Mbwana Samatta Man of the Match achemka kutema Ung'eng'e

Mbwana Samatta Man of the Match achemka kutema Ung'eng'e

Jambo Tz

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
670
Reaction score
203
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal
 
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal

Vipi angekua mchina afu akaomba kuulizwa kwa kichina, sredi ingekuwepo?
 
Wewe usiwe mtumwa,sisi tupo afrika mashariki tunataka lugha yetu ikue, pia wao ndio walimfuata kufanya naye mahojiano, kwahyo hana uamuzi wa kuchagua lugha anayotaka yeye,pia jifunze pia kuangalia wachezaji wa mbele wanapenda kuhojiwa kwa lugha za kwao, sawa mjomba?
 
Chezeiya Lugha ya Malkia wewe kidhungu kimekuja na Meli achana nacho kabisa
 
Taifa Stars imefuzu kucheza Nusu fainali baada ya kuivurumisha Uganda, na mtu aliye teuliwa man of the Match ni Mbwana Samatta ana hojiwa na Ssport kwa kimombo akashindwa na kuomba kuhojiwa kiswahili
kwa hili la Samatta ni dhahiri shahiri wanatakiwa kupelekwa twishen ya kidhungu ili wawe realy Profeshenal
Lugha za watu hizo kuchemka kawaida kama wewe ulivyochemka kuandika profeshenal badala ya professional, michuano ichezwe Africa mashariki kwa waswahili na bado mkomae na lugha za watu, hivi kwanini kwa kukijua kiswahili isiwe sababu ya kujivunia kwani kila kitu tunategemea kutoka nje but mwisho wa siku tumeweza kuwa na lugha yetu wenyewe kama ilivyo kwa wachina. Kwahiyo ili uwe professional unahitaji kujua kiingereza?
 
Mimi amenifurahisha kuliko kama angeongea broken.

Mbona huwa hamumsemi Rais wa China?

BTW Samatta is talented....najivunia huyu Mtanzania mwenzangu kama ninavyojivunia the man himself Mwl JK Nyerere.
 
Achana na mawazo finyu wewe maskini wa kufikiri. Kumbuka mawazo sahihi yanatokana na fikra ulizofikiri katika lugha sahihi.kwanza nampongeza kwa kukipa hadhi kubwa kiswahili maana siyo kila taaluma inahitaji kiingereza.tambua huyo mchezaji anacheza congo huko wanaongea kifaransa mungu akipenda anaweza kwenda nchi mbalimbali .je atakwenda tution ngapi?. Tambua kujua kiingere siyo kwamba ndiyo unajua kila kitu. Epuka utumwa penda kwako. Aibu imempata muandishi wa habari kutojua kiswahili maana hii a.mashariki
 
Acha utumwa wewe kwani kiswahili ndio hakifai? Juzii niliona mchezaji wa somalia alikuwa nyota wa mchezo mtangazaji Akamhoji kingereza jamaa Alijibu kisomalia Na akapewa king'amuzi chake akasepa...
 
Vipi angekua mchina afu akaomba kuulizwa kwa kichina, sredi ingekuwepo?

Samata ni mzalendo. Wewe ulitaka alaximishe kuongea asichojua?. big up ms.

Wewe usiwe mtumwa,sisi tupo afrika mashariki tunataka lugha yetu ikue, pia wao ndio walimfuata kufanya naye mahojiano, kwahyo hana uamuzi wa kuchagua lugha anayotaka yeye,pia jifunze pia kuangalia wachezaji wa mbele wanapenda kuhojiwa kwa lugha za kwao, sawa mjomba?

Kuelimika sio kujua English,acha ukoloni mamboleo JITAMBUE SHTUKA JISIKIE AIBU

Kwa nchi kuwa na lugha yake ya mawasiliano ni mafanikio tosha kabisa, soka lichezwe Africa Mashariki alafu lugha ya mawasiliano iwe kizungu si majanga haya, mbona yeye amechemka kuandika professional kwa kuandika profeshenal
 
Lugha za watu hizo kuchemka kawaida kama wewe ulivyochemka kuandika profeshenal badala ya professional, michuano ichezwe Africa mashariki kwa waswahili na bado mkomae na lugha za watu, hivi kwanini kwa kukijua kiswahili isiwe sababu ya kujivunia kwani kila kitu tunategemea kutoka nje but mwisho wa siku tumeweza kuwa na lugha yetu wenyewe kama ilivyo kwa wachina. Kwahiyo ili uwe professional unahitaji kujua kiingereza?

we si una ona kichina?
 
Wewe usiwe mtumwa,sisi tupo afrika mashariki tunataka lugha yetu ikue, pia wao ndio walimfuata kufanya naye mahojiano, kwahyo hana uamuzi wa kuchagua lugha anayotaka yeye,pia jifunze pia kuangalia wachezaji wa mbele wanapenda kuhojiwa kwa lugha za kwao, sawa mjomba?

alianza na kidhungu cha kikongo mbonaa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom