Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,897
- 941
MBUNGE NDAISABA AVUNJA NGOME ZA CHADEMA NGARA, WAPIGWA MLALO WA MENDE
Mbunge wa Jimbo la Ngara Mkoa wa Kagera, Mhe. Ndaisaba George Ruhoro katika ziara yake ya kikazi Jimboni wakati akizungumza na wananchi ameendesha Kampeni na zoezi la kuwapokea na kuwakaribisha mamia ya wanachama wa CHADEMA ambao wameapa rasmi kukitumikia Chama Cha Mapinduzi
"Karibuni kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM), nataka niwathibitishie, CCM ina viongozi wazuri na kwa CCM mnakwenda kuyashuhudia maendeleo. CCM kitaendelea kuongoza Tanzania kwa miaka mingi sana. Mmefanya maamuzi mazuri kuhamia ndani ya CCM" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara
"Nilisema CHADEMA kwisha, kwisha, kwisha kabisa! Nyanganyanga, Ndembendembe, Mlalo wa Chali, Kifo cha Mende! Asubuhi nimekutana na meseji kutoka CHADEMA Makao Makuu na wamenipigia wanasema niliwatukana. Nasema hivi wameniongeza kasi, tutaendelea kuwavuna CHADEMA warudi CCM" - Mhe. Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Jimbo la Ngara
Mbunge wa Jimbo la Ngara Mkoa wa Kagera, Mhe. Ndaisaba George Ruhoro akiimba pamoja na wananchi wimbo na kucheza wimbo wa kumpenda na kumsifu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.