Mbwa hufanana a mabwana wao

MAMMAMIA

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
3,811
1,604
Marafiki watano walishinda juu ya umahri wa mbwa wao, kila mmoja akdai wake ni mahiri zaidi:
Mbwa wa Fundi Mjenzi akakusanya vifaa akajenga nyumba
Mbwa wa Mhasibu akaenda kwenye kabati akarudi na boksi la biskuti 30 akazigawa mafungu matano ya sita-sita.
Mbwa wa Mpishi akaingia jikoni na kutayarisha aina mbali za vyakula kwa muda mfupi sana
Mbwa wa Fundi Kompyuta katengeneza programu na "database", wote wakashangaa.

Akabakia Rais na mbwa wake, alipoona wote wanamshangaa hafanyi kitu akamwamrisha mbwa wake aoneshe umahiri wake:
- Akataifisha nyumba ilojengwa
- Akala biskuti zote na vyakula vyote peke yake
- Akamwaga kinyesi juu ya kompyuta na zulia
- Akaamrisha atangazwe yeye kuwa ndie mahiri zaidi na kwa hivyo mshindi, asitokee mtu wa kupinga uamuzi huo na hakuna mahakama ya kuweza kumshitaki.
 
Back
Top Bottom