Mbunge Nancy Nyalusi ahoji uhalali wa KADCO kuendelea kusimamaia shughuli za Uwanja wa Ndege wa KIA

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944

MHE. NANCY NYALUSI AHOJI KADCO INASIMAMIA SHUGHULI ZA UWANJA WA NDEGE WA KIA KWA MKATABA UPI?

"Nampongeza sana CAG kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kuweza kubaini madudu. Ucheleweshaji wa Malipo kwa wakandarasi umesababisha riba ya Shilingi Bilioni 68.77 kwa Serikali kwa taasisi 12. Hapo hatujazungumzia kwenye Halmashauri na Wizarani" - Mhe. Nancy Nyalusi, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Iringa

"Hali ni mbaya, tatizo ni kubwa, limeendelea kukua siku kwa siku. Ifike mahali watendaji wa Wizara wamuonee huruma Mheshimiwa Rais. Mheshimiwa Rais anahaingaika usiku na mchana kuhakikisha kwamba anatafuta fedha kwaajili ya miradi ya Maendeleo" - Mhe. Nancy Nyalusi, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa

"Mimi nina ushauri (Kuhusu ripoti ya CAG) Naomba ufanyike ukaguzi Maalum kwenye taasisi 12 ili tujue chanzo cha tatizo ni nini ili tuweze kutatua tatizo hili maana inaweza kuonekana ni chaka la watu kuiba fedha za Serikali" - Mhe. Nancy Nyalusi, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa

"Bunge la 12 Mkutano wa 9 tarehe 2 Novemba, 2022 Bunge liliadhimia kwamba shughuli zote za Uwanja wa Ndege wa KIA zisimamiwe na TAA, lakini hadi kufikia Septemba 2023 shughuli za KIA zilikuwa bado zinasimamiwa na KADCO. Waziri atuambie KADCO inasimamia kwa Mkataba upi na utaratibu upi" - Mhe. Nancy Nyalusi, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa

"Wizara husika imepuuzia azimio la Bunge kwasababu hawajafanyia kazi utekelezaji na hamna taarifa yoyote na hii ni kuonyesha dharau kubwa kwa Bunge. Haiwezekani Bunge tunakaa tunaweka maazimio lakini hakuna kinachofanyiwa kazi" - Mhe. Nancy Nyalusi, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2023-11-03 at 19.16.42.mp4
    29.1 MB
  • WhatsApp Image 2023-11-03 at 19.04.57.jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-03 at 19.04.57.jpeg
    436.3 KB · Views: 4
Naona Ole Sendeka kagusia as if mmiliki ana vinasaba vya wale wa diiipiii ,wakati serikali inasema wazi kuwa ni Mali ya serikali. Sasa huyu sendeka sijui hii shaka anaitoa wapi
Mkurugenzi wa KADCO alikuwepo kwenye msafara Dubaï Trade Fair ulioongozwa na Bimkubwa.... Na alishuhudiwa akisaini mikataba ya KADCO na waarabu. Ole Sendeka ana hoja.
 
Naombeni maelezo ya kina hasa watu wa Kilimanjaro na Hai kujua KADCO ni nani na ana maslahi gani kwa serikali maana Bunge limechanginyikiwa
KADCO ni ya serikali kwa 100%
TIA ni ya serikali kwa 100%.
KADCO mkataba wake umeisha tangu Juni lakini bado anaendelea kutoa huduma. Something smell fish.
 
Vipi ya DPW?? Na ile ya OBC loliondo?
Mashirika yote yanayoitwa ya umma na makampuni yaliyotaifishwa mwaka ya 1967 kutoka kwa wahindi na waarabu yalikuwa yanafanya vizuri wakati wa uhai wa Mwl J.K.Nyerere. Baada ya hapo yalibakia kuwa mitaji ya watendaji wake wakuu wakishirikiana na viongozi wa juu walioamua kufumbwa macho kwa mgao maarufu wa 10%.

Mkapa alipoingia ndio kabisa mlango wa ufisadi wa mali ya umma ndipo ulipofunguliwa rasmi kupitia kale kamradi ka kubinafsisha mashirika ya umma. Unachokiona sasa, Bandari, Loliondo, KADCO ni sehemu ndogo tu ya mashirika mengine ambayo hayatajwi tena licha ya kuendelea kuwepo kimya kimya ni muendelezo wa ufisadi unaoendelea bila kujali malalamiko ya wananchi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom