Mchumba ninayekaribia kumuoa simuelewi

kwanza mie sio mtoa mada halafu sio me.vilevile hujajua raha ya ndoa ni pamoja na kutimiza majukumu na wajibu sidhani kama kuna mtu anayemfurahia mtu mchafu na mvivu

Ok ok, Lakini unadhani hicho ni kigezo tosha kumuacha huyo mwanamke?
 
Kwa sasa hatuishi wote maana tuko kwenye michakato ya ndoa lakini mara kadhaa anakuja na kukaa siku mbili tatu.

Kusema ukweli mimi nafanya almost vitu vyote, kwa mfano nina uhakika hajawahi kuosha vyombo!! Tukishakula(hata kama ni chips) ataacha sahani chafu mezani na kukaa sebuleni moviez. Either mimi nitoe na kupeleka kwenye sink au na mimi niache.

Mara nyingi napenda kukaa zangu chumbani au kwenye computer tu maana ananikera.

Aiseee...pole sana.kweli upo kwenye dilema.
 
Hakyanani mkuu kweli naona umekereka sana...Raha ya nyumba mwanamke awe msafi na mchapa kazi.

Na raha ya mwanaume sio kutegemea mshahara wa mke!... nakubaliana na habari ya mwanamke kuwajibika lakini kunawakati inaangaliwa tofauti, let us be fair we also have our own weaknesses
 
unajua shida ya kuishi na jitu lenye maneno ya kejeli wewe? Mbona mwenzio anakuvumilia na udhaifu wako?

Ukitaka mwanamke/mwanaume perfect muumbe wa kwako, la sivyo maisha ni kuvumiliana.....

Kuhusu kufua simple si wote mna kazi changeni laki nane nane mmnunue mashine ya kufulia....

Zungumza nae kuhusu kupika (ila mmmh huyo nae uvivu kapitiliza hata kupika??????) je anarudi amechoka sana?

Kama kuna wanawake watu wazima kwao zungumza nao, waketi nae na kumfundisha majukumu ya mke kwenye nyumba.....

Na kama mna uwezo wekeni house girl, maana kumbuka wewe unafanya kazi yeye anafanya kazi, mkirudi ofisini wewe unachukua remoti na yeyeaingie jikoni kupika, aoshe vyombo, asafishe nyumba, uwanja, apige pasi mwisho ya siku atachoka ashindwe kukupa unyumba urudi hapa na thread mpya......

Swali la nyongeza, mnaporudi ofisini unamsaidia kazi? Au wewe miguu juu mwenzio ahenyeke?

WELL SAID.. I SALUTE!:israel:
 
mkuu, watu wote hawapo sawa! sasa unataka kuniambia asiyejua kupika au kufua haolewi? halafu nani amuoe? we mwenyewe ushasema unadharau, hasira nk nk... unadhani nani anapenda kuolewa na mtu mwenye tabia kama zako??? Hapo hamna cha dini wala nini, ingekua unafuata dini basi wewe unatakiwa kula kwa jasho na yeye atulie nyumbani kukufulia nyumba kubwa , Blaki Womani
Elia hapa tunazungumzia uchafu na uvivu na sio swala la kupika au kufua.....malezi mengine tunajidanganya pale unapolea watoto wako hawajui kufua wala kupika ni kuwaweka matatizoni hapo baadae tena haswa binti khaaaa mwanamke shurti ujishughulishe kidogo sio kila kitu kufanyiwa na hg/hb au machine na wanaume wanapenda kuona mkewe anajishughulisha/kupika japo mara moja moja na kufurahia pishi lake
 
Last edited by a moderator:
Kwa sasa hatuishi wote maana tuko kwenye michakato ya ndoa lakini mara kadhaa anakuja na kukaa siku mbili tatu.

Kusema ukweli mimi nafanya almost vitu vyote, kwa mfano nina uhakika hajawahi kuosha vyombo!! Tukishakula(hata kama ni chips) ataacha sahani chafu mezani na kukaa sebuleni moviez. Either mimi nitoe na kupeleka kwenye sink au na mimi niache.

Mara nyingi napenda kukaa zangu chumbani au kwenye computer tu maana ananikera.

Hapa nimekuelewa zaidi na yeye nimemuelewa.... For those few days you can't jump to conclusion kwamba ni mchafu ama mvivu... count the positives and the negatives then see for yourself what to do!
 
Elia hapa tunazungumzia uchafu na uvivu na sio swala la kupika au kufua.....malezi mengine tunajidanganya pale unapolea watoto wako hawajui kufua wala kupika ni kuwaweka matatizoni hapo baadae tena haswa binti khaaaa mwanamke shurti ujishughulishe kidogo sio kila kitu kufanyiwa na hg/hb au machine na wanaume wanapenda kuona mkewe anajishughulisha/kupika japo mara moja moja na kufurahia pishi lake

Umenena..
 
Last edited by a moderator:
Elia hapa tunazungumzia uchafu na uvivu na sio swala la kupika au kufua.....malezi mengine tunajidanganya pale unapolea watoto wako hawajui kufua wala kupika ni kuwaweka matatizoni hapo baadae tena haswa binti khaaaa mwanamke shurti ujishughulishe kidogo sio kila kitu kufanyiwa na hg/hb au machine na wanaume wanapenda kuona mkewe anajishughulisha/kupika japo mara moja moja na kufurahia pishi lake
Ninacho pingana sana na mtoa maada ni kuona hili tatizo kwamba ni kubwa sana! ninamfano wa dada mmoja(shemeji yangu) alikuwa na sifa kama hizo.. lakini leo hii ana miaka mi5 ya ndoa na tatizo la sijui kujua kupika, kufua nk nk.. ni hadithi.. kikubwa lazima utake kujua kwanini ni mvivu mambo mengine ni makuzi tu na utoto... akipigwa kicheni part tu kwishneey.. anarudi kwenye mstari.... matatizo madogo hayo B.W
 
Pole kaka. Huyo angemfaa Elia maana bora angekuwa na tabia za kibeijini kila mtu aoshe chake (ingawa nayo si tabia ya mke) sasa yeye anataka umwoshee na chake???

SIsi hatukujuhi kuwa kama ukimwacha labda utaoa wadogo zetu tufaidike...au tunamuonea wivu huyu mamaa....lakini nakwambia tatizo ka uvivu, uchafu na ujeuri halitakuwa tatizo lako pekee litakuathiri kisaikolojia kwenye ndoa yako kwani hutajisikia kupata wageni; watoto wako hawataisha kuharisha na ma UTI, hutataka kukaa nyumbani...utakuwa unashinda bar; marafiki na ndugu watakuwa wanakucheka.

Hivyo hatuongei kwa ushabiki...tunakutakia mema...JF ipo na itaendelea kuwepo...utaja tuambia kuwa tulikuwa watabiri.

Hatukatai kuwa hawa wachafu hawaolewi...ila wengi wanawaoa kwa kuingi mkenge...na kwa kuwa ndoa si rahis kuvunja...wanaishi nao tu..sasa wafanyeje na ni too late. Wewe umejua...ukishindwa kuamua utaja jilaumu siku za usoni.

Kwa sasa hatuishi wote maana tuko kwenye michakato ya ndoa lakini mara kadhaa anakuja na kukaa siku mbili tatu.

Kusema ukweli mimi nafanya almost vitu vyote, kwa mfano nina uhakika hajawahi kuosha vyombo!! Tukishakula(hata kama ni chips) ataacha sahani chafu mezani na kukaa sebuleni moviez. Either mimi nitoe na kupeleka kwenye sink au na mimi niache.

Mara nyingi napenda kukaa zangu chumbani au kwenye computer tu maana ananikera.
 
Mimi naona hii ni case tofauti...huyo alikuwa hajuhi kazi...huyu anajua...ndio maana mdau kasema anapika akiwa kwenye mood; Ila kula hakuna mood ujue; na hatujuhi anakuwa na mood mara ngapi kwa wiki, mwezi au mwaka?

Sasa huyu unataka kumfundisha umfundishe nini na kila kitu anajua ila HATAKI.


Lakini hata hao the so called "hawajuhi kazi za ndani" mi naona wanachekesha na wala si wa kuwahurumia. Wamekulia dunia gani ambako unaweza ukafika 20-25 years bila kujua kupika...Hata kaka zangu walolelewa ki mfumo dume wanakaangiza kama hawana akili nzuri; na mila zetu mwanaume haruhusiwi kupika.

Ninacho pingana sana na mtoa maada ni kuona hili tatizo kwamba ni kubwa sana! ninamfano wa dada mmoja(shemeji yangu) alikuwa na sifa kama hizo.. lakini leo hii ana miaka mi5 ya ndoa na tatizo la sijui kujua kupika, kufua nk nk.. ni hadithi.. kikubwa lazima utake kujua kwanini ni mvivu mambo mengine ni makuzi tu na utoto... akipigwa kicheni part tu kwishneey.. anarudi kwenye mstari.... matatizo madogo hayo B.W
 
Ninacho pingana sana na mtoa maada ni kuona hili tatizo kwamba ni kubwa sana! ninamfano wa dada mmoja(shemeji yangu) alikuwa na sifa kama hizo.. lakini leo hii ana miaka mi5 ya ndoa na tatizo la sijui kujua kupika, kufua nk nk.. ni hadithi.. kikubwa lazima utake kujua kwanini ni mvivu mambo mengine ni makuzi tu na utoto... akipigwa kicheni part tu kwishneey.. anarudi kwenye mstari.... matatizo madogo hayo B.W

nimtakie kila la heri mtoa mada huyo mke mtarajiwa abadilishwe na kitchen part kama hatabadilika atajamsikia mumewe kwenye radio.....
 
Mimi pia nina mapungufu yangu kama vile ni mkali sana, pia nina maneno ya kukejeli(wengine wanasema dharau), but mara nyingi nakuwa open sana sio mtu wa kuficha ficha.

Je nifanyeje? Binti nampenda, napenda niishi nae ila kwa style hii nyumba si itawaka moto?!

Ushauri

@nymba kubwa Hebu tusimuangalie huyo dada tu ona tabia za huyu jamaa kama tuna tegemea wageni watoto na kuishi vizuri na watu nadhani wote wana mapungufu na wanahitaji ushauri wa kina
 
Mimi naona hii ni case tofauti...huyo alikuwa hajuhi kazi...huyu anajua...ndio maana mdau kasema anapika akiwa kwenye mood; Ila kula hakuna mood ujue; na hatujuhi anakuwa na mood mara ngapi kwa wiki, mwezi au mwaka?

Sasa huyu unataka kumfundisha umfundishe nini na kila kitu anajua ila HATAKI.


Lakini hata hao the so called "hawajuhi kazi za ndani" mi naona wanachekesha na wala si wa kuwahurumia. Wamekulia dunia gani ambako unaweza ukafika 20-25 years bila kujua kupika...Hata kaka zangu walolelewa ki mfumo dume wanakaangiza kama hawana akili nzuri; na mila zetu mwanaume haruhusiwi kupika.

ukimfuatilia jamaa wala haishi na huyo mwanamke sasa kamsoma saangapi?
 
sijasema kwamaa amuache yeye anakaa naye anamjua vizuri tabia maamuzi ni juu yake lakini siyo siri namchukia mtu mvivu na mchafu hasa wasichana
 
ukimfuatilia jamaa wala haishi na huyo mwanamke sasa kamsoma saangapi?

Muda mchache ambao ninakuwa nae, mambo anayoyafanya ndio yamenifanya nitafute ushauri. Pia ni stage tuliyopo kwa sasa ya kuelekea kwenye ndoa.
 
Kaka hata mimi nipo kama wewe,ila ni kawaida kwa wanaume wasafi kuwa namna hiyo na hasa ukikutana na mwanamke mchafu na mvivu,anakera sana.me naona hakuna cha kukushauri maana unalijua tatizo na uamuzi tayari unao,sema unaogopa tu kuutekeleza kwa kuhofu utachukuliwaje..we tekeleza unachoona ni sahihi kwako.

Hapo umenena mkuu
 
kwa huyo jamaa na tabia zake kwa vile anazitambua na muda mwingine anaweza ku zicontrol anaweza kujirekebisha imagine hao watoto watapata mafunzo gani ikiwa mwenendo wa mama ndo upo hivyo.tusiwe na jumuisho la kusema wataweka wasaidizi.je ni msingi gani utamwekea mtoto wa kuweza kuishi na watu zaidi ya wazazi in case of their absence malezi ni kitu muhimu sana ambayo humjenga mtoto toka utoto huku aki copy maisha ya walezi fikiria endapo atapata watoto wa kike yeye kama mama ni msingi gani atakao waachia
 
Kumkosoa ninaweza. Nitakaa nae chini kiupole kumuelezea tena maana nilishakaa nae chini ila nikatumia lugha kali sana. Ila asipobadilika ataniweka kwenye wakati mgumu sana maana nakereka mno.

Mi naona wewe ndo unashindwa kumrekebisha

Hapo kwa red ndo unapokosea kabisa ndg yangu, ukishatumia lugha kali kwa mwanamke unampanikisha kisha anajenga woga kupita kiasi.

Tatizo pia umeishamjengea mazingira kuwa hizo kazi unazifanya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom