Mchoro huu umenifikirisha sana

Mchoro huu umenifikirisha sana

Hizi barabara unazoziona sio za kiwango tukiamua tuzitumie kupitishia punda na wanajeshi waliovaa sendo na wananchi ambao wako peku, basi life span yake itakuwa ndefu zaidi

Ishu sio siasa, ishu ni kwamba tupo kwenye ulimwengu ambao una watu ambao wanapenda vya bei ndogo katika mazingira ambayo ni magumu kwa upatikanaji wa material.

Inawezekana kutengenezewa barabara nzuri yenye ubora utaodumu kwa kipindi kirefu zaidi lakini je bajeti hiyo mnaweza kuimudu?

Halafu unavyoliongelea hili ni kama unalenga africa na Tanzania kiujumla lakini hata huko kwa mabeberu zipo barabara za kirumi na bado barabara za mainjinia wa kisasa bado zina potholes je nao hao utasema wazungu wana siasa za kuweka watu ambao hawa fit kwenye idara husika?

View attachment 2131784
Na kwanini hatutengenezi barabara zenye viwango? Tutarudi kulekule.... Siasa. Sasa kama Mbunge wa darasa la saba anabishana na mhandisi mbobezi... na anamshinda kwa kupigiwa makofi mengi bungeni. Na bajeti inapitishwa... Sio siasa hiyo?

Au nifundishe siasa ni nini?
 
Na kwanini hatutengenezi barabara zenye viwango? Tutarudi kulekule.... Siasa. Sasa kama Mbunge wa darasa la saba anabishana na mhandisi mbobezi... na anamshinda kwa kupigiwa makofi mengi bungeni. Na bajeti inapitishwa... Sio siasa hiyo?

Au nifundishe siasa ni nini?
Sasa tukifika hapo tunatakiwa tujikosoe sisi na sio ma engineer

Hilo swala mimi nishawahi kulisema hapa

Kipindi cha magufuli kulikuwa na tabia ya yule mkuu wa mkoa agrey mwanri kuzunguka na makamera man kwenye sites ili ku criticize tu aonekane ni kiongozi mfatiliaji mwenye umakini na kazi yake

Alienda site akacukua tofali akaliangusha chini, halikupasuka, akaliokota tena akalitupa chini kwa nguvu likavunjika vipande viwili

Akawa anamtukana engineer kwamba amechakachua cement kwasababu tofali halina ubora limeangushwa limevunjika

Engineer akamjibu kwa busara na kwa taaluma kwamba tofali likianguka na kupasuka vipande viwili hilo ni imara, ila lingepasuka zaidi ya vipande viwili ungekuwa sahihi kwa hiyo mheshimiwa sio kweli kwamba tofali hizi zimechakachuliwa

Mwanri akatumia mamlaka yake ya ukiongozi kumnyamazisha na sio hoja maana ilionesha wazi kabisa kua hakuwa na hoja yakum conquer mkandarasi zaidi ya amri za kitemi kwa mgongo wa cheo
 
Walikua wazalenda, wa siku hizi wanakula mpaka wanavimbiwa...
 
Haha we nakataa hao jamaa walitumia elimu tena kubwa sana rudi shule historia haidanganyi.
 
Msipende kuitukana elimu, engineer anatengeneza barabara kulingana na pesa ambayo ipo

Pia kipindi zinatengenezwa hizo barabara ndio kile kipindi ambacho usafiri uliokuwa unatamba ulikuwa ni punda

Punda anauzito gani wa kufanya barabara ikreki?

Utafananisha na digital world ya kisasa ambayo mpaka excavators zenye minyororo zinapita kwenye barabara ya lami?
Mzee umeua kila kitu,hapo siongezi wala kupunguza neno.
 
Mkuu, kama ma elfu ya miaka iliyopita walibuni barabara zilizodumu mpaka sasa licha ya kwamba unadai sababu ya kudumu ni kutumika na punda ambao sio wazito
swali langu ni je kwanini nyie ma engineer mnashindwa kutengeneza barabara ambayo itahimili uzito wa juu wakati you have everything at your disposal from materials to knowlodge itself ? kwanini mnashindwa wakati ninyi ni bora zaidi ?
Hujaipata point yake wewe, Amesema ubora wa barabara inategemea na pesa aliyopewa injinia, Hilo namuunga mkono kwasababu yeye hawezi kwenda kinyume na bajeti; Mfano Umeona barabara ya Kwenda Ludewa ilivyosukwa nondo na zege?, Nakwambia pale kuna guarantee ya miaka 100, hadi kuanza kuharibika,itapisha gari za uzito mkubwa,sasa linganisha na barabara ya Kwenda Makete ambayo ni lami ya kawaida, hamna kitu pale.
 
Msipende kuitukana elimu, engineer anatengeneza barabara kulingana na pesa ambayo ipo

Pia kipindi zinatengenezwa hizo barabara ndio kile kipindi ambacho usafiri uliokuwa unatamba ulikuwa ni punda

Punda anauzito gani wa kufanya barabara ikreki?

Utafananisha na digital world ya kisasa ambayo mpaka excavators zenye minyororo zinapita kwenye barabara ya lami?
Kama mtaalam anatakiwa kukataa sio kukubali kufanya kitu kibovu
 
Msipende kuitukana elimu, engineer anatengeneza barabara kulingana na pesa ambayo ipo

Pia kipindi zinatengenezwa hizo barabara ndio kile kipindi ambacho usafiri uliokuwa unatamba ulikuwa ni punda

Punda anauzito gani wa kufanya barabara ikreki?

Utafananisha na digital world ya kisasa ambayo mpaka excavators zenye minyororo zinapita kwenye barabara ya lami?
Hata Sasa mwanza zinajengwa Barabara za mawe milimani ni Bora kuliko hizo za lami
 
Kuna jengo la soko limejengwa halijaanza kutumika tayari viraka sakafu yote ,viambata vimeshalika ..milngo imepasuka ...aseee
Sikatai kuwa mbishi nitakuwa mnafki kwa hilo, ila atleast nabisha kwa hoja

Sina ubishi kwamba hakuna mainjinia wasio walaghai wenye kufanya njama na watu waserikali. Ila nitakuwa mtu wa mwisho kukubaliana na wewe kua kwa uwepo wa aina hiyo ya mainjinia ndio kigezo cha kuishusha hadhi moderm technlogy na civil engineering kiujumla

Hapo utakuwa unafanya kitu kinachoitwa "Hasty Generalization" kufanya makosa ya kufananisha hoja kwa mifano michache ku prove point yako

Hiyo ni sawa na kusema, benadi alifeli kiswahili, ashura naye akafeli kiswahili, christian alifeli pia hivyo nahitimisha kua yeyote atayefanya mtihani wa kiswahili atafeli pia

Hiyo haiwezi kuwa sababu ya kujustify kwa watu wote, vipi kama benadi, ashura na christiani walikuwa hawazingatii masomo? Au kipindi mwalimu anafundisha wao walikuwa wanaumwa hawakuweza kuhudhuria?


Hizo barabara za kikoloni ziliweza ku handle circumstances kama hiziView attachment 2129265

Au hatahivi
View attachment 2129274

View attachment 2129273

Wote tutakubaliana kwamba zilijengwa mahususi kwa ajili ya hivi
View attachment 2129292

Wakoloni walijenga barabara kwa ajili ya kupitisha majeshi na watumwa ambapo wanajeshi walivaa sendos na watumwa walikuwa peku, ulitegemea uone damage gani tena kwa matumizi hayo ya barabara?
 
Kuna jengo la soko limejengwa halijaanza kutumika tayari viraka sakafu yote ,viambata vimeshalika ..milngo imepasuka ...aseee
Kwa hiyo hapo sababu ni degree ya siku hizi au material yaliyotumika hayakuwa na ubora?
 
Msipende kuitukana elimu, engineer anatengeneza barabara kulingana na pesa ambayo ipo

Pia kipindi zinatengenezwa hizo barabara ndio kile kipindi ambacho usafiri uliokuwa unatamba ulikuwa ni punda

Punda anauzito gani wa kufanya barabara ikreki?

Utafananisha na digital world ya kisasa ambayo mpaka excavators zenye minyororo zinapita kwenye barabara ya lami?
Duuh!!! mbona umeongea pumba ndg..
Hivi hujui kwanini mifugo hairuhusiwi kupita kwenye lami?
Ushawahi kuona hata mifugo wanapita juu ya daraja?
Kuhusu pesa ungesema miaka hiyo walijenga kwa pesa gharama kadhaa na sasa pesa imepungua au?
Gharama ya kujenga lami na hizo barabara za kitambo ipi ni kubwa?
Ungekuwa unajua basic za physics usingeongea huu utumbo.
 
Duuh!!! mbona umeongea pumba ndg..
Hivi hujui kwanini mifugo hairuhusiwi kupita kwenye lami?
Ushawahi kuona hata mifugo wanapita juu ya daraja?
Kuhusu pesa ungesema miaka hiyo walijenga kwa pesa gharama kadhaa na sasa pesa imepungua au?
Gharama ya kujenga lami na hizo barabara za kitambo ipi ni kubwa?
Ungekuwa unajua basic za physics usingeongea huu utumbo.
Hivi umeelewa hata nilicho kiandika au umekurupuka tu?
 
Back
Top Bottom