Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Mbunge wa Rombo, Mhe. Joseph Selasini kapata ajali mbaya sana muda si mrefu.
Ajali hiyo imemtokea akiwa safarini toka Arusha kwenda Rombo na ni eneo la Bomang'ombe mjini.
Watu watatu akiwemo mamake mzazi wamekufa papo hapo.
Mhe. Selasini amepekimbizwa Hospitali ya wilaya ya Hai pale Bomang'ombe; hali yake si nzuri.
Ajali hiyo imemtokea akiwa safarini toka Arusha kwenda Rombo na ni eneo la Bomang'ombe mjini.
Watu watatu akiwemo mamake mzazi wamekufa papo hapo.
Mhe. Selasini amepekimbizwa Hospitali ya wilaya ya Hai pale Bomang'ombe; hali yake si nzuri.
Ni kweli. Mbunge Joseph Selasini kapata ajali eneo la Bomang'ombe Mjini, karibu na pale wanapouza nyanya...
Gurudumu moja la mbele la gari alilokuwa akisafiria lilipasuka. Gari likaacha njia likaangukia darajani. Kwa wale wanaofahamu eneo hilo kuna daraja maarufu linaitwa Daraja la Mjapani.
Alikuwa akitokea Arusha kumtoa baba yake hospitalini. Yeye na Baba yake wamesalimika. Walikuwa wamefunga mikanda. Ndiyo iliyowasaidia. Wengine watatu, mama yake, shangazi yake na mama mwingine, wamekufa pale pale.
Mbunge anaendelea vizuri. Amelazwa Hospitali ya Wilaya ya Hai, Anaongea na anatembea. Magari mawili ya Ambulence ndio yamefika, watahamishiwa KCMC kwa uchunguzi zaidi.
Tumaini Makene,
Kurugenzi ya Habari - CHADEMA