Mchumba mchaga ,msomi jamani naomba ushauri

Mchumba mchaga ,msomi jamani naomba ushauri

jamani mimi ni kijana mwenye miaka 27 mwenyeji wa mkoa wa shinyanga muda wa kuoa naona umekaribia nikiwa masomoni nilimpata mchumba binti wa kichaga ana degree lakini nyumbani wanataka nioe kwetu usukumani na awe std vii wana jamvi nifanyeje?

Maneno ya Mama ni dhahabu hayatupagwi.

Anyway, Jiandae kuulizwa kila siku umeingiza shilingi ngapi.?
 
Achana na chaga,Oa mdengereko wa ngomani, chaka Hawezi cheza makandawira inawene)
 
kifo hakiko mbali na wewe,halafu chonga jeneza lako mapema maana usije tusumbua
 
heading na kilichopo ndani haviendani......

hufai kuitwa baba nashangaa huyo msomi wa kichaga umempateje....

mwanaume wa ukweli anakuwa na maamuzi sahihi juu ya maisha yako....

lazma uwe na misimamo na desion making....

mamako ndo anaoa/??
 
Huyo mchaga hachelewi kukupumzisha kwa amani ukipata hela.
 
jaribu kukaa chini na wazazi wako uwaeleweshe,wakupe nao reasons kwanini hawamtaki uyo mchaga, wanaeza kuwa na point ambayo itakuingia akilini, otherwise listen to ur heart but take your brain with you..
 
Tatizo lenu mnajiona mmesoma sana na kudharau wazazi wenu, hebu muulize mzazi sababu za kukataa ni nini na uone kama zina logic kisha ukiona ni suala la hulka basi jaribu kusema naye taratibu, kwa vyovyote vile msilete uzungu kwa masuala haya yenye historia na tamaduni, kumbuka unaunganisha koo hapo na wanaouliza unaoa wewe au unaoa ukoo hawajui kuwa pamoja na kuwa mke ni wako lakini anakuwa sehemu ya jamii unayomleta na wao anakuwa ndugu yao, sasa ukileta jeuri tu ukasema maisha ya kisasa mama amezeeka au amepitwa na wakati, angalia urembo na mnato wa huyo unayemuita mchaga then puuzia wazazi then utarudi kutupa report hapa. Wengine wanachangia hata ndoa hawaijui hata hawajawahi kuwa na mahusiano yanayozidi wiki moja. Changanya na zako ila at the very end mwamuzi ni wewe, kikubwa hekima na umtangulize Mungu.
 
kaka swala la kuwasikiliza wazazi ni la muhimu sana wani wao ndio wanaoukujua tokea ukiwa mdogo nini kinakufaa na nini ukiepuke..lakin pia hauwezi kuulazimisha moyo wako kuwa na mtu ambaye ujampenda kwani chochote chaweza kutokea kama kutokuwa na maelewano mazuri ndani ya ndoa na kuwa na nyumba ndogo ambaye umempenda na kuleta madhala katika familia..
cha msingi kaa na wazazi wako waeleweshe mtazamo wako kwani wewe ndo utakaye oa na kutunza hiyo familia .
kumbuka mke ni kifungo cha maisha wakati yanakukuta mabaya wao hawatakuwepo ni wewe utakaye hangaika.
pia jalibu kuwatafuta wazee ambao wazazi wako wanawaheshimu hata viongozi wa dini unayoamin watakusaidia.balaka za wazaz ni muhimu katika maisha kamwe usilete kibuli juu yao kuwa mpole watakuelewa.
nakutakia mema mkuu naimani utafanikiwa kuwa na yule umpendae.
 
hatupo tayari kunyanyasika huu ni ujinga miaka 52 ya uhuru unaendekeza ukabila kwani wanataka kutambika

Sio ukabila. Ni muhimu kuelewa kuwa ridhaa inahusika na pia ni uongo kuwa kuna baadhi yenu huua waume zao hasa wakiwa na mali? Bisha!
 
Sio ukabila. Ni muhimu kuelewa kuwa ridhaa inahusika na pia ni uongo kuwa kuna baadhi yenu huua waume zao hasa wakiwa na mali? Bisha!

kutegemeana na mwenendo wako mkuuu... na hiyo ni individual heart and not society mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom