Mbunge: SGR itajengwa kwa miaka 81

Mbunge: SGR itajengwa kwa miaka 81

Angekuwepo Magufuli huo huo mradi ungekamilika kwa muda mfupi .Ardhi ya Dar mpaka morogoro ina changamoto nyingi kwanza ni mchanga ardhi yake sio ngumu pili ni mito mingi na ardhi tope nyingi lakini ukitoka morogoro ukiingia Dodoma kwenda mbele ardhi ngumu unaenda spidi ya kufa mtu kujenga
Huyo mbunge hayuko sahihi hakuangalia hali ya ardhi alipofanya hizo calculations anafikiri ardhi zote ziko sawa na kipande hicho cha morogoro na Dar

Magufuli alikomaa waanze kwanza sehemu korofi kipande cha Dar na Morogoro akijua wakimaliza hicho huko mbele itakuwa spudi kali ya ujenzi
Unaongea kwa upole na unyenyekevu kama siyo wewe vile, ila hongera naona akili zimekaa sawa sasa. Tuombe kwa Mola tusijepata mtu kama jiwe abadani.
 
Miradi ya SGR, stiglaz, daraja la busisi na hata manunuzi ya ndege itakuwa na variations kibao kutokana na serikali kushindwa kukidhi matakwa ya mikataba kutokana na kuhitaji pesa nyingi na hivyo mkandarasi kudai fidia.......hii ndo shida ya kukurupuka kwa sababu hiyo miradi haikupata mjadala wa kutosha ndani ya bunge, miongoni mwa wataalamu na wadau mbalimbali...mungu mtu akiamua basi anafanya chochote kile.
 
Ile neno laana ndo mbaya brother
Sasa ameua akina Ben saaanane,maiti za watu zilikuwa zinaokotwa kwenye viroba baharini,amenyang'anya watu haki zao za kuchagua viongozi wanaowataka kwa kuiba kura,watu wasiokuwa na hatia wamebambikiwa kesi za kuhujumu uchumi na kuozea ndani,ameua watu kwa Corona kupitia leadership negligence,watu wamekuwa masikini kwa sababu ya kufunga biashara zao kwa sababu ya sera mbovu zake za uchumi,ametumia jeshi la polisi kunyanyasa watu na kadhalika je,hii siyo laana ni nini?
 
Evidence iko wapi?
Sasa ameua akina Ben saaanane,maiti za watu zilikuwa zinaokotwa kwenye viroba baharini,amenyang'anya watu haki zao za kuchagua viongozi wanaowataka kwa kuiba kura,watu wasiokuwa na hatia wamebambikiwa kesi za kuhujumu uchumi na kuozea ndani,ameua watu kwa Corona kupitia leadership negligence,watu wamekuwa masikini kwa sababu ya kufunga biashara zao kwa sababu ya sera mbovu zake za uchumi,ametumia jeshi la polisi kunyanyasa watu na kadhalika je,hii siyo laana ni nini?
 
Huna macho ya kuona,
Hata ivyo palikuwa na miaka mitano Tena Kama Mungu angempa angefanya zaidi ya hayo pengine ungeweza kuona,
Haya kakwachia sasa, tuone nawe utafanya Nini.
Unafikiri watu walimsifia bureee..
Alisifiwa na watu wapumbavu kama wewe, samahani kama umekwazika kuambiwa ukweli.
 
Cha ajabu awamu iliopita kabla ya magufuli ccm ilikuwa imezama ,,magufuli akafanya jitihada zake ccm ikakaa kwenye reli yani ilifika kipindi ukivaa tisheti ya ccm unaonekana waajabu nakuzomewa juu.
Naona tutarudi kule

Magufuli aliisimamisha CCM kwa nguvu ya dola lakini si kwa hoja. Leo hii ikijulikana kuwa Polisi hawatachukua hatua mwanaCCM akizomewa mitaani, subiri uone wangapi watakuwa na jeuri ya kuvinjari na magwanda ya kijani kwa street.
 
Huduma ipi iliyoshindwa kupelekwa?

Huyu naye ni mjinga mjinga
Nadhani wewe ndo mjinga kea Sababu CAG amesema tumepigia faini ya bil14 kea sababu ya kushindwa kuipeleka HUDUMA kwa wakati, sasa Bil 14 zingeweza kujenga mabweni mangapi au kukarabati, ukizingatia kuwa Magufuli hostel ziligharimu bil 20 tu.
 
I know that but hebu tupunguze unafiki sisi wa tz
Shida sio unafiki shida ni pale kiongozi anapopenda kusifiwa tu na ukimkosoa unaambiwa umetumwa na mabeberu. Mtu kama huyo ni kumsifia tu hamna namna.

Hapo tatizo ni magu.
 
Cha ajabu awamu iliopita kabla ya magufuli ccm ilikuwa imezama ,,magufuli akafanya jitihada zake ccm ikakaa kwenye reli yani ilifika kipindi ukivaa tisheti ya ccm unaonekana waajabu nakuzomewa juu.
Naona tutarudi kule
Awamu hii ya kuwekwa kwenye viroba, kukutwa cocobeach, kutishiwa kuuliwa kila siku na wasiojulikana, nani angethubutu kuzomea mwanaccm yeyote??? Awamu ambayo watu wameishi kwa hofuuuuu.
 
Evidence iko wapi?
...
100745.jpg
20210318_.jpg
00946.jpg
 
Mbunge wa Handeni Mjini CCM, Reuben Kwagilwa, ameishauri Wizara ya Fedha na Mipango, waangalie namna ya kufadhili miradi mikubwa kwa mfumo wa dhamana ya miundombinu ‘infrastructure bond’ ili kuiwezesha Serikali kutoa huduma za wananchi kila siku.

Amesema isipofanya hivyo mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa wa SGR utachukua miaka 81 kukamilika kwakuwa mpaka sasa hata kilometa 300 bado hazijakamilika.

Kwagilwa ametoa ushauri huo jana bungeni wakati akichangia mjadala wa mpango wa tatu wa maendeleo wa kitaifa kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2021/22 - 2025/26,

“Standard Gage Railway tunayoijenga ukijumlisha zile njia tunazotakiwa kujenga ni kilomita 4886 hapo naongelea zile njia tu, siongelei mahala ambapo reli huwa zinapishana. mpaka sasa tumeshajenga kipande kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kilometa 300 na tunaendelea kipande cha Morogoro Makutupora kilometa 422 lakini tuko upande mwingine wa Isaka na Mwanza kilometa kilometa 249,

Kwa namna tunavyohudumia mradi huo kama tukiendelea kwa mfumo huo tutajenga kwa miaka 81 kwa nchi nzima ikiwa miaka mitano tumejenga kwa kilameta 300 na kilometa zilizosalia tutazijenga kwa miaka 81 hii katika nchi ambayo inapambana kujenga uchumi kasi hiyo haikubaliki na imegharimu Sh11 trilioni ambazo ni ‘hido investiment’ kwa sababu hatutaanza kutumia leo.,”amesema

Ameongeza “Serikali inatakiwa kujifunza na kuondokana na mfumo wa kizamani wa kufadhili miradi mikubwa kwa sababu inajipa pressure kubwa halafu inashindwa kupeleka huduma za kila siku kwa wananchi wake” amesema

Sisi ni matajiri ,tunajenga kwa fedha zetu za ndani.
 
Aliiba na miradi ilienda umeme kila kijiji ulienda , Elimu bure ilipatikana vituo vya afya nchi nzima vilijengwa na barabara za mataa mitaani uswahilini zilijengwa nk hakuna kilichosimama sababu ikiwa moja kuu Magufuli alisema nchi yetu ni tajiri

Fikiria yote yaliwezekana pamoja na CAG kusema kuna wizi!!! Midege ilinunuliwa Cash na maneli kibao yalijengwa .Sasa serikali iliyopo wasio wezi changamoto iko kwao.Je waweza kufanya mambo makubwa kwa nchi kama aliyofanya huyo wanayemwita fisadi papa na kibaka Magufuli? tusubiri muda ni mwalimu mzuri tutajua kati ya fisadi papa magufuli na watakatifu wao nani zaidi.Majaji kwenye hili watakuwa wananchi wanyonge walio wengi sio CAG na viripoti vyake vya kwenye vikaratasi vya toilet papers
MWAMBIENI CAG, SISI TUMERIDHIKA!!

1. Mwambieni CAG kwamba sisi wenyewe tumeridhika, tumezoea kuibiwa. Mwambieni tofauti ya wizi wa zamani na huu ni kwamba wizi wa sasa unafaida kwa Wananchi wala asiumize kichwa. Mwambieni sisi Wananchi hatuna tatizo na hasara au wizi uliofanyika wakati wa JPM. Sisi tumeridhika hivyohivyo kwa sababu tuna macho ya kuona!!

2. Mwambieni CAG kwamba tuliibiwa hapa kupitia EPA. Pesa bilioni 135 zikaliwa na watu wachache, wakati huo elimu bure ilikua bado kuja. Mikopo ya elimu ya juu ilikua ni songombingo kwa hiyo hatuoni hatari kuibiwa sasa huku elimu bure ikiwa imeanzishwa na mikopo ikitoka kwa wakati. Sisi tumeridhika kabisa na hasara au wizi wa JPM!!

3. Mwambieni CAG kwamba tuliibiwa hapa bilioni 300 Serikali ikilipa Makampuni hewa katika kashfa ya MEREMETA. Mwambieni hapakua na tatizo lolote na wakati huo bajeti ya Dawa ilikua chini ya bilioni 30 lakini sasa na wizi wa JPM umepandisha bajeti ya DAWA zaidi ya mara tisa; yaani bilioni 270. Mwambieni kwa wizi huu Mungu atupe nini? Tumeridhika sana na wizi wa JPM.

4. Mwambieni CAG kwamba tulishaibiwa sisi kwenye mauzauza ya uwekezaji wa Bulyanhulu na Buzwagi na hata leo hakuna maelezo ya yanayoeleweka. Kodi hazikulipwa na pesa zikapigwa na wajanja wachache. Wakati huo wote madini na migodi yote ilikua ni mali ya wawekezaji wasiolipa kodi, Wananchi ilikua ni marufuku kukaribia migodi katika nchi yao. Kama JPM ameiba halafu wananchi wanachimba madini wenyewe kwa uhuru, ninaumia kwamba atakua ameiba kidogo sana. Wizi wenye manufaa kwa umma una maana zaidi kuliko wizi usio na manufaa. Sisi tumezoea kuibiwa, lakini kwa huu wa JPM tumeridhika.

5. Mwambieni CAG kwamba sisi tumezoea kuibiwa. Tumeshaibiwa haswa, ilikuja hapa tukaibiwa katika Mkataba wa kijinga wa DOWANS. Nchi ikalipa bilioni 111 kwa sababu ya maslahi ya watu wachache. Wakati tunaibiwa kupitia DOWANS, Mv. Victoria ilikua inalaza watu siku mbili ziwani kwa ubovu wake. Maisha yao yalikua hatarini kila safari, leo JPM akiiba au akitutia hasara ya bilioni 60 huku Mv. Victoria ikiwa MPYA kuna tatizo gani? Meli mpya tele kuanzia ziwa Nyasa, Tanganyika na Bahari ya Hindi Kilwa. Tunapenda wizi wa namna hii, angeiba kabisa za kutosha akajenga nyumba nzuri kama wenzake, akamiliki magari za mizigo meupe kukuki na sheli za kumwaga. Au akamilika supermakert za Da'slam kama wenzake. Sisi kuibiwa tumezoea, wizi wa JPM una manufaa, tumeridhika.

6. Mwambieni CAG kuwa sisi tumezoea kuibiwa asijiumize bure na ma-press ya kutangaza vi-wizi vya kitoto hivyo. Tulipigwa hapa pesa TAKATIFU katika Mkataba maarufu wa RICHMOND ulioondoka na Serikali ya mwaka 2008 hadi sasa hakuna kilichofanyika. Wakati tukipigwa pesa za Richmond daraja la Mfugale lilikua halipo, Daraja la Ubungo (Kijazi Interchange) haikuwahi kufikiriwa, Daraja la Tanzanite (Salender) lilikua katika ndoto, lile la Busisi halikufikiriwa kabisa. Kama tumeibiwa leo na mambo yote haya yamefanyika mwambieni CAG sisi roho kwatu, tumeridhika riport zake tupa kule hatusikii la mwazini wala mnadi swala. Tumefunga masikio!!

7. Mwambieni CAG sio hata siku nyingi zilichotwa BOT bilioni 306 kwa kilichoitwa kashfa ya TEGETA ESCROW. Nchi ikaibiwa tena na wajanja wachache, wakabeba pesa kwenye masandarusi. Wakati tukiibiana bilioni 306 za Escrow umeme vijijini ulikua unaunganishwa kwa Tsh. 454,000 ila kwa wizi wa JPM umeme vijijini unaunganishwa kwa Tsh. 27,000; asilimia zaidi ya 70 umeme umefika vijijini. Wizi mzuri kiasi gani huu!? Sasa tunajenga megawati 2400 kutoka Bwawa la Nyerere ili umeme ushuke zaidi. Ingalikua uwezo ni wangu ningalimrudisha mtu huyu aendelee kuiba na kutia hasara zaidi kwa sababu wizi na hasara zake zina manufaa kwa watu. Mwambieni CAG sisi tumeridhika hivyohivyo, atuwache!!

8. Mwambieni CAG sisi tumewahi kuibiwa Twiga mzima akabebwa na shingo yake akaondoka zake. Hii nchi tunaibiana na Wanyama yeye anahangaika na vipesa vidogo vidogo vya matengenezo ya ATCL. Mwambieni wakati tukiibiana TWIGA upatikanaji wa maji Vijijini ulikua ni asilimia 47 na sasa kwa wizi na hasara za JPM upatikanaji wa Maji vijijini umefikia asilimia 70.1 huku mijini upatikanaji ukitoka asilimia 74 hadi 84. Ni mtu mjinga pekee anaweza kuchukizwa na wizi wa JPM, mwambieni CAG sisi tumeridhika tunatamani angekuwepo aibe tena. Hatutakagi ujinga!!

9. Mwambieni CAG kuwa tumeibiwa sana nchi hii. Wakati wote tuliibiwa huku Nchi ikiwa haina Ndege hai hata moja. Mwambieni leo tuna Ndege 11 za kwetu wenyewe. Hizo hasara za ATCL zisimuumize kichwa, hakuna biashara isiyo na hasara, JPM keshawawekea mtaji na heshima ni wajibu wao kutafuta akili za kupata faida sio kuua mtaji. Mwambieni CAG, sisi tunampenda mwizi anayeiba halafu akanunua Ndege kwa ajili ya Nchi nzima, akajenga reli ya kasi, stend kibao za kisasa, masoko kwa ajili ya biashara nk. Kwakweli sisi tumeridhika sana na wizi huu!! Mungu amlaze mahala pema JPM, ametutoa tongotongo!!

10. Mwambieni CAG asipoteze nguvu zake bure kwa sababu hata hao wezi huwa hawafanywi kitu. Mwambieni tumezoea na zaidi tumeridhika na wizi au hasara za JPM. Mwambieni CAG nchi hii imeongozwa na wezi wengi lakini huyu alikua ni mwizi wa heshima. Tunampenda, tutammiss hivyohivyo na yeyote mwenye kumchafua atachafuka kwanza yeye. Tutakua Taifa la kijimga sana kuacha ALAMA za mtu huyu zifutwe na watu wajinga, wavivu
wasio na lolote walioachiwa Nchi wasiongoze wakihangaika na umbea, udaku na ushambenga.
Kwa taarifa yenu #SISI TUMERIDHIKA HATA ANGEIBA NCHI YOTE AIUZE!! Tuna macho ya kuona, tus ichoshane.
#TutakukumbukaDaimaJPM.

C$P
 
Mifisadi.nanibya CCM aliinyoosha barabara sada hivi CCM ina pesa nyingi baada ya kuibana mifisadi ya mali za chama pesa sasa inaonekana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom