Mchange awashambulia viongozi wa CHADEMA

Mchange awashambulia viongozi wa CHADEMA

Mdogo wangu Habibu Mchange,nini kinachokusumbua na kukunyima utulivu wa kimaisha. Kama CHADEMA hawakutaki,kwanini usijielekeze kwingineko? Unadhani utawaweza CHADEMA wewe kweli? Mdogo wangu Mchange,achana na utapeli wa kisiasa na kutumika. You have a great future if you choose rightly.
Wewe ni kibaraka na mchumia tumbo
 
Mchange mchange...!!mbona ww ulihongwa na Mbunge wa Kibaha ili ukubali matokeo..ukaenda kujenga nyumba pale kwenu Uyaoni..Kibaha..!!😀😀😕

mimi naishi uyaoni mchange hana hata kibanda cha udongo hapa uyaoni,labda tuambie ww na mmeo mchange mlijenga wapi
 
kwani hili suala la chacha wangwe ni uongo mbona kweli kabisa au unapingana na ukweli?

Mchange yuko upande na anawatumikia CCM, na CCM ndio chama kinachounda serikali. Na kazi ya serikali ni kuhakikisha raia wake wanafuata sheria zilizowekwa. Sasa kama Mchange anawajua waliomuua Chacha Wangwe na ana ushahidi imeishinda nini serikali kuwafungulia mashtaka hao wauaji kwa kutumia ushahidi huo wa Mchange?

Acha kujitoa akili kwa ajili tu ya book 7, tunajua kifo cha Wangwe ulikuwa ni mpango wa CCM kwa kumtumia Mallya baada ya Wangwe kula hela za CCM na kushindwa kuisambaratisha CDM kama alivyoahidi. Kamuulize Makamba huu mpango anaujua kwa karibu, wewe unabwabwaja tu hapa.


Tiba
 
uzuri wa mchange husema ukweli ambao hauna hata chenga suala la chacha wangwe chadema hawakwepi.

mimi sishangai maana hawa chadema walishasema nchi haitatawalika,nashangaa sana mwenyekiti wangu mbatia kuwaunga mkono hawa magaidi waliopoteza mvuto ndani ya chama
 
Yaani utumbo mtupu utaandikwa na uhuru sidhani kama kuna gazeti litakaloandika
 
DAAA R.I.P CHACHA WANGWE
Dunia Nzima inajua kwamba watu hawa wameshiriki kikamilifu kumuondoa DUNIANI aliyekuwa makamu mwenyekiti wa chama CHACHA ZAKAYO WANGWE, Hii haina ubishi kwamba, MBOWE, SLAA na MNYIKA walijaribu mara kadhaa kutaka kumuua CHACHA WANGWE kwa kutumia sumu na kushindwa mpaka walipofanikiwa kumuua kwa ajali ya kutengeneza tarehe 28.7.2008 wakimtumia kijana ambaye Dunia nzima inamjua.
 
Kumbe CCM kuchelewa koote kujibu tuhuma za kulipua helkopta walikuwa wanatunga huu upuuzi na kutafuta wa kumtumia?
 
Kumbe Wajifunze kwa Zitto kukaa kimya na kuendelea na Maisha.
Lissu namshauri aache ubinafsi na ubabaishaji.

Dunia nzima inafahamu kwamba alikula milioni 250 za wafadili kwenye shirika lao la kiraia na shirika likafia hapo hapo nay eye kwenda kujenga ghorofa pale tegeta.

Lissu hawezi kuwa kama zitto, zitto ni zitto na lissu ni lissu. Ninamshauri apunguze kukubali kuchukuliwa kama zezeta.
@tundu lissu kelele nyingi na yeye ni fisadi duuu
 
LISSU ni MBINAFSI ALIYEPITILIZA na UBINAFSI WAKE ndio umemfanya mpaka alipoombwa kushauri namna bora ya kupatikana kwa wabunge wa viti maalum kama mwanasheria wa chama, akaweka sharti na kuhakikisha kwanza Dada yake CHRISTINA LISSU anakuwa Mbunge wa Viti maalum, na ndio maana dada yake alikuwa MBUNGE wa viti maalum wa chadema kwanza kabla ya kuwa MWANACHADEMA. Alipelekewa kadi ya CHADEMA bungenidodoma baada ya kula kiapo cha ubunge.
 
Mchange nimekusoma ni dhahiri umeweweseka na tukio lakutaka kuwadhuru viongozi wa CHADEMA hutachomoka.
 
Last edited by a moderator:
Hawa watu ni wapumbavu sana. Kama wamesingiziwa si waend mahakamani, wanapokuwa kuleta utetzi wao hapa ni ishara tosha kwamba wanaogopa kwenda mahakamani. Ukweli wanaudhi sana.

Kumbe CCM kuchelewa koote kujibu tuhuma za kulipua helkopta walikuwa wanatunga huu upuuzi na kutafuta wa kumtumia?
 
Duu huu ni mwiba kwa lissu

Ni lissu ndiye ndiye aliyemtukana na kumdhihaki Prof. BAREGU na kutaka ajitoe kwenye chama ama abaki tume ya katiba kwa kuwa Tume haina weledi
Ni lissu ndiye aliyemzihaki JOSEPH WARIOBA na kusema kwamba anaendesha tume ki CCM CCM na kwamba CHADEMA haiungi mkono kitakachotolewa na Tume. – leo LISSU na CHADEMA wamekuwa makwapani mwa TUME na WARIOBA

Aliwakashifu CUF akawaita WAKE WA CCM, akawakashifu NCCR na MBATIA wao, akawakashifu MAASKOFU na MASHEIKH akawakashifu wazanzibar. Leo aibu ya CHADEMA imefichwa na CUF na NCCR-MAGEUZI. Aache kuwa mnafiki wa kisiasa.
 
Back
Top Bottom