Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Mbunge Godbless Lema akamatwa na polisi

Habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa Askari Polisi walivamia nyumbani kwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mh Godbless Lema alfajiri ya leo na kumkamata.
Hivi sasa yupo central police ya Arusha.

Sababu za kukamatwa kwake haijajulikana bado....


Tutawajuza kila kitakachokuwa kinajiri
Sasa wakuu wa vitu vya polis imekuwa ni ujiko kwao kuwakamata wabunge wa upinzani inatumika Kama daraja la kujipatia vyeo na sifa , Safari hii Tanzania itakuwa kama Uganda yaani wanasiasa wajipange kuteseka sana .
 
Sasa huko ndio ataenda kuongea vizuri. Unavijua vyombo vya dola kamanda?
Umewahi ingia mahabusu na kupewa kibao au unasimuliwa tu? Vyombo vya dola ni pamoja na polisi,wapelelezi na special...
 
Safari hii JPM atakuwa katibu mwenezi wa kuiweka chadema kwenye peak kuliko mtu mwingine aliye wahi kutokea
 
Safi sana hii italeta utulivu maana walivimba kichwa
 
Ndugu zangu wanaarusha na watanzania wapenda demokrasia kwa ujumla Lema amekamatwa asubuhi ya leo na sasa yuko mikononi wa polisi lakini mipango hii kwa taarifa tulizokuwa nazo walipanga kumkamata Jana tulipoenda mahakamani kwenye swala la Bananga aliyewekwa ndani siku tatu kwa kosa la kusema huwezi angusha ukuta bila 'kuushika ukuta' na hii kamata kamata haitoishia hapo itaendelea.. Nini kifanyike? kwakuwa wameweka mtego wa kuendelea kutukamata kabla ya sept 1 ninawaomba wanaarusha tusijazane polisi tuendelee na maandalizi yetu ya sept 1 kama viongozi Wetu wanavyo tupa maelekezo, Lema watamwachia tu...
 
Safi sana hii italeta utulivu maana walivimba kichwa
 
Kweli Mh. Mbowe kachukua akili zenu zote, ngoja tumwombe awarudishie, baad ya kutafuta sababu kwann kakamatwa ww unaanza ilaumu serikali, kwan yy ni nani mpaka asikamatwe? Tafuta sababu ya yy kukamatwa nenda fuatilia. Kwel Mh. Magufuli kawazidi kete mwaka huu mnahaha kumfukuza na kwan speed yake hamtampata hahaha
 
Sivyo.Lkn kwa sababu nchi hii hakipo chama pinzani makini bado CCM Chakii wataendelea kuongoza tu hadi hapo wapinzani wa kweli watapopatikana.Kinachotufanya(Baadhi yetu)tusiwaamini no huko kushindwa kwenu kusimamia hoja na takarashi zenu!Hilo ni tatizo kubwa.Hamjajipanga kimkakati na ki-sera pia.Itoshe kusema,ninyi bado ni GENGE fulani la watamanio madaraka na si uongozi.JIPANGENI na hasa punguzeni UTOTO.
Utoto ni nini? Kudai haki ya mikutano ni Utoto , kuzuia au kupiga marufuku mikutano ndiyo Utu mzima ? Tambua aina ya siasa ya CCM hata angekuja Obama Tanzania hawezi kushinda uchaguzi , Nani kakuambia CCM bila kamati za January na wale vijana wake wa IT kuchakachua wangeshinda uchaguzi ? Kama CCM wanataka siasa waruhusu uhuru wa kujieleza , mikutano , maandamano wasiwe wasiwe wapiga ramli kuwa kutakuwa na Fujo wakati hakuna Fujo .
 
Hiyo hadhi ya kuzungumza na JPM kwanza huna!Na hana mda mchafu km huo.
Kwani huyo JPM ndio mungu wa dunia hii mbona sisi wote tunaisi njaa, tunalala hata kama chini, yeye kitandani, alafu pia tutakufa, sasa unapo zungumza hadhi nini maana yake, unadhani pana binadamu ana hadhi zaidi ya mwenzake hadi eti msizungumze, hakika mbora kwenu ni yule anaeniabudu Tu.
Haya, umeridhika
 
Kwani huyo JPM ndio mungu wa dunia hii mbona sisi wote tunaisi njaa, tunalala hata kama chini, yeye kitandani, alafu pia tutakufa, sasa unapo zungumza hadhi nini maana yake, unadhani pana binadamu ana hadhi zaidi ya mwenzake hadi eti msizungumze, hakika mbora kwenu ni yule anaeniabudu Tu.
Kelele za nini sasa?
 
Back
Top Bottom