Mch. Mhe. Dr. Getrude Lwakatare achunguzwe!

Mch. Mhe. Dr. Getrude Lwakatare achunguzwe!

Pengine anawalipa kwa hiyo kazi wanayotumikishwa kama misukule
 
Bongo ishaokota makopo hii! Mwenzako mama Lwakatare anafanya yake, wewe huna ya kufanya? Dunia ya sasa wewe pambana na magumu ya maisha kivyako,, ukianza kuangalia wanaofanikiwa wamepataje utajiri utapatwa na stress bure! Wajinga ndo waliwao, na wewe tafuta wajinga wako uwale usonge mbele na si kujifanya mkaguzi eti watu wanatoboa vp kimaisha.
 
Mwanakijiji,

Mimi naamini kwa YESU YOTE yanawezekana!

Isimuhukumu huyu mama. Ina maana waumini wote hapo kanisani hawayaoni hayo yote?

FP

''Enter thr. the narrow gate. For wide is the gate and broad is the road that leads to destruction, and many enter thr. it."
They have eyes, but they can't see.
 
Mzee kajihami mapema. Kama ni kweli kawafufua, kumwomba msamaha tu yatosha kwa tuhuma nzito hivi?
 
With all due respect, mapema sana nilishasema kuwa huyu mama mimi ninamshitukia sana kwa sababu ninajua according to the dataz, kuwa anajirusha na Mkulu mmoja wa CCM,

Kwa hiyo haya mengine yote ni tisa, kumi Mungu hawezi chezewa na bina-adam hata siku moja, ndio maana yanaanza kujitokeza, ni aibu sana kwa wale tunaomuamini Mungu.

Field Marshall ES mbona unaasi na kupiga ikulu? Mkuu wa majeshi amepona kweli? Biblia Takatifu inatuambia kuwa Yesu alisema ni vigumu kwa tajiri kupenya katika tundu la sindano lakini kwa ngamia inawezekana! Mama Lwakatare ni tajiri na utajiri wake ni haramu na wafuasi wake ni ngamia wa imani! Naunga mkono viti maalumu kufutiliwa mbali.
 
Mkuu Mwanakijiji, Mungu aliyeumba vitu vyote vinavyoonekana na visivyo onekana akubariki sana kwa kutokuwa na imani na mama Lwakatare. Na isiwe kwa mama huyu msanii peke yake, iwe pia kwa wachungaji wengine matapeli,wezi na wanaofanya biashara haramu za kuuza madawa ya kulevya kwa kivuli cha kanisa!

Siku moja house girl wetu alipandwa na mashetani. Mke wangu akasema tumpeleke kwa Lusekelo mzee wa upako kwani huwa anaona kwenye TV jinsi anavyowaombea watu na kupona! Tulipofika kanisani kwake tulimkuta ndani ya gari (Range Rover nyeusi), alipotuona tunashuka kwenda kumwomba huduma alimwamuru dereva na kuondoka bila kutoa msaada!

Baadaye tulipokuwa tunashangaa alijitokeza mhudumu mwingine na kusema eti mzee wa upako ana siku maalumu za kufanya maombi! Kwa hiyo siku tuliyoenda haikuwa siku ya yeye kuombea watu! Yesu alimponya mgonjwa siku ya SABATO! Tukashauriwa tununue mafuta ya baraka yanayouzwa shilingi 10,000/- na kumpaka mgonjwa wetu.

Nilinunua mafuta hayo yanayosemwa ni ya baraka wakati si kweli na kumpaka mgonjwa na kufanyiwa maombi na yule mhudumu, lakini hakuna mabadiliko yoyote yaliyopatikana pale kanisani mpaka tuliporudi nyumbani ambako alitulia kisha siku iliyofuata alikwenda kwao kudumisha mila na desturi. Baadaye alirudi akiwa mzima kabisa mpaka leo hii. AMEN.
 
bahati mbaya kuliko ZOTE kuhusu manabii, mitume, na wanamiujiza wa leo ni kwamba mara nyingi wagonjwa na walemavu wanaopona huwa ni wageni na hawajulikani na wenyeji wa eneo husika, wagonjwa wetu tunaowafahamu hawaponi. na waumini hatusemi. tunapumbazwa na matatizo yetu, na kutojiamini kwetu, na udhaifu wa mawazo.
 
Bongo ishaokota makopo hii! Mwenzako mama Lwakatare anafanya yake, wewe huna ya kufanya? Dunia ya sasa wewe pambana na magumu ya maisha kivyako,, ukianza kuangalia wanaofanikiwa wamepataje utajiri utapatwa na stress bure! Wajinga ndo waliwao, na wewe tafuta wajinga wako uwale usonge mbele na si kujifanya mkaguzi eti watu wanatoboa vp kimaisha.
Uko sahihi
 
Hekima ya dunia hii inahesabiwa kuwa ni upumbavu mbele ya Mungu wetu
 
Back
Top Bottom