Mch. Mhe. Dr. Getrude Lwakatare achunguzwe!

Mch. Mhe. Dr. Getrude Lwakatare achunguzwe!

Mh jamani hapa kuna usanii unatembea, mie nilikuwa simwamini huyu DR. na Mbunge wetu, wife wangu alikuwa anapenda kwenda kwa maombezi huko mikocheni, alipenda kwenda kuombewa kwenye hilo kanisa, mie sijawahi kwenda hapo na sikuwa na mpango wa kwenda kabsaa. Mwaka jana mwezi kama wa saba hivi wife alimpeleka mtoto wetu akaombewe maana alikuwa anatatizo sana la kukataa kula. mara nyingi nilikuwa namwambia wife kwamba pale ni imani yako ndo inakuponya, lkn si uwezo wa yule mama, wife alikwenda pale alikutana na mmoja kati ya wale wachungaji wawili wa kiume ambao mara nyingi hounekana na yule mama MBUNGE, kilichotokea yule mchungaji akaanza KUMTONGOZA wife, kwa kweli wife alishtuka sana akauliza hii ndo huduma ya mungu mnayosema mnatoa hapa? yule mchungaji akatetemeka akaomba msamaha, wife akageuza hapo akanipigia simu nikamwambia, I TOLD YOU HOME GIRL! kweli pale ni pure bizness, wengi wetu tunaenda sali kwenye haya makanisa tukiwa na SHIDA, pale mchungaji atakujaza woga na ile shida yako basi utaamini kila kitu. Nilienda kwenye kanisa Moja mbezi, mchungaji alisisitiza sana fungu la kumi, tena sana hata sisi wakatoliki huwa hatukamuani namna ile DAH!
 
Mh jamani hapa kuna usanii unatembea, mie nilikuwa simwamini huyu DR. na Mbunge wetu, wife wangu alikuwa anapenda kwenda kwa maombezi huko mikocheni, alipenda kwenda kuombewa kwenye hilo kanisa, mie sijawahi kwenda hapo na sikuwa na mpango wa kwenda kabsaa. Mwaka jana mwezi kama wa saba hivi wife alimpeleka mtoto wetu akaombewe maana alikuwa anatatizo sana la kukataa kula. mara nyingi nilikuwa namwambia wife kwamba pale ni imani yako ndo inakuponya, lkn si uwezo wa yule mama, wife alikwenda pale alikutana na mmoja kati ya wale wachungaji wawili wa kiume ambao mara nyingi hounekana na yule mama MBUNGE, kilichotokea yule mchungaji akaanza KUMTONGOZA wife, kwa kweli wife alishtuka sana akauliza hii ndo huduma ya mungu mnayosema mnatoa hapa? yule mchungaji akatetemeka akaomba msamaha, wife akageuza hapo akanipigia simu nikamwambia, I TOLD YOU HOME GIRL! kweli pale ni pure bizness, wengi wetu tunaenda sali kwenye haya makanisa tukiwa na SHIDA, pale mchungaji atakujaza woga na ile shida yako basi utaamini kila kitu. Nilienda kwenye kanisa Moja mbezi, mchungaji alisisitiza sana fungu la kumi, tena sana hata sisi wakatoliki huwa hatukamuani namna ile DAH!

Jamani mtoto akikataa kula naye anapelekwa kuombewa kanisani? Don't take it personal mzee, lakini watu wakishakuwa brainwashed kiasi hicho basi hao walio wa-brainwash wanawacheka kimoyo moyo na kufikia kuwatongoza.

Sasa niambie wanawake wangapi watakuwa wameshatongozwa na hao watoa huduma na wakakubaliana nao kufanya mapenzi? Lazima ni wengi sana! Halafu mbaya zaidi lazima inakuwa siri kubwa, mwanamke tena mke wa mtu akitembea na mchungaji hawezi kumsimulia mtu yeyote kutokana na hofu anayokuwa kajazwa! Kuna mchungaji mmoja ana kanisa Mbagala halafu bia anakuja kunywa Kijitonyama!
 
Jamani mtoto akikataa kula naye anapelekwa kuombewa kanisani? Don't take it personal mzee, lakini watu wakishakuwa brainwashed kiasi hicho basi hao walio wa-brainwash wanawacheka kimoyo moyo na kufikia kuwatongoza.

Sasa niambie wanawake wangapi watakuwa wameshatongozwa na hao watoa huduma na wakakubaliana nao kufanya mapenzi? Lazima ni wengi sana! Halafu mbaya zaidi lazima inakuwa siri kubwa, mwanamke tena mke wa mtu akitembea na mchungaji hawezi kumsimulia mtu yeyote kutokana na hofu anayokuwa kajazwa! Kuna mchungaji mmoja ana kanisa Mbagala halafu bia anakuja kunywa Kijitonyama!


Mkuu MASAKI najua utashangaa mtoto akikataa kula kwa nini akaombewe,tatizo ni kumeza, hata ufanyaje alikuwa hawezi kumeza chakula, tulienda kwa Dr. Massawe pale morocco, akampima akasema ana vijinyama vimeota kwenye koo na puani, akapewa dawa akatumia kwa 2 weeks, hali yake ikawa km ime improve lkn baada ya wiki moja akaanza tena tatizo lile lile la kumeza chakula, ndipo wife kwa kuwa alikuwa anasali pale mara kwa mara hakutukuona vibaya kama akiombewa pale, na ni heri uende kwenye maombi kuliko kwa mganga wa kienyeji, huko ndo alikokumbana na hiyo FEDHEHA. tuhuma ni nyingi tu pale kwa mama Mchungaji lkn ndo hiyo waumini hawaishi kwenda tokana nashida zao. Namshukuru Mungu mwanangu ame improve kwenye kula japo anakula almost 2hrs ndo amalize msosi wa kula dk 20 tuu
 
Hivi kwanini wachungaji wengine ni waongo sana ! huyu ni tapeli kama mchungaji masapila! a.k.a babu wa Loliondo !
 
kweli nimefurahi hata nimeiona post moja ya Regia Mtema R.i.p dada Mungu kama ulimtumikia na kujitoa kwa ajili ya wanadamu wake legelege wa tanzania ninaamini sasa dada unakula bata za ukweli huko kwake nlisema Mungu ana nafasi yako Regia sisi huku tunaendelea kupambana nina mpango mwaka 2015 nigombee udiwani kata flan hivi dsm rip
 
...mnamzungumzia Getrude Lwakatare yupi, au mnamaanisha huyuhuyu anayejifanya kuwa mchungaji na wakati huohuo mbunge huku akiwa anatembea na FELICIAN MUTTA aka. Mzee wa Kino?
 
masikini waumini wa imani za namna hii wanatia huruma muumba alisema watu wangu wanakufa kwa kukosa maarifa. miujiza itawapeleka watu pabaya
 
...mnamzungumzia Getrude Lwakatare yupi, au mnamaanisha huyuhuyu anayejifanya kuwa mchungaji na wakati huohuo mbunge huku akiwa anatembea na FELICIAN MUTTA aka. Mzee wa Kino?

kwani huyu mtumishi wa Mungu hajaolewa?
 
Kwa jina la Yesu watakuja na watadanganya wengi!!Kwa jina la gadgets wata -make huge amounts of money!

Kweli mkuu; maandiko ktk Bible yako wazi sana kuhusu viongozi wa dini wa sampuli ya akina Mama Lwakatare. Wanatumia mgongo wa dini kujinufaisha wao na familia zao. "Mtawajua kwa matendo yao".
 
Mkuu,
Heshima yako kwa post hii na uthubutu wa kuhoji watumishi wa Mungu ambao wanatumia kinga ya kuwa hawawezi kusemwa kwa maana watalaaniwa wale wawasemao watumishi wa Mungu.
Kwa sisi tunaoamini,kwenye Mithali kuna mstari unaosema, "kama theluji wakati wa joto,kadhalika laana isiyo na sababu haimpati mtu..."

Niliwahi kuandika siku kadhaa zilizopita, fuatilia link hii
https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/198261-mtumishi-wa-kuogopwa-kama-ukoma.html

Huyu mtumishi bado anaendelea kuwapoteza kondoo. Mtandao wake wa "kiumungu" umeanzia South Africa ambako hata mkuu wa nchi ile anafadhiliwa na big boss wa mtumishi huyu. Hapa Tanzania kuna daktari mmoja yuko Aga Khan hospt ambaye anawapa watumishi hawa raw materials za kazi zao. Nikikamlilisha uchunguzi,nitamwaga data hapa hapa jamvini.

Kuna haja ya kumchunguza kwa kina ili kama yuko genuine huyu mbunge basi tukiri kwa kinywa kuwa yu mtumishi wa kweli. La, itabidi tumuanike ili hata Mungu wetu aliye hai akimtwaa, na kaburi lake liandikwe kuwa "Mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo alizikwa hapa"
 
Katika hiyo miujiza ambayo wakatoliki huwa wanachunguza na kutangaza ni ipi? sijawahi kusikia miujiza katoliki , kama una mifano toa mkuu!??

Waberoya
Nimingi kabisa ambayo haitatosha kuiandika kwa mstari mmoja. Kwa mfano kuna inayotokea hata leo kule Lurdi, Ufaransa ambako inasemekana Bikira Maria alimtokea Binti mmoja karne ya kumi na tisa na kuahidi miujiza toka sehemu ile itakayodumu. Na ni kweli miujiza ya uponyaji wa kiroho na kimwili unaendelea tokea miaka ya 1800 ile hadi sasa. Kanisa limeweka madaktari wanaowachunguza watu kabla na baada ya kwenda kwenye ibada kule na kamwe halijinadi wala kuwahamasisha watu kwenda huko! Kuna vipande vya tishu ya binadamu ya mfumo wa nyama na damu iliyotokana na mageuzi ya mkate na divai zaidi ya karne tano sasa bila ya kuoza wala kuharibika na kanisa limekubali shirika la utamaduni na sayansi la UNESCO kufanya utafiti wa tissue hizo toka miaka ya sabini ambapo matokeo yake yamethibitisha muujiza usio na ufafanuzi wa kisayansi kwani wanasayansi hawakukuta dawa ya aina yoyote iliyotumika kuihifadhi damu na tissue hiyo iliyothibitika kwamba ni kipande kilichokatwa toka katikati ya moyo wa binadamu wa kiume na aliye hai hadi kila wakati specimen hizo zilipochukuliwa kwa utafiti! Kuna miili ya watu wacha Mungu waliokufa wengine karne za mwanzo kabisa wa historia ya kanisa ambayo baada ya kufukuliwa mamia ya miaka baadae ilionekana kutooza bila ya kuwekewa dawa yoyote ya kuihifadhi! kuna Sanda inayosadikiwa kuwa ni ya Yesu ambayo hadi sasa wanasayansi wamepigwa butwaa na kile wanachokishuhudia kutokana na utafiti wao....na miujiza mingi tu, kwa hiyo si dhambi kuichunguza miujiza.
 
Si Mama lawakatare tu, hata akina Mwingira, Mzee wa upako, Kakope and the likes ni matapeli tu. Haiwezekani muhubiri anahubiri watu kupata uponyaji, na mali tu. Mimi sijawahi kuwasikia wakihubiri kwa nguvu kuhusu waumini wao kuishi maisha ya uadilifu na kuonyesha upendo kwa binadamu wengine.
 
Back
Top Bottom