Mbwana Samatta Man of the Match achemka kutema Ung'eng'e

Mbwana Samatta Man of the Match achemka kutema Ung'eng'e

nahisi unamaanish kilimanjaro stars,,,
Manake hiyo ilofuzu sio taifa stars
 
Kiingereza sio ishu,ishu ni kwamba alianza kwa kuongea kiingereza alipoona kina mshinda ndo akaomba poo na kuomba ajieleze kwa kiswahili.kwa nini asingeanza na kiswahili toka mwanzo??tatizo watanzania hatutaki kukubali kwamba hatujui

hatujui english? Tukijua itatusaidia nini? Ramires naye ni kama mbwana maana english kwake bado ishu, chelsea hawaoni kama ni tatizo wao wanataka aonyeshe viwango uwanjan
 
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal

Hapo kwenye lugha hakuna tatizo hata kidogo. Ulaya, wachezaji walio wengi hawajui lugha ya nchi husika walipoajiliwa!
 
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal
mkuu kuna wachezaji wengi tu wa kulipwa katika ligi mbalimbali duniani ambao hutumia lugha zao na bado wanakubalika,vipi wewe kutekwa na ukoloni,acha hizo ngd jikubali na wengine watakukubali,au ndio nyie mnaotoka vijijini kwenu mkifika mjini mnakataa kabila lenu na kijiji pia
 
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal

Bora Mmesema Nyie Kwani Ningechangia Mimi Ungesikia Lawama Zao. Hili Jambo Nimeshaliongea Sana Lakini Nashangaa bado tuna Watu ambao Wana Vimelea Vya Ukoloni. Hivi Wewe Unayesema Mbwana Samatta Poppa Hajui Kiingereza Una Habari Kwamba Kwa Pesa tu Alizonazo na Utajiri Wake Anaweza Akakuajiri hadi Wewe Unayemcheka na Akakulisha, Kukuvalisha na Ikibidi hata Kukupiga KIBOGA? Wewe na Kujua Kwako Kiingereza Umeifanyia Nini Nchi Yetu hadi na Wewe Tukutambue na Tukufagilie? Huyo Unayemsema Muda Wowote Anakwenda Ulaya Kula Bata huku Mimi na Wewe Tukibaki Kula Vumbi la Jijini Bongo bila Kusahau Joto letu Kali hili. Nawapenda Sana Watu na Haswa Wasomi Wanaodumisha na Kukienzi Kiswahili Chetu.
 
Safi kijana Samata, ni vizuri na wanamichezo pamoja na wasaniiwengine wakaiga mfano wake.
Kuna wasanii wanajitutumua kuandika english blocken kwenye twita zao matokeo yake wanaaibika tuu.
Tujivunie lugha yetu.
 
Uzalendo mbele... pongezi kwa Captain Samatta; kila la heri safari ya kufika majuu imewadia tupandishie Bendera kileleni.
 
Huu ndo ungese nna0ukataaga angekua messi kashindwa kuongea ung'eng'e ungeanzisha thread?
 
Hivi hao wakina Messi mara nyingi
huongea sijui kikwao lakini sio Kiingereza
Cha msingi na muhimu ni uwezo hasa
ushindi tulioupata na hatimaye kunyakua

KIKOMBE!
 
Huyu aliyeandika post hii tumsamehe bure. Akili yake bado anawaza na kuota itokee siku moja mkoloni arudi Afrika. Hajiulizi kwanini Wachina hawataki utumwa wa lugha nyingine? Hasumbuki kufikiria kwanini leo mataifa mengi ya Afrika yanajifunza Kiswahili. Mbwana Samatta ana akili nyingi kuliko mtoa mada
 
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal

Kwa kawaida mtu yeyote huhojiwa na kujieleza kwa lugha anayoifahamu. Na kujua lugha au kutokujua lugha fulani siyo kigezo cha usomi au kutosoma
 
Acha ushamba!! Angekuwa raisi wa china kashindwa kuongea kingereza au kiswahili ingekuwa siyo hoja kubwa ila mtanzania kashindwa basi tabu....acheni ushamba wakifikra.
 
Very Good kwa kijana wa elimu yake! Pia kule anapocheza wanatumia French!
Cha msingi ni confidence mbele ya camera na usahihi wa majibu
Binafsi nilifurahishwa nae na alichokusudia kusema ni kuwa the Cranes wamekuwa wakitufunga mfululizo hivyo tulitaka kubadili hilo na tumeweza
Wabongo wenzie tuliosomea chini ya mti tumemsoma vema
 
Acha utumwa ndugu Mtanzania. Kujua ung'eng'e c kigezo cha kuwa real proffesional. Kaulize Brazil km wote wanaonunuliwa Ulaya km wanajua English.
 
Yakubu,
Now this is interesting...especially when it comes from the Economist Magazine

Dont get me wrong as i think it is incredibly concise and detailed, covering the entire globe,their depth and wide coverage is very impressive, and I like the way that they do not need to grab readers with sensationalism, like many othe papers most junk out there which still have narrow view of Africans and their leaders.

Dont forget that the Economist has a very specific stance, ie. free market championing among other things. The article was abit simplistic even though according to the Economist standard of Journalism (RIGHTWING) they were overall favourable to JK but be adviced it wont last long.

waiting for Mwanasiasa's input on this

Kama hajui au hataki kiingereza na kaomba ahojiwe Kiswahili namuheshimu zaidi kwa hilo.

Castro anajua Kiingereza vizuri, lakini waandiahi qa Marekani walikuwa wanamuhoji yeye anaongea lugha yake tu Kihispania.

Kwa nini tunakisujudia Kiingereza?

Kwa nini muafrika mmoja aongee na mwinvine kwa lugha ya Muingereza wakati tuna lugha zetu?
 
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal

kwani kidhungu ndio kujua mpira wapi chinese lads..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom