Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,897
- 941
MBUNGE GULAMALI ATOA MIFUKO 700 YA SIMENTI UJENZI WA SHULE NA ZAHANATI JIMBO LA MANONGA
Mbunge wa Jimbo Manonga Wilaya ya Igunga, Mhe. Seif Khamis Gulamali ameendelea na ziara yake katika Vijiji vya Kata ya Uswaya na kutoa Mifuko 700 ya Simenti kwaajili ya kusaidia ujenzi wa Shule za Msingi na Sekondari na Zahanati.
Ziara ya Kikazi aliyofanya katika Kata ya Uswaya kwa Vijiji vya Chalamo, Utuja, Uswaya na Mwakadele ambapo ameweza kukagua Miradi, Kuzungumza na Wananchi na Kupokea Zawadi kutoka kwa wananchi
Mbunge Gulamali pia amegawa Vifaa vya Michezo kwa Vijiji vyote na Shule zote 3 za Msingi na Sekondari lakini Pia nimetoa mifuko 700 ya Simenti kwa Miradi mbalimbali kwenye Kata ya Uswaya inayohusu Ujenzi wa Shule Mpya ya Msingi, Ujenzi wa Zahanti na Ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Afya
Akizungumza na wananchi waliohudhuria na kushuhudia michezo mbalimbali, Mhe. Gulamali amewashukuru sana wananchi na viongozi wa Vijiji kwa Mapokezi Mazuri na Upendo waliouonyesha kwake na kusema kwamba "Nasema Asanteni sana Wana Uswaya"