti vya Paul Albert M ambavyo naamini anavyo kwenye brief case yake amevitunza!!

Issue hapa naona watu wanachanganya ....... issue siyo kuwa ana vyeti au hana. Issue ni je ana vyeti halali??
 
Daudi Albert Bushite angekuwa Mjapani muda huu tungesikia keshajiua kwa "harakiri".
 
*CV YA PAUL MAKONDA*

1. Alizaliwa tar.15/02/1981 katika kijiji cha Koromije, wilaya ya Misungwi, mkoa wa Mwanza.

2. Majina yake halisi ni *Daudi Albert Bushite*

3. Alianza darasa la kwanza mwaka 1988 katika shule ya msingi Koromije akitumia majina ya *Daudi Albert Bushite*. Mwaka 1991 alifeli darasa la 4, akarudia.

4. Mwaka 1992 alifeli tena na hivyo akahamishiwa Mwanza mjini, ili aweze kusoma na kupata masomo ya jioni (tuition).

5. Mwaka 1996 alihitimu darasa la 7 lakini hakuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya serikali.

6. Mwaka 1997 akajiunga na kidato cha kwanza shule ya sekondari ya Pamba.

7. Mwaka 2000 akahitimu kidato cha 4 na kupata daraja sifuri (division zero).

8. Mwaka 2001 akatumia cheti cha Ndg.Paul Christian Muyenge (chenye div.3 ya points 25) kujiunga na chuo cha uvuvi Nyegezi (Nyegezi Fisheries Training Institute) kwa masomo ya Certificate akahitimu mwaka 2002.

9. Mwaka huohuo 2002 akitumia cheti cha *Ndg.Paul Christian Muyenge*, alijiunga na Chuo cha uvuvi Mbegani Bagamoyo kwa masomo ya Diploma ya uvuvi (ORDINARY DIPLOMA IN MASTER FISHERMAN, NTA LEV.6), na kuhitimu mwaka 2005.

10. Mwaka 2003 alikutana na Ndg.Benjamin Sitta (mtoto wa Marehemu Samwel Sitta, ambaye ni Mayor Kinondoni kwa sasa). Wakawa marafiki.

11. Mwaka 2005 baada ya kuhitimu Stashahada yake ya uvuvi, aliomba admission Chuo cha Kilimo Sokoine kusoma shahada lakini akakosa nafasi.

12. Baada ya kukosa nafasi alienda kuishi nyumbani kwa Marehemu Sitta akiwa kama rafiki wa Ben (mtoto wa Sitta). Kwakuwa alitoka familia duni, Sitta aliahidi kumsomesha elimu ya juu.

13. Mwaka 2006, alipata udahili Chuo cha ushirika na biashara Moshi (wakati huo kikiwa chuo kikuu kishiriki cha SUA), kwa kutumia vyeti vyake vya certificate (ya Nyegezi) na diploma (ya Mbegani).

14. Alidahiliwa kwa course ya BA in Cooperate Management &Accounting. Mwaka 2007 alimaliza first year lakini akashindwa kuendelea na 2nd year baada ya kupata Suplementary 6 kati ya Course 8 alizokua akisoma (akawa discontinued).

15. Mwaka huohuo 2007 akaomba Admission upya. Akamaliza first year akiwa na _carries 3_ ambazo alienda nazo 2nd year. Mwaka 2008 akiwa 2nd year akapata supplementary 4 kati ya course 8 alizokua akisoma. Akawa na mzigo wa _carry over_ na _supplementary_. Akaamua kuacha chuo.

16. Mwaka 2008 akaenda kujaribu kuomba udahili chuo kikuu SUA kwa mara nyingine lakini akakosa.

17. Mwaka 2009 akarudi tena MUCcoBS kwa udahili mpya. Akaachana na CMA akachagua Community &Economic Development (CED).

18. Mwaka 20012 akahitimu shahada ya kwanza ya Community &Economic Development kwa jina la *_Paul C Makonda_* badala ya majina yake halisi ya *_Daudi A Bushite_*

19. Jina *_Makonda_* analitumia baada ya kula kiapo mahakamani kubadili jina. Cheti cha Form four kinasomeka *_Paul C Muyenge_* lakini vyeti vya elimu ya juu vinasomeka *_Paul C Makonda_* baada ya kuapa mahakamani.

20. Ndugu Daudi Albert Bushite ameoa (tangu mwaka 2009) lakini hajabahatika kupata mtoto. Na ndiye mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kwa sasa.

Source : M. Mahanga (Facebook)
 
Ukweli upi? Si aweke vyeti hadharani aache maneno? Then na yeye aweke vyeti vyake vya uchungaji sheinzi type, atuambie alisomea wapi uchungaji

Serikali ndio inayonafasi ya kuthibitisha ukweli wa vyeti vya bashite.pole lakini
 
Kwa dua zile za mashekhe, walakhi watu pamoja na Gwajima wajisumbua tu! Tena waliomwombea dua ni mashekhe vingunge, aaahhhh Sidhani! Kama ikatokea kelele hizi zikamletea matatisi sitozikubali tena dua!
Masheikh maslahi hizo dua hata mwisho wa bati hazikufika itakuwa mbinguni? Pale bahasha tu. Tena anatakiwa kuwa makini sana, masheikh watampiga za kichwa akitoka wanamng'ong'a
 
Jamaa amepitia wakati mgumu sana, lakini Mungu ni mwenye nguvu amempigania
 
Kama unatumia cheti cha mwingine jiondoe tu.

Kuna picha niliona mitandaoni, amelala wenzake wanasoma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…