Nancy nyalusi (mb) atoa msaada magodoro 50 kwa shule ya walemavu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944
MHE. NANCY NYALUSI (MB) ATOA MSAADA MAGODORO 50 KWA SHULE YA WALEMAVU

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Mhe. Nancy Nyalusi tarehe 24/2/2023 amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ambapo Pamoja na mambo mengine ametembelea Shule ya Msingi Mchanganyiko Makalala iliyopo wilayani humo na kutoa msaada wa magodoro 50 kwa uongozi wa shule hiyo ili kusaidia kupunguza mzigo wa changamoto ya magodoro katika shule hiyo ambayo ina idadi kubwa ya wanafunzi wenye ulemavu mbalimbali.

Katika ziara hiyo Mhe. Nyalusi ameongozana na viongozi mbalimbali wa UWT Wilaya ya Mufindi.

Aidha, Mhe. Nyalusi ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kufanya maboresho kwenye miundombinu ya elimu katika maeneo mengi mkoani Iringa jambo ambalo amesema halipaswi kufumbiwa macho badala yake ni vyema likasemwa ili kila mmoja ajue mambo yanayofanywa na Serikali.

#KAZIIENDELEE #CCM #IRINGA
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.14.jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.14.jpeg
    67.5 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.14(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.14(1).jpeg
    60.5 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.17(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.17(2).jpeg
    62 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.17(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.17(1).jpeg
    55 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.17.jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.17.jpeg
    50.1 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.16(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.16(2).jpeg
    67.3 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.16(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-25 at 13.27.16(1).jpeg
    73.2 KB · Views: 3
Sijali kama CHADEMA watakuwa au watakosa wabunge bungeni bila aina hiyo ya ubunge. Kote kwenye mataifa ya demokrasia ya kweli ubunge unatokana na wapiga kura tu.
Huwezi kuwa mbunge bila kuchaguliwa na kura za wananchi katika jimbo la uchaguzi.
Kwa sababu zipi Ubunge wa Viti Maalumu ufutwe? Kwani waliouweka walikuwa na sababu zipi? CHADEMA isingekuwa Ubunge wa Viti Maalumu akina Mdee wangekuwa mjengoni now?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom