Mchoro huu umenifikirisha sana

Mchoro huu umenifikirisha sana

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,014
Reaction score
6,834
1645638854805.png
 
Msipende kuitukana elimu, engineer anatengeneza barabara kulingana na pesa ambayo ipo

Pia kipindi zinatengenezwa hizo barabara ndio kile kipindi ambacho usafiri uliokuwa unatamba ulikuwa ni punda

Punda anauzito gani wa kufanya barabara ikreki?

Utafananisha na digital world ya kisasa ambayo mpaka excavators zenye minyororo zinapita kwenye barabara ya lami?
 
Msipende kuitukana elimu, engineer anatengeneza barabara kulingana na pesa ambayo ipo

Pia kipindi zinatengenezwa hizo barabara ndio kile kipindi ambacho usafiri uliokuwa unatamba ulikuwa ni punda

Punda anauzito gani wa kufanya barabara ikreki?

Utafananisha na digital world ya kisasa ambayo mpaka excavators zenye minyororo zinapita kwenye barabara ya lami?
Mkuu, kama ma elfu ya miaka iliyopita walibuni barabara zilizodumu mpaka sasa licha ya kwamba unadai sababu ya kudumu ni kutumika na punda ambao sio wazito
swali langu ni je kwanini nyie ma engineer mnashindwa kutengeneza barabara ambayo itahimili uzito wa juu wakati you have everything at your disposal from materials to knowlodge itself ? kwanini mnashindwa wakati ninyi ni bora zaidi ?
 
Mkuu, kama ma elfu ya miaka iliyopita walibuni barabara zilizodumu mpaka sasa licha ya kwamba unadai sababu ya kudumu ni kutumika na punda ambao sio wazito
swali langu ni je kwanini nyie ma engineer mnashindwa kutengeneza barabara ambayo itahimili uzito wa juu wakati you have everything at your disposal from materials to knowlodge itself ? kwanini mnashindwa wakati ninyi ni bora zaidi ?
Na ndio maana nimesema engineer anafanya kazi kulingana na hela uliyo offer, hiyo ikimaanisha kuna grade za ubora ambazo kadri ubora unapokuwa wakiwango cha juu basi na gharama yake inakuwa ghali mno
 
Mkuu yaani kabisa unafananisha barabara zilizojengwa na Ccm Empire dhidi ya zilizojengwa na Rome Empire.

Tukianza na hao wahandisi wahenga kwenye picha hawakuwa malayman kama unavyodhani jamaa walikuwa wanakabidhi kazi kwa wahandisi waliokua njema upstairs, adhabu kali kwa wahandisi kama kifo iwapo kazi ikiharibika hivyo umakini ulikuwepo.

Pia ukumbuke hizo projects zao zilikua funded na falme zao hivyo kila walichohitaji kuanzia manpower, materials & equipments walivipata kwa wakati muafaka na kwa ubora uleule waliouhitaji.

Sasa ukija hapa Ccm empire kwanza tenda zinatolewa kwa michongo, wahandisi makanjanja, uhaba wa vifaa na materials, mwisho kabisa hakuna uwajibishwaji wala adhabu mujarabu wa hawa wahuni.
 
Mkuu, kama ma elfu ya miaka iliyopita walibuni barabara zilizodumu mpaka sasa licha ya kwamba unadai sababu ya kudumu ni kutumika na punda ambao sio wazito
swali langu ni je kwanini nyie ma engineer mnashindwa kutengeneza barabara ambayo itahimili uzito wa juu wakati you have everything at your disposal from materials to knowlodge itself ? kwanini mnashindwa wakati ninyi ni bora zaidi ?
Halafu anakuja na huo ujinga unaitwa elimu- nani hana elimu- yaani anaona kusoma na kuandika ndiyo elimu?
 
Na ndio maana nimesema engineer anafanya kazi kulingana na hela uliyo offer, hiyo ikimaanisha kuna grade za ubora ambazo kadri ubora unapokuwa wakiwango cha juu basi na gharama yake inakuwa ghali mno
Sasa nyumba zetu nazo ubora wake nao ni wa mashaka au nazo hampewi hela?
 
Na ndio maana nimesema engineer anafanya kazi kulingana na hela uliyo offer, hiyo ikimaanisha kuna grade za ubora ambazo kadri ubora unapokuwa wakiwango cha juu basi na gharama yake inakuwa ghali mno
Kuna kipindi unaleta ubishi kama wa Yanga na Simba. Mbali ya bajeti, barabara nyingi na hata Majengo yanaharibika kutokana na kutengenezewa chini ya kiwango huku bajeti ikiwa ya kutisha. Mkandarasi na Mainjinia wa serikali wanaotoa vyeti vya ubora wanakula njama na kupitisha barabara zisizomudu hata ule uzito uliopitishwa na Msanifu.
 
Back
Top Bottom