Mchumba ninayekaribia kumuoa simuelewi

Mchumba ninayekaribia kumuoa simuelewi

Nna shaka Hata Game...utakuwa mpaka ubembeleezee...shaka ondoa kama. Unampenda ..mwekee Dada wa kazi huku unamfundisha jinsi ya. Kuishi na watu.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Yaani madudu yote hayo USHAURI wa nini?? Something wrong in your brain... JITAMBUE Mwanaume...

Kuomba ushauri si jambo baya. Je unadhani siko katika dilemma mpaka nifikie hatua hii!? Labda nikuulize, unanishauri nini?
 
jaribu kufanya uchunguzi baba na mama yake wanaishije! unaweza kukuta mama yake ndivyo anavyo-mtreat baba yake na kama ni hivyo hataacha atakusumbua.Ningekuwa naoa leo hili ni jambo muhimu ningelifanyia kazi vyema, hawa wanawake wanaweza ukuharibia maisha ukajuta ukatamani ulivyokuwa unaishi kisela.
 
Miaka mitano ni mingi kikubwa kaa chini na kuorodhesha weakness zake against strength kisha unapima mwenyewe kuona mzani unaangukia kwingine huku ukifanya cost - benefit analysis kwa kuangalia gharama ya kumwacha huyo mrembo wako against gharama ya kumpata mchumba mwingine pia unaangalia je ukimpata mwingine akawa anajua kupika na kazi zingine za ndani alafu akawa na mapungufu mengine itakuaje (assuming anakula tunda nje). Nimekupa tafakuri tu mambo mengine unaamua mwenyewe kwani mie ninaamini binadamu ni SUBJECT TO CHANGE hivyo hata wewe kutokana na kuishi na watu mbalimbali kuna vitabia flani ulikuwa navyo vimeondoka na rafiki zako wengine pia wamejifunza toka kwako (exposure sio kufika Nairobi au London bali hata kama kujifunza vitu vya kawaida tu katika maisha yetu nayo ni exposure, hivyo pima mwenyewe uone kama kuna uwezekano wa hayo matatizo kuondoka in the near future), kwa kuwa wewe i muwazi nadhani mtakaa chini na kujadili kwa kina hatima ya maisha yenu kwani mtaendelea kula chips (KWENYE MAHUSIANO WAKATI MWINGINE WATU HUWA HAWAPO REAL ILA UKIFUATILIA BACKGROUND YAKE UNAKUTA UGALI ALIKUWA ANAUKANDAMIZA KAMA KAWA). Cheki pia alternatives alizokupa Kaunga maana kila mtu amelelewa katika mazingira flani ambayo huwezi kumbadilisha kwa siku moja hivyo ukute mwenzako amekulia mazingira ya mdada wa kazi na vitu kama hivyo jaribuni ku-hire mtu wa kufanya baadhi ya kazi za nyumbani.

Nje ya mada hapa: SWALI KWAKO MLETA THREAD, KWANI WANAUME WANAOA ILI WAPIKIWE NA KUFULIWA? KAMA NI KUFULIWA MBONA KUNA MADOBI NA KAMA KUPIKIWA MBONA KUNA MAMA/BABA LISHE? NI NINI HASA KINACHOFUATWA KWENYE NDOA? (EMBU TUTAFAKARI KWA PAMOJA HAPA)
 
Last edited by a moderator:
WanaJF ma great thinkers,

Nimefanikiwa kuongea na mchumba wangu nikiwa ''CALM" na ningependa nishare tena nanyi kwa yaliyojiri;

Tumeongea taratibu, tukiwa wote hatuna tension(especially mimi ambaye dakika moja tu nakuwa mkali), nikagundua vitu kadhaa sababu ya kuongea kwa upole na lugha laini.

Kuhusu kupika
Binti anapenda kupika lakini mara chache anajisikia kama kauvivu. Ni kwasababu hatujakaa sana wote kwa muda mrefu(max ni 3-4 days) but anapenda na atajirekebisha kwenye hilo. Angependa sana tuwe tunashirikiana kama ikiwa weekend(ambayo mimi nilishaafiki maana sikuwa najua kupika), so nami pia najifunza.

Kuhusu moviez
Ni kweli anapenda kuangalia moviez, hiyo inatokana na kuwa idle kwa kipindi fulani(likizo) lakini kwa jinsi tulivyoongea atahakikisha mengine yanapewa priority

Uvivu
Ameadmit anahisi uvivu ila anahisi ni kwa namna alivyolelewa maana walikuwa wanapewa kila kitu. Mara nyingi nikimfokea anajisikia vibaya na kuniogopa but atabadilika

Kutokufua
Hii inaunganishwa na uvivu ila atajirekebisha

Kujibu, jeuri na kisirani
Mara nyingi approach yangu inamuoffend na nikagundua kumbe asiponijibu(nawaza kama ananidharau), kumbe mimi ndiye namfanya ajibu. Ila tukiongea nikiwa calm, anasikiliza na anaheshimu.

Kisirani na kuamua kukaa kimya kwa muda, anahisi nikikasirika nahitaji muda wa kucalm down, so anafanya hivyo ili kunipa nafasi nitulie. Ameadmit ataacha.

Hitimisho
Kusema ukweli huyu binti tunajuana sana. Kikubwa ambacho naona kimejenga tabia ambazo zinaweza kubadilika ni malezi na MIMI mwenyewe approach yangu kwake.

Nimeamua kutafuta consultation/kusali etc namna ya kutokukasirika na kupanic. Jana tumeongea mambo mazito, makubwa mno ambayo siwezi kuandika mengine(personal sana) but in open and calm way. I'm happy.

Yeye atakuwa karibu na rafiki yake ambaye ameingia kwenye ndoa muda kadhaa kujaribu kumshauri namna ya kuhandle situations, namna ya kutake care husband etc. Ukikaa na mtu unayempenda utaona kasoro, lakini kasoro ndio challenges. Nobody is perfect.

Mipango ya harusi inaendelea. Nitarudi tena kwa ushauri. Mbarikiwe
 
Nje ya mada hapa: SWALI KWAKO MLETA THREAD, KWANI WANAUME WANAOA ILI WAPIKIWE NA KUFULIWA? KAMA NI KUFULIWA MBONA KUNA MADOBI NA KAMA KUPIKIWA MBONA KUNA MAMA/BABA LISHE? NI NINI HASA KINACHOFUATWA KWENYE NDOA? (EMBU TUTAFAKARI KWA PAMOJA HAPA)

Hapana lakini ningependa mke akiwa responsible kwenye mambo ya usafi/upishi. House girl anakuwa supportive especially tunavyobanwa na kazi. Mimi ningependa mfano weekend tunafua na kupika wote!
 
Hapana lakini ningependa mke akiwa responsible kwenye mambo ya usafi/upishi. House girl anakuwa supportive especially tunavyobanwa na kazi. Mimi ningependa mfano weekend tunafua na kupika wote!

Ok hapo sawa mdau, maana kumwachia kila kitu house girl nae si vizuri lazima kushughulika mwanamama nae ajaribu kama hawezi basi hata kuwa risasi kidole kwa kumwonyesha nini anataka
 
tabia ya mtu ya kila siku ikikusumbua, ni kosa lako mwenyewe na si mwenye tabia husika, ukishafahamu mwenzako yukoje jifunze kuishi naye........step ya kwanza ni kutambua madhaifu yake, step ya pili ni kuyakubali....step ya tatu ni kutafuta mbadala wa mapungufu hayo...ambayo tayari umeupata, kwa kuwa umesema hapo, kuwa unafagia, unafua nk.....TATIZO lako kubwa ni kuwa uimeruka step ya pili...........kama una nia ya kufunga naye pingu za maisha, na kweli unampenda...nakushauri kubali mapungufu ya mwenza wako...na ingia naye kwenye ndoa, IF naye anakupenda kama au zaidi ya umpendavyo.........for more advise on the matter of relationships and marriage...inbox me.....kwa wanaJF natoa ushaur bure............
 
kaka kwa maelezo yako hamtafika mbali.kama umeshindwa kumbadirisha kwa iyo miaka 5 huyo ni vigumu kubadirika.Nakushauri husitoe mahali kwanza ili umpatie kipindi cha kujirekebisha.ni ayo tu.
Naomba ushauri wenu. Nina mchumba wangu tumekaa muda mrefu kama miaka 5 hivi. Sasa tumeona ni muda muafaka wa kuoana. Kipindi kirefu cha uhusiano wetu hatukuwa tunaishi pamoja as yeye alikuwa anasoma mkoa mwingine nami mwingine. Lakini hii haikupunguza mapenzi yetu maana tulikuwa tunawasiliana na kutembeleana mara kwa mara.

Sasa alimaliza chuo na kuanza kazi, na mimi pia nina kwangu. Tukawa tuko close zaidi na siku moja moja tunakaa pamoja nyumbani. Hili kufanya mambo yaende kwa heshima, tukafikia hatua ya kutambulishana kwa wazazi rasmi na kuanza kujipanga kwa ajili ya mahari na ndoa

Kuna tabia ambazo nimezigundua zinanikera na ninaomba ushauri.

1. Huyu binti ni mvivu
Anapenda kukaa kuangalia moviez tu. Moviez, kuchat thats it. Nyumba chafu nasafisha mwenyewe. Kila kitu kipo ndani(jiko, chakula), hataki kupika eti mpaka awe kwenye mood kwahiyo tunaishia kula chips. Nguo zangu chafu(hata za kwake) kufua ugomvi.

2. Kisirani
Mtu wa visirani, kujibu, kununa.

Sasa tunaelekea kwenye mahari lakini kichwa changu kinawaka moto. Hivi tu kwenye ndoa bado, tukiwa ndani ya ndoa si itakuwa balaa?

Mimi pia nina mapungufu yangu kama vile ni mkali sana, pia nina maneno ya kukejeli(wengine wanasema dharau), but mara nyingi nakuwa open sana sio mtu wa kuficha ficha.

Je nifanyeje? Binti nampenda, napenda niishi nae ila kwa style hii nyumba si itawaka moto?!

Ushauri
 
kaka kwa maelezo yako hamtafika mbali.kama umeshindwa kumbadirisha kwa iyo miaka 5 huyo ni vigumu kubadirika.Nakushauri husitoe mahali kwanza ili umpatie kipindi cha kujirekebisha.ni ayo tu.

KWa bahati mbaya au nzuri sana mawazo mengi na ushauri nilipewa na wadau humu JF etc. Baadhi walinishauri kujiangalia kwanza mwenyewe(mimi) na kweli kabisa nilifanya yafuatayo;

1. Niliamua/Nilipigania(to fight) kuacha hasira, maneno makali na kuwa msikivu kwake. Niliongea nae nikiwa calm na kumuelezea namna ninavyojisikia. Hii ilisaidia sana maana kweli hakuwa hivyo, inaonekana nilivyozidi kuwa mkali kwake na yeye ndio akazidi kuwa defensive.

2. Tuliendelea na plans za mahari na tayari nimekwishamposa. Kusema ukweli kwa jinsi tunavyofahamiana na huyu mchumba wangu, 70% mimi nilisababisha awe hivyo.

3. Kupitia ushauri ambao pia alisoma hii thread na kuona namna mlivyojaribu kutusaidia/kutushauri, alifurahi na kuona kweli nimedhamiria kuwa nae.

4. Kupika anapika(kwa sasa mara nyingi anakuja weekend), so katikati ya wiki kuna dada nimemuajiri ananipikia(mnajua mambo ya kazi kutoka usiku kuondoka asubuhi).

5. Calmness and openness imeokoa vingi sana.

Sio kwamba naongeza chumvi kwa mchumba wangu, lakini natamani mngeona namna nilivyoacha ukali na kuongea kwa jeuri ilivyosababisha awe the most beautiful thing ever.

Naandaa kadi za michango sasa,,,,,, nitawaletea
 
tabia ya mtu ya kila siku ikikusumbua, ni kosa lako mwenyewe na si mwenye tabia husika, ukishafahamu mwenzako yukoje jifunze kuishi naye........step ya kwanza ni kutambua madhaifu yake, step ya pili ni kuyakubali....step ya tatu ni kutafuta mbadala wa mapungufu hayo...ambayo tayari umeupata, kwa kuwa umesema hapo, kuwa unafagia, unafua nk.....TATIZO lako kubwa ni kuwa uimeruka step ya pili...........kama una nia ya kufunga naye pingu za maisha, na kweli unampenda...nakushauri kubali mapungufu ya mwenza wako...na ingia naye kwenye ndoa, IF naye anakupenda kama au zaidi ya umpendavyo.........for more advise on the matter of relationships and marriage...inbox me.....kwa wanaJF natoa ushaur bure............

Asante sana mkuu kwa ushauri. Nafanyia kazi!
 
Hakuna kitu kilichonifurahisha kama self analysis yako na kukubali mapungufu.
You are one step ahead, ninakushauri kaa mjadili bila kutumia ukali; make her reason with you na especially hiyo ya kula junk food. Lakini kama wote ni wafanyakazi, mnaweza kuhire a help, mtu akawa anakuja anafanya usafi na kufua at least 4 times a week, huku mkijipanga jinsi ya kujitegemea.

Nina uhakika sababu ya kumpenda ni zaidi ya kuwa mfanyakazi wa nyumbani; hivyo basi, hizo shughuli mjadiliane zitafanyika vipi coz lazima zifanyike; mwambie aje na suggestion.
Kaunga you are the most wise woman i have met.

mtoa mada hivi kwani at first ulimpendea nini? je ulichofikiri kwamba ni sababu ya kumpenda bado kipo ama hakipo? Pia hili swala la mtu kisirani nazid kuliona tena hapa jamvii hivi huyu ni mtu wa namna gani hadi aitwe kisirani?

ushauri wangu kwako ingawa nataka majibu ya maswali yangu, ongea nae akwambie yeye anafikir kazi za ndani mtazimudu vipi hilo la kwanza, pia mweleze kuna wakati mama anakuwa more than busy ndani nyumba hasa anapokuwa na mtt mchanga hata kama kuna msaidizi but kuna kazi ambazo lazima azifanye yeye kama mama na kama mke je kwa uvivu alio nao atamudu? akiuliza kazi gan mwambie kazi ya kunyonyesha mtoto na kumnyonyesha baba atamudu kama ni mvivu?
 
Last edited by a moderator:
Hapana lakini ningependa mke akiwa responsible kwenye mambo ya usafi/upishi. House girl anakuwa supportive especially tunavyobanwa na kazi. Mimi ningependa mfano weekend tunafua na kupika wote!

"Tigga Mumba" ni kati ya hadithi nilizotokea kuzipenda mno,ni vema ujitaidi kuwa mvumilivi kama yeye...
 
WanaJF ma great thinkers,

Nimefanikiwa kuongea na mchumba wangu nikiwa ''CALM" na ningependa nishare tena nanyi kwa yaliyojiri;

Tumeongea taratibu, tukiwa wote hatuna tension(especially mimi ambaye dakika moja tu nakuwa mkali), nikagundua vitu kadhaa sababu ya kuongea kwa upole na lugha laini.

Kuhusu kupika
Binti anapenda kupika lakini mara chache anajisikia kama kauvivu. Ni kwasababu hatujakaa sana wote kwa muda mrefu(max ni 3-4 days) but anapenda na atajirekebisha kwenye hilo. Angependa sana tuwe tunashirikiana kama ikiwa weekend(ambayo mimi nilishaafiki maana sikuwa najua kupika), so nami pia najifunza.

Kuhusu moviez
Ni kweli anapenda kuangalia moviez, hiyo inatokana na kuwa idle kwa kipindi fulani(likizo) lakini kwa jinsi tulivyoongea atahakikisha mengine yanapewa priority

Uvivu
Ameadmit anahisi uvivu ila anahisi ni kwa namna alivyolelewa maana walikuwa wanapewa kila kitu. Mara nyingi nikimfokea anajisikia vibaya na kuniogopa but atabadilika

Kutokufua
Hii inaunganishwa na uvivu ila atajirekebisha

Kujibu, jeuri na kisirani
Mara nyingi approach yangu inamuoffend na nikagundua kumbe asiponijibu(nawaza kama ananidharau), kumbe mimi ndiye namfanya ajibu. Ila tukiongea nikiwa calm, anasikiliza na anaheshimu.

Kisirani na kuamua kukaa kimya kwa muda, anahisi nikikasirika nahitaji muda wa kucalm down, so anafanya hivyo ili kunipa nafasi nitulie. Ameadmit ataacha.

Hitimisho
Kusema ukweli huyu binti tunajuana sana. Kikubwa ambacho naona kimejenga tabia ambazo zinaweza kubadilika ni malezi na MIMI mwenyewe approach yangu kwake.

Nimeamua kutafuta consultation/kusali etc namna ya kutokukasirika na kupanic. Jana tumeongea mambo mazito, makubwa mno ambayo siwezi kuandika mengine(personal sana) but in open and calm way. I'm happy.

Yeye atakuwa karibu na rafiki yake ambaye ameingia kwenye ndoa muda kadhaa kujaribu kumshauri namna ya kuhandle situations, namna ya kutake care husband etc. Ukikaa na mtu unayempenda utaona kasoro, lakini kasoro ndio challenges. Nobody is perfect.

Mipango ya harusi inaendelea. Nitarudi tena kwa ushauri. Mbarikiwe


hongera sana kaka,sasa umeshapata mc?mc nipo hapa kiongozi!
 
kaka ndoa haijalibiwi . fikir kabla ya kutenda

Ni kweli mkuu,huyu kashahisi harufu ya kukosa ndoa,ndio anajidai atajirekebisha,kiongozi mtoa mada uvivu ni kama ulemavu tu ambao kuondokana nao ni ishu kubwa sana,nachokushauri nimegundua unampenda sana mwanamke wako,so usijifariji kama atabadilika,nakuhakikishia utarudi tena humu kuomba ushauri,wakati huo ukiwa umeshamuoa,cha kufanya kubali tu hayo mapungufu yake na uangalie jinsi ya kukabiliana nayo na usitegemee mabadiliko ya moja kwa moja ukarelax ndoa itakushinda.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom