Yiyu Sheping
JF-Expert Member
- Jun 21, 2016
- 1,720
- 850
Wee jamaa mfatiliaji mzuri wa masuala na mtunzaji kumbukumbu mzuri!!! Katika kumbukumbu zako yule Kihiyo yuko wapi? Tafadhali.
Na washawasha!
Na washawasha!
Hivi unafahamu kuwa katika muda huu kuna majaji wanne, wapo kazini, huku wawili wakikabiliwa na tuhuma za kuwasaidia wauza unga na wawili wakiwa miongoni mwa waliopokea mgao wa Tegeta Escrow? Ukidhafahamu hilo huenda ukaanza kuwekeza nguvu zako katika masuala ya maendeleo yako binafsi kuliko kujipa matumaini hewa kuhusu "kutumbuliwa kwa Makonda."
Watanzania ni viumbe wa ajabu sana. Wamesahau kabisa kuwa mtu mmoja aitwaye Masauni, alilazimika kung'oka huko UVCCM kwa tuhuma za forgery/udanganyifu. Guess leo ni nani serikalini?
Prof Muhongo ni miongoni wa watu waliohusishwa na kunufaika na skandali ya Escrow. Leo ni nani?
Wale jamaa wa GSM, sote twajua walioyafanya na hatimaye "kujifilisi" only to come back with another name. Ungejua Home Shopping Centre "ilifilisika" huku inadaiwa kiasi gani, yet ni "wadau muhimu wa maendeleo kwa Awamu ya Tano" basi huenda usingepoteza muda wako kutarajia kuona "Makonda akitumbuliwa."
Tunawalipa IPTL sh milioni 400+ KILA KUKICHA ilhali sote twafahamu kuhusu hali ya Tanesco na kushamiri kwa mgao wa umeme. Talking about mgao, umeshadumu kwa miaka mingapi, na nani kawajibishwa so far "solely kwa kuchangia kudumu uwepo wa mgao wa umeme"?
Endeleeni kutarajia miujiza. Ni haki yenu kikatiba anyway!