Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 942
MHE. JULIANA MASABURI AZUNGUMZA NA VIJANA WA BARAZA LA UVCCM WILAYA YA BUNDA MKOA WA MARA
Mbunge wa Viti Maalum Vijana Taifa, Mhe. Juliana Didas Masaburi tarehe 15 Julai, 2023 amekutana na Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bunda lenye Majimbo matatu ya Bunda Mjini, Bunda Vijijini na Mwibara.
Katika Baraza hilo Vijana wa UVCCM Bunda wamemueleza Masaburi kuwa wanakutana na changamoto za Kukosa Miradi; Kutoshirikishwa kwenye Miradi ya Serikali; Ukosefu wa Kadi za UVCCM na Vijana wanaojitoleq kufanya kazi Serikalini kutopewa kipaumbele nafasi zinapotolewa.
Aidha, Mhe. Juliana Masaburi amewachangia Vijana UVCCM Bunda Viti 50@15,000 vyenye thamani ya shilingi 750,000; na ameahidi kuwapatia Mashine ya Kufyatulia Matofali yenye thamani ya Shilingi Milioni 7,000,000 kama mradi wa UVCCM Wilaya ya Bunda
Vilevile, Mhe. Juliana Masaburi amewasihi Vijana kuendelea kuwa na mshikamano kwani wao ndiyo jeuri ya Chama Cha Mapinduzi huku akiwataka kuunga mkono kwa vitendo kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Serikali awamu ya sita inayosimamiwa na Chama Cha Mapinduzi chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan
Attachments
-
WhatsApp Image 2023-07-19 at 14.05.55.jpeg71.1 KB · Views: 4
-
WhatsApp Image 2023-07-19 at 14.05.53.jpeg74.2 KB · Views: 4
-
WhatsApp Image 2023-07-19 at 14.05.52(2).jpeg93.7 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-07-19 at 14.05.52.jpeg77.8 KB · Views: 6
-
WhatsApp Image 2023-07-19 at 14.05.50(1).jpeg102.3 KB · Views: 3
-
WhatsApp Image 2023-07-19 at 14.05.50.jpeg79.8 KB · Views: 4