Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,214
- 42,087
Wanajamvi, Wasalaam.
Ni ukweli usiofichika kabisa wasanii na wadau wa sanaa Tanzania walikuwa na mategemeo makubwa baada ya kuona mtu ambaye alikuwa kwenye sanaa ya muziki muda mrefu amekwenda bungeni.
Wengi walitegemea Mh Joseph Mbilinyi (Sugu )angekuwa kiungo kikubwa cha wasanii na wasanii au wasanii na wadau wa sanaa hasa muziki.
Kila mtu anajua fika sanaa ya Tanzania ina matatizo mengi ambayo kwa nafasi yake angeweza kuyatatua haraka hasa hii migogoro ya wasanii kwa wasanii au wadau wa sanaa au muziki na wasanii.Lakini kinacho sikitisha zaidi yeye amekuwa akichochea mivutano hiyo kwa kujionesha yuko upande fulani kwa wakwaruzanao,wakati tulitegemea yeye ndio angekuwa msuluhishi mkuu wa hiyo migogoro hiyo jitokeza na kupata suluhu.
Tunajua fika hakuna mwanadamu aliye kamilika na hata hao anao watetea kwenye hiyo migogoro nao wana matatizo yao pia na unaweza kukuta wao ndio chanzo. Tunajua Mh Mbilinyi aliwai kuwa na migogoro na baadhi ya wadau wasanaa lakini asiwafanye wasanii wote nao wawe na migogoro nao bali alitakiwa aoneshe njia kwa kuhakisha ana waunganisha wasanii.
Pia tulitegemea kuona Mh mbilinyi angekuwa wa kwanza kuanzisha mfuko maalum wa wasanii ambao ungetumika kuwaunganisha na kuwasaidia wasanii wakati wa shida hasa wanapo patwa na misiba waache kuwa omba omba.
Hivi Mh mbilinyi hadi sasa kafanya nini kuokoa sanaa hii?Hivi atakumbukwa kwa lipi? Yani hata hili la kutatua migogoro kati ya wasanii na wadau wa sanaa limemshinda? Kwanini asiitwe waziri kimvuli mzigo?
Nilitegmea Mh Mbilinyi ange shirikiana bega kwa bega na waziri Fenela kutatua matatizo yale yanayo weza kupatiwa ufumbuzi kwa haraka at least wasanii na wadau wafaidike na uwepo wake,kinyume chake ameweka siasa mbele na kuona kila mdau au waziri wana nia mbaya na sanaa, na hili analifanya ili kupandikiza chuki wakati anajua fika chuki haijengi.
Naulize tena Mh mbilinyi amefanya nini kwenye sanaa tangu awe mbunge?Bado najiuliza kwanini amekuwa akiwa katisha tamaa wadau wasanaa na kuonesha wao ni wezi na wana wanyonya wasanii. Yeye hadi leo kafanya nini?
Ni ukweli usiofichika kabisa wasanii na wadau wa sanaa Tanzania walikuwa na mategemeo makubwa baada ya kuona mtu ambaye alikuwa kwenye sanaa ya muziki muda mrefu amekwenda bungeni.
Wengi walitegemea Mh Joseph Mbilinyi (Sugu )angekuwa kiungo kikubwa cha wasanii na wasanii au wasanii na wadau wa sanaa hasa muziki.
Kila mtu anajua fika sanaa ya Tanzania ina matatizo mengi ambayo kwa nafasi yake angeweza kuyatatua haraka hasa hii migogoro ya wasanii kwa wasanii au wadau wa sanaa au muziki na wasanii.Lakini kinacho sikitisha zaidi yeye amekuwa akichochea mivutano hiyo kwa kujionesha yuko upande fulani kwa wakwaruzanao,wakati tulitegemea yeye ndio angekuwa msuluhishi mkuu wa hiyo migogoro hiyo jitokeza na kupata suluhu.
Tunajua fika hakuna mwanadamu aliye kamilika na hata hao anao watetea kwenye hiyo migogoro nao wana matatizo yao pia na unaweza kukuta wao ndio chanzo. Tunajua Mh Mbilinyi aliwai kuwa na migogoro na baadhi ya wadau wasanaa lakini asiwafanye wasanii wote nao wawe na migogoro nao bali alitakiwa aoneshe njia kwa kuhakisha ana waunganisha wasanii.
Pia tulitegemea kuona Mh mbilinyi angekuwa wa kwanza kuanzisha mfuko maalum wa wasanii ambao ungetumika kuwaunganisha na kuwasaidia wasanii wakati wa shida hasa wanapo patwa na misiba waache kuwa omba omba.
Hivi Mh mbilinyi hadi sasa kafanya nini kuokoa sanaa hii?Hivi atakumbukwa kwa lipi? Yani hata hili la kutatua migogoro kati ya wasanii na wadau wa sanaa limemshinda? Kwanini asiitwe waziri kimvuli mzigo?
Nilitegmea Mh Mbilinyi ange shirikiana bega kwa bega na waziri Fenela kutatua matatizo yale yanayo weza kupatiwa ufumbuzi kwa haraka at least wasanii na wadau wafaidike na uwepo wake,kinyume chake ameweka siasa mbele na kuona kila mdau au waziri wana nia mbaya na sanaa, na hili analifanya ili kupandikiza chuki wakati anajua fika chuki haijengi.
Naulize tena Mh mbilinyi amefanya nini kwenye sanaa tangu awe mbunge?Bado najiuliza kwanini amekuwa akiwa katisha tamaa wadau wasanaa na kuonesha wao ni wezi na wana wanyonya wasanii. Yeye hadi leo kafanya nini?