skilled masala
Senior Member
- May 2, 2019
- 118
- 158
Kama wapo private sectors ambao wangependa kuwekeza kwenye huu mradi sioni kama ni vibaya wakipewa ila kwa conditions faidishi kwa kila upande.Mbunge wa Handeni Mjini CCM, Reuben Kwagilwa, ameishauri Wizara ya Fedha na Mipango, waangalie namna ya kufadhili miradi mikubwa kwa mfumo wa dhamana ya miundombinu ‘infrastructure bond’ ili kuiwezesha Serikali kutoa huduma za wananchi kila siku.
Amesema isipofanya hivyo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa wa SGR utachukua miaka 81 kukamilika kwakuwa mpaka sasa hata kilometa 300 bado hazijakamilika.
Kwagilwa ametoa ushauri huo jana bungeni wakati akichangia mjadala wa mpango wa tatu wa maendeleo wa kitaifa kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2021/22 - 2025/26,
“Standard Gage Railway tunayoijenga ukijumlisha zile njia tunazotakiwa kujenga ni kilomita 4886 hapo naongelea zile njia tu, siongelei mahala ambapo reli huwa zinapishana. mpaka sasa tumeshajenga kipande kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kilometa 300 na tunaendelea kipande cha Morogoro Makutupora kilometa 422 lakini tuko upande mwingine wa Isaka na Mwanza kilometa kilometa 249,
Kwa namna tunavyohudumia mradi huo kama tukiendelea kwa mfumo huo tutajenga kwa miaka 81 kwa nchi nzima ikiwa miaka mitano tumejenga kwa kilameta 300 na kilometa zilizosalia tutazijenga kwa miaka 81 hii katika nchi ambayo inapambana kujenga uchumi kasi hiyo haikubaliki na imegharimu Sh11 trilioni ambazo ni ‘hido investiment’ kwa sababu hatutaanza kutumia leo.,”amesema
Ameongeza “Serikali inatakiwa kujifunza na kuondokana na mfumo wa kizamani wa kufadhili miradi mikubwa kwa sababu inajipa pressure kubwa halafu inashindwa kupeleka huduma za kila siku kwa wananchi wake” amesema