Mbowe: Tumechoka!

Mbowe: Tumechoka!

ccm inavyofanya
Eti anasema amechoka, si ajiuzuru sasa.
kwanza rekebisha kiswahili ndio maana tunazidiwa na wachina, ajiuzulu sio ajiuzuru, ila ccm inavyofanya sio kabisa, yani dah, yani iko juu ya sheria, wanadanganya kuwa mahakama imezuia, mahakama inakanusha kuwa hakuna kitu kama hicho, halafu unachekelea, ati kama kachoka ajiuzulu, mie naona upo katika huo mgawo wa huo ufisadi uliogundulika
 
Kuna mambo yanaendelea yanaonyesha kabisa ni upuuzi wa kisiasa ...kilombero walikamata wabunge wa CDM matokeo yake uchaguzi ukawapa ushindi CCM...Dar wanazuga na kuzunguka tu. Tujaribu kutazama mambo bila kuegemea mitazamo ya kisiasa. Kwa haya yanayoendelea wenye akili wanasoma michezo ya kitoto ya CCM...wataharibu amani bila sababu ya msingi.


Hakuna anayeweza kuharibu Amani TanZania tusidanganyane wala kutishana kwa maana hakuna alikuwa juu ya Sheria za nchi yetu isipokuwa Raisi wa JMTZ!
 
Tanzania nchi yangu! Tusipokuwa makini nchi ilishatekwa! sioni logic ya kuwakamata wabunge na madiwani wakati aliyetoa zuio feki akiendelea kushangilia uraiani! hatakama tungekuwa wendawazimu tungeelewa nini kinachofanyika!!!! siku hizi siyo bao la mkono tena bali imegeuka netball kabisa ya kufunga kwa mikono miwili. Msijidanganye hili siyo jipu!!!!! hii ni kansa ambayo mgonjwa anatakiwa akatwe mguu kabisa au afe!!!!

mimi sielewi sana haya mambo viongozi wa ukawa ninyi ndo wakupelekwa mahakamani!! je ninyi hamuoni shauri lolote la kupereka mahakamani???? mbona wanasheria wazuri mnao?? sielewi!!! Mbowe utachoka sana temu hii na mwisho utakuwa mremavu kabisa siku miguu hiyo ikipigwa kirungu! kaeni mpange uamuzi wa maana ambao mpaka dunia itajua nini kinachoendelea!!!
 
Nionavyo mimi ni kwamba viongozi wachache kutoka vyama vyetu vya upinzani wanapenda kufanya vitendo vinavyoambatana na jazba kwa lengo la kuwaridhisha wapiga kura wao bila kujua kwamba vitendo hivyo ni kinyume cha sheria za nchi matokeo yake wakikamatwa wanasingizia kuonewa. Hakuna mtu ambaye yuko juu ya sheria zilizopo ukituhumiwa kuzivunja huna budi kukamatwa na ufikishwe mbele ya mahakama
 
Aisee Chadema mngejua tu jinsi mnavyotuchosha na siasa zenu za magazeti na TV, mngetafuta tu namna nyingine ya kufanya siasa mtupumzishe na huo utoto wenu, sasa nani atamjua halima au lijualikali bila kujikamatisha kwa polisi halafu kesho yake atangazwe kua kakamatwa, halafu mbowe aseme kua amechoshwa tulijua tu lazima mbowe aseme hivyo ili kujipatia media coverage baada ya Chadema kudoda, hiyo ni nitoke vipi ya wanaukawa, tufanye shughuli zetu tuachane na watafuta umaarufu kupitia magazeti na TV.
 
Hakuna anayeweza kuharibu Amani TanZania tusidanganyane wala kutishana kwa maana hakuna alikuwa juu ya Sheria za nchi yetu isipokuwa Raisi wa JMTZ!

Hata Rais hayupo juu ya sheria. Na amani hujengwa kwenye misingi ya haki na usawa. Unapokuwa na Dola inayokandamiza upande fulani ni hatari kwa mustakabli wa nchi...hii ni fact ndugu sio vitisho. Mifano ipo lukuki dunia nzima kila Bara kihistoria.
 
Nionavyo mimi ni kwamba viongozi wachache kutoka vyama vyetu vya upinzani wanapenda kufanya vitendo vinavyoambatana na jazba kwa lengo la kuwaridhisha wapiga kura wao bila kujua kwamba vitendo hivyo ni kinyume cha sheria za nchi matokeo yake wakikamatwa wanasingizia kuonewa. Hakuna mtu ambaye yuko juu ya sheria zilizopo ukituhumiwa kuzivunja huna budi kukamatwa na ufikishwe mbele ya mahakama

Aliyepeleka zuio feki la kuzuia uchaguzi yuko juu ya sharia>?
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Dua la kuku? Kulaani kumeshasaidia vipi?
 
Kama kachoka aingize Kwato yeye mwenyewe au vurugu zianzie Moshi ths time, haiwezakn Miaka yote Kilimanjaro kuwe tulivu wanaendelea na shughuli za maendeleo fujo waje kuchochea kwny miji ya wenzao, kama tatizo ni Ccm hata moshi Iko chini ya serikal ya ccm
Very narrow mind! Poor you.
 
Na Sisi tumechoka yeye kuendelea kuwa mwenyekiti wa chadema TANGU miaka nenda rudi.
 
Aisee Chadema mngejua tu jinsi mnavyotuchosha na siasa zenu za magazeti na TV, mngetafuta tu namna nyingine ya kufanya siasa mtupumzishe na huo utoto wenu, sasa nani atamjua halima au lijualikali bila kujikamatisha kwa polisi halafu kesho yake atangazwe kua kakamatwa, halafu mbowe aseme kua amechoshwa tulijua tu lazima mbowe aseme hivyo ili kujipatia media coverage baada ya Chadema kudoda, hiyo ni nitoke vipi ya wanaukawa, tufanye shughuli zetu tuachane na watafuta umaarufu kupitia magazeti na TV.
Aisee hivi unakunywa kinywaji gani, weekend nitafute bill on my wallet.
[HASHTAG]#HAPAKAZITU[/HASHTAG]
 
Hakuna anayeweza kuharibu Amani TanZania tusidanganyane wala kutishana kwa maana hakuna alikuwa juu ya Sheria za nchi yetu isipokuwa Raisi wa JMTZ!
Mkuu vipi yule aliyetoa zuio feki,unadhani anatengeneza nini?kwa mujibu wa sheria ilitakiwa awe ndani na kupandishwa kizimbani,kwa kosa LA kudanganya na kuisingizia mahakama,lakini imekuwa kinyume chake na si ajabu akapandishwa cheo
 
Hii nchi ya ajabu sana ............. Mwnyekiti wa kijiji au Mtendaji wa Mtaa wa CCM anaheshimiwa na kuogopwa na police kuliko Mbunge wa Upinzania!!

Bora turudi kwenye mfumo wa chama kimoja tu kama North Korea, China na Cuba!!
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Wawe na nidhamu huwezi kuitwa Mheshimiwa kama huwezi kutawala hasira, Mnamburuta mama wa watu-RAS wa Dar na kuchana nguo zake, Mbona huo udhalilishaji wa huyo mama hamulaani?
Magufuli si Kikwete hamna cha Juisi.
 
Kwa kauli hii moja kwa moja Mbowe amepoteza uhalali wa kuwa mwenyekiti wa Chadema wala kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani....ni ambayo haikutegemewq kutolewa na mtu kama yeye hasa katika kipindi hiki kigumu kwa wabunge wa upinzani hapa Dar.....Mbowe amepoteza mvuto na hamasa kwa wanachama
Hana budi kuondoka na kuwaachia wengine.....

SEMA KWELI JAPO INAUMA....

Ulitaka aongee nini mkuu?
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.

Wawe na nidhamu huwezi
kuitwa Mheshimiwa kama
huwezi kutawala hasira,
Mnamburuta mama wa watu-
RAS wa Dar na kuchana nguo
zake, Mbona huo udhalilishaji
wa huyo mama hamulaani?
Magufuli si Kikwete hamna cha
Juisi.
 
Back
Top Bottom