JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 6,833
- 14,193
Habari wakuu,jamani naomba kufahamishwa jambo moja linalo nisumbua kichwa changu,
kuna binti mmoja mwenyeji wa kilimanjaro,nina mpenda sana na tumepeana ahadi ya kuishi pamoja katika maisha ya ndoa,
Tatizo ni kwamba ameniambia kwamba siwezi kwenda kwao kujitambulisha mpaka kwanza nimpeleke yeye kwetu,sababu anayonipa ni kwamba
kwao wapo mabinti watano,na baba mkwe yaani baba yake anawataka binti zake kwanza wapafahamu nyumbani kwa vijana wanaowapenda kabla hawaja waleta kwake ili atoe idhini michakato mingine iendelee.
sasa wakuu naomba kujuzwa hizi ni taratibu za wenzetu wachaga,au vp nisije kuwa napigwa changa la macho,
kwa wababa wenye mabinti je huo ni utaratibu ambao mwaweza kutumia ili kujilidhisha kwamba kijana anayeletwa na binti zenu ni muoaji au.
Mpenzi wangu bado yupo masomoni anahitimu mwezi wa saba
kuna binti mmoja mwenyeji wa kilimanjaro,nina mpenda sana na tumepeana ahadi ya kuishi pamoja katika maisha ya ndoa,
Tatizo ni kwamba ameniambia kwamba siwezi kwenda kwao kujitambulisha mpaka kwanza nimpeleke yeye kwetu,sababu anayonipa ni kwamba
kwao wapo mabinti watano,na baba mkwe yaani baba yake anawataka binti zake kwanza wapafahamu nyumbani kwa vijana wanaowapenda kabla hawaja waleta kwake ili atoe idhini michakato mingine iendelee.
sasa wakuu naomba kujuzwa hizi ni taratibu za wenzetu wachaga,au vp nisije kuwa napigwa changa la macho,
kwa wababa wenye mabinti je huo ni utaratibu ambao mwaweza kutumia ili kujilidhisha kwamba kijana anayeletwa na binti zenu ni muoaji au.
Mpenzi wangu bado yupo masomoni anahitimu mwezi wa saba