Mchango wa Kumsaidia Tundu Lissu Matibabu Nje ya Nchi

Status
Not open for further replies.

Tumaini Makene

JF-Expert Member
Jan 6, 2012
2,642
6,071
Kuhusu mchango wa matibabu ya Mhe. Tundu Lissu

Tunaomba kuwataarifu wanachama, wapenzi na wafuasi wa CHADEMA pamoja na watu wote wenye mapenzi ambao wanawiwa kuchangia kiasi (kitu) chochote kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Tundu Lissu, wawe wavumilivu kidogo hadi kesho ambapo Chama kitatoa utaratibu mzima ikiwa ni pamoja na njia zitakazotumika.

Tumelazimika kuratibu suala la matibabu ya Mhe. Lissu ikiwemo kuchangisha fedha kutoka kwa watu wote wenye mapenzi mema, baada ya Bunge kusema haliwezi kugharamia matibabu yake nje ya nchi, ambako CHADEMA tunaamini atakuwa na usalama wa uhakika wakati akipata matibabu.

Tuendelee kumuombea Mhe. Lissu wakati anaposafirishwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi huku tukisubiri chama kitangaze utaratibu wa wananchi kushiriki katika kuchangia matibabu hayo kesho wakati wa mkutano na waandishi wa habari saa 4 asubuhi.

Makene
 
Napenda kuwajulisha kwa mara nyingine, kwamba Lissu wetu anaendelea vizuri.

Ametoka chumba cha upasuaji na hali yake inaendelea kuimarika.

Matibabu yake yanashughulikiwa kikamilifu na wabunge wa UKawa, chama chake na baadhi ya marafiki zake.

...
Hii ni baada ya serikali kukataa kumtibia nje ya nchi na sisi kukataa kumtibu ndani ya nchi kwa sababu ya usalama wake.

Hivyo basi, tunaomba kila anayependa kuchangia matibabu ya Lissu kwa kiasi chochote alichonacho, kutuma mchango wake kupitia Na. 0759 865 786 ambayo ni ya Mhe. Esther Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini.

Huyu ndiye aliyeteuliwa na uongozi kwa kazi hiyo.

Saed Kubenea
Mbunge wa Ubungo
Lazima nichangie!...Eeee Mwenyezi Mungu nipe uvumilivu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Napenda kuwajulisha kwa mara nyingine, kwamba Lissu wetu anaendelea vizuri.

Ametoka chumba cha upasuaji na hali yake inaendelea kuimarika.

Matibabu yake yanashughulikiwa kikamilifu na wabunge wa UKawa, chama chake na baadhi ya marafiki zake.

...
Hii ni baada ya serikali kukataa kumtibia nje ya nchi na sisi kukataa kumtibu ndani ya nchi kwa sababu ya usalama wake.

Hivyo basi, tunaomba kila anayependa kuchangia matibabu ya Lissu kwa kiasi chochote alichonacho, kutuma mchango wake kupitia Na. 0759 865 786 ambayo ni ya Mhe. Esther Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini.

Huyu ndiye aliyeteuliwa na uongozi kwa kazi hiyo.

Saed Kubenea
Mbunge wa Ubungo
Lazima nichangie tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Napenda kuwajulisha kwa mara nyingine, kwamba Lissu wetu anaendelea vizuri.

Ametoka chumba cha upasuaji na hali yake inaendelea kuimarika.

Matibabu yake yanashughulikiwa kikamilifu na wabunge wa UKawa, chama chake na baadhi ya marafiki zake.

...
Hii ni baada ya serikali kukataa kumtibia nje ya nchi na sisi kukataa kumtibu ndani ya nchi kwa sababu ya usalama wake.

Hivyo basi, tunaomba kila anayependa kuchangia matibabu ya Lissu kwa kiasi chochote alichonacho, kutuma mchango wake kupitia Na. 0759 865 786 ambayo ni ya Mhe. Esther Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini.

Huyu ndiye aliyeteuliwa na uongozi kwa kazi hiyo.

Saed Kubenea
Mbunge wa Ubungo
mimi natuma kwa namna ninavyo guswa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom