EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Kiwanga (Chadema) yuko nje ya nchi kwa matibabu ya moyo hali ambayo imesababisha kesi inayomkabili pamoja na washitakiwa wengine kuahirishwa hadi mwezi ujao. Taarifa hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki mahakamani ambapo Kiwanga pamoja na wanachama wengine watatu wa Chadema wanakabiliwa na mashitaka matatu ya jinai dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatma Kimario.
Kwa mujibu wa hakimu, amepokea taarifa ya maandishi kutoka kwa daktari inayoeleza kuwa Kiwango yuko India kwa matibabu ya moyo. Mashitaka yanayowakabili ni matumizi ya lugha ya matusi, shambulio la madhara mwilini na kumweka chini ya ulinzi isivyo halali, tukio lililotokea Septemba mwaka jana wilayani Igunga wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Igunga.
Kwa mujibu wa hakimu, amepokea taarifa ya maandishi kutoka kwa daktari inayoeleza kuwa Kiwango yuko India kwa matibabu ya moyo. Mashitaka yanayowakabili ni matumizi ya lugha ya matusi, shambulio la madhara mwilini na kumweka chini ya ulinzi isivyo halali, tukio lililotokea Septemba mwaka jana wilayani Igunga wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Igunga.