Mbunge adai hamiliki smartphone!

Mbunge adai hamiliki smartphone!

Ni kweli mkuu na inakuwa na net full time, huko ndio nakimbilia yaani nimesahau kabisa kuhusu smart phone

Uko vizuri maana hunahaja ya kubeba power bank
 
Salary Slip (mwezi uliopita umechelewa sana kutokea; naomba mwezi huu ujitahidi kuwahii...ehehehe)

Anyway kuhusu mada yako:
Kuwa na smartphone ni jambo moja kujua matumizi yake ni jambo lingine tena kubwa...!!!
 
Papa Fransis wa kanisa katoliki ni kiongozi anayeongoza watu wengi duniani, huyo mbunge ambaye ni viti maalumu nimemsikia na kumuona anaweza kuwa muhimu katuka jamii kuliko papa?
Waweza jiuliza kwa nini nauliza hivi, kifupi ni kwamba Papa kwa mara ya mwisho kuangalia Television ni tarehe 7/07/1990 ana miaka 25 hajaangali tv, pia hatumii kabisa internet, akitaka kupata taarifa za kimataifa huwa anatenga dakika kumi kila siku kusoma gazeti moja la Italy

Sasa na wewe umeambiwa hivyo ukaamini au kwa vile ni Maneno ya mtu mzima?
Vitu vingine siyo vya kuamini hata kidogo eti haangaliagi tv na hatumii internet.
 
Salary Slip (mwezi uliopita umechelewa sana kutokea; naomba mwezi huu ujitahidi kuwahii...ehehehe)

Anyway kuhusu mada yako:
Kuwa na smartphone ni jambo moja kujua matumizi yake ni jambo lingine tena kubwa...!!!

Mkuu,huu ukiwa ndio mwezi wa mwisho wa bajeti ya serikali,sijui itakuwaje.

Tusubiri.
 
A E I O U atakuwa anajua tena kwa kigugumizi, ila kikoloni hajui, na smartphone zipo kikoloni zaidi, che teh teh teh

Mgosi moja ya mambo yanayotia aibu mkoa wa Tanga ni huu mzigo walio tuwekea watu wa Korogwe.
 
Mgosi moja ya mambo yanayotia aibu mkoa wa Tanga ni huu mzigo walio tuwekea watu wa Korogwe.

Mngoni anatia aibu wagosi balaa, ila wagosi ndo vilaza wakutupwa, wameshindwa hata kumpa Dr. Mndolwa? Hawa ndugu zangu wa korogwe wanadanganywa kama watoto kisa mbunge maji marefu anawabebea maiti toka magunga hospital,
Safari hii bilashaka yule dada jembe Aminata Sabuni amewapa shule ya kutosha wataichagua UKAWA
 
Sijawahi kuwa na smart phone na sijawahi kukosa usingizi juu ya hilo.
 
Aje nimpe smart phone yangu. Au mganga aliyemsaidia kupata ubunge alimkataza kutumia smart phone?
 
Hivi habari kama hii ya kuianzishia uzi ili tutenge muda tujadili? Salary slip unaniangusha. Sidhani kama ni vema kujadili personal life za watu. yeye anajua anavyofanya mawasiliano. Anzisha mada za maana vinginevyo soma mada za wengine kama mimi.Sio kila kikujiacho ni cha ku share
 
Mimi mwenyewe situmii simu janja(smartphone) naona si ajabu.
 
Sawa tu!
Tajiri Billionear wa Dunia Warren Buffet mwenyewe mpaka sasa anatumia ka Nokia ka zamaniii!
Kila mtu na mapenzi yake
 
Mngoni anatia aibu wagosi balaa, ila wagosi ndo vilaza wakutupwa, wameshindwa hata kumpa Dr. Mndolwa? Hawa ndugu zangu wa korogwe wanadanganywa kama watoto kisa mbunge maji marefu anawabebea maiti toka magunga hospital,
Safari hii bilashaka yule dada jembe Aminata Sabuni amewapa shule ya kutosha wataichagua UKAWA
Hahahaha ila kawasaidia sana wana korogwe kabla ata ajawa mbunge,enzi hizo maji marefu ni marefu kweli kweli,misikiti kawajengea na miradi mbali mbali ndo maana jamaa bado wataendea kumchagua ,alijua mapema kucheza na akili zao
 
Smartphone mda mwingine michosho, mfano intention yake ni jamii forum lakini ghafla app nyingine hizo zina display notification,mapicha picha,ads kibao labda zinamkwaza!.. Siku hizi kuna ads kwenye DU Speed za maswala ya ngono/mapenzi..notification inakujaa tu pap..alafu utumiaji wa hivi vitu changamoto!
 
Hivi habari kama hii ya kuianzishia uzi ili tutenge muda tujadili? Salary slip unaniangusha. Sidhani kama ni vema kujadili personal life za watu. yeye anajua anavyofanya mawasiliano. Anzisha mada za maana vinginevyo soma mada za wengine kama mimi.Sio kila kikujiacho ni cha ku share
Kitokeo chake na wewe ukaenda kufungua uzi!!!!!
 
Back
Top Bottom