The only person wa kumaliza utata wa hili ni ndugu Makonda mwenyewe. Lakini hebu tujiulize. Who is Makonda? si ni mwananchi kama sisi? kwa nini swala kuhusu vyeti vyake liwe big deal? I mean Mh. Rais alisema kuna uhakiki. Sasa huo uhakiki unawagusa watu gani na kuwaacha watu gani? Kwani Makonda siyo mtumishi wa umma? I mean si analipwa kwa kodi zetu? What happened to Leadership by example?
Kuna watu wanakatwa 15% ya HELSB. Kuna watu wameanikwa kwamba ni vilaza. Kuna watu wamerudishwa nyumbani wakajipange upya kwamba qualifications zao hazitoshi kuingia vyuoni. I mean hili swala limeumiza wengi. Na ni very unfair watu kuamka na kusema kwamba huyu Makonda tumuache. It is double standard ambayo itatutafuna mpaka kizazi.
Makonda should come out clean and say: Nina vyeti halali au kama hana basi arudi shule akasome. Ni kijana mdogo. Anakokwenda ni mbali kuliko alikotoka. Sioni sababu kwa nini yeye awe mgumu katika hili.
Akishindwa ku-deal na hili swala, hakika hatakuwa na moral authority ya kukemea maovu kwenye jamii yetu. Utaanzaje kukemea utendaji mbovu na vyeti feki wakati wewe ni mtuhumiwa nambari moja? Makonda atumie busara. Asi-push mpaka Rais afanye maamuzi ya hatma yake. Kama hana vyeti aombe kujiuzuru akiwa bado na credibility kwa aliye mteua then arudi shule.
Though Kiukweli, Makonda as the rising star, amempa pigo Rais wetu aliyemwamini mpaka kumsifia kwenye public. Na media (za ndani na nje) zisivyo na adabu, lazima kesho na kesho kutwa kwenye press conference ya Rais, Magufuli ataulizwa. Atajibu nini? na vita yake aliyoianzisha dhidi ya vyeti feki? In fact mpaka leo tunaambiwa mishahara haipandi kwa sababu ya watu wenye vyeti fake/hewa!
You cant simply whitewash hii kitu kwamba ni kelele za wauza madawa ya kulevya. Ni zaidi ya wivu na chuki binafsi. Makonda awajibike. Ni elimu yake. Inagusa utu wake na strggle zake kama binadamu yeyote yule. Kama hana cheti halali, basi, akung'ute kanzu yake na kurudi shule. Kama ni kusoma QT hajachelewa pia.
Masanja.