kama umeokoka, Mungu akubariki. kwa waliookoka hiyo ni jambo la kawaida, Mungu hua anagawa vipawa, na Roho Mtakatifu huwa anaongea kwa namna mbalimbali, anaongea na huyo dada pia. binafsi wakati niko misri, mke wangu alikuwa mtu wa imani sana, hadi leo ni mtu wa imani. ilikuwa hata nikicheat, anajua, anaonyeshwa kwenye ndoto. kuna siku nimesafiri nikafanya ujinga, niliporudi akaniambia ameota ndoto ambayo anaona ni ya kimungu, akaeleza mazingira yooote sawasawa na niliyokuwa, na jinsi mwanamke yule alivyonilaghai, hadi kiasi cha pesa alfu hamsini alichochukua.
nilipokuja kuokoka, hadi leo hii, kama kuna jambo baya lipo mbele yangu, huwa nalijua, nikilala usingizi hasa mida ile ya asubuhi saa kumi na moja au kumi, huwa naoteshwa au naona kama maono kitu kilicho mbele yangu, aidha direct kabisa au indirectly kuwa na uzito kwamba kuna jambo baya limetegwa au linanikaribia, kazi sasa huwa ni kulisambaratisha kwenye ulimwengu wa roho, kama sitafanya hivyo, huwa linatokea kweli ndani ya wiki mbili, na hata nikisambaratisha huwa kufeli kwa hilo jambo kunaonekana. kwa kifupi, Mungu huwa anaongea, na akiongea kama wewe ni mtu wa Mungu utajua huyu ni Mungu na huyu sio MUngu. kuna ndoto za ugali tu umeshiba, ndoto za mambo uliyofikiria mchana au yaliyojaa kichwani mwako, ila kuna ndoto za Mungu kabisa, anakuonyesha, na ziko tofauti, zile za Kimungu ni kama mhuri umegongwa, zina upako wake haufutiki, mimi kuna ndoto nilioteshwa mwaka 2000 nikionyeshwa na kundi la malaika wakiimba wimbo, hadi leo huwa siisahau hadi huo wimbo upo kichwani hadi leo.
Yohana 10:27 inasema, Kondoo wangu waisikia sauti yangu, nami nawajua, nao wanifuata. Nami nawapa uzima wa milele, wala hawatapotea kamwe, wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.
Yoel 2:28 Hata itakuwa baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili na wana wenu waume kw awake watatabiri na wazee wenu wataota ndoto na vinana wenu wataona maono.
Yohana 10:5 Yesu alipokuwa akiongelea kondoo wake alisema, Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni.
kwa ninyi ambao hamjaokoka, hayo ndiyo marupurupu ya wokovu (mojawapo tu, yapo mengi), wakati wengine wanahangaika kupambana kimwili sisi Mungu ameshatuonyesha rohoni nini kinakuja, tunapiga magoti tunasambaratisha kwa Jina la Yesu, wewe huku nje unapambana na sisi kimwili au kwa kutumia wanadamu, utashindwa na tunajua mwisho wako hata kabla haujaufikia. vita vyetu ni vya rohoni. pia Mungu huwa anaongea nasi kwa maono na ndoto, just to mention a few.
Yesu anasema, kondoo wake wanaijua sauti yake, wanamfahamu, wapo wachungaji wengi wana discourage kwamba ndoto huwa sio za kimungu, NO, zipo za kimwili na za kishetani, ila zipo za Mungu kabisa, na wale walio na Mungu moyoni wataijua sauti ya Mungu, hautakuwa na haja kwenda kuuliza kwa mtu tafsiri yake or whether hii ni ndoto ya Mungu au sio? hautauliza kwasababu jambo la kimunguni dhahiri na lina amani ya Kristo na utaona kama linasema moyoni kabisa kwa ule utamu wa Roho Mtakatifu, automatically utatafsiriwa na utaijua kuwa hii ni sauti ya Mungu na hii ni sauti/ndoto ya adui. ziko tofauti kabisa. ndio maana Yesu alisema kondoo wake wanaijua sauti yake, akiongea Yesu utajua huyu ni Yesu kama wewe ni kondoo wake, na akiongea mwizi utajua huyu sio Yesu kama wewe ni kondoo wa Yesu.