Mbowe: Tumechoka!

Mbowe: Tumechoka!

Wawe na nidhamu huwezi kuitwa Mheshimiwa kama huwezi kutawala hasira, Mnamburuta mama wa watu-RAS wa Dar na kuchana nguo zake, Mbona huo udhalilishaji wa huyo mama hamulaani?
Magufuli si Kikwete hamna cha Juisi.

Alichokifanya ni sawa? Kudanganya kuna zuio la mahakama kubwe sio kweli, mbona anaogopa kivuli chake
 
Watanzania wamechoka kutawaliwa Na ccm miaka 54 sasa, tumewachoka
Mlishasema mkishindwa kuwatoa CCM madarakani 2015, basi hamtakaa muitoe.
Nafikiri kauli yako ni sawa na mazungumzo baada ya habari.
Carry on...
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Msichoke yakhe! Fuateni nyayo za wazanzibari. Tunamwachia mungu
 
Wapi deusi kibamba na genge lako? Au kwa kuwa ni wa dini yetu ndo hatutoi hata matamko? Wapi kijo bisimba? Wapi tamwa, taula, wapi vituo vya haki za binadamu, demokrasia inakanyagwa mko kimyaaaa! Mbona kipindi cha yule muislamu ilikuwa kama mmepakwa pilipili? Anyway endeleeni na kulindana
KILA KOMENTI KWAKO INAHUSU DINI.BLACK IS DEAD

 
Yupo Arusha,hawezi kusema maana ndiye aliyetoa order.Na pia watasema haimuhusu inamuhusu Mkuu wa Mkoa na Mkurugenzi

saivi yenu Sirro muacheni Rais achape kazi ya kutuondolea umasikini watanzania
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.

Sawa, tupo wengi tuliochoshwa na uonevu huu. Tatizo nadhani hakuna anaejuwa kwamba kuna haki zaidi ya 'haki za binadamu' hebu someni kitu inaitwa CCPR Convention for Civil and Political Rights. Inaelekea watu wengi wa chama tawala na upinzani wenyewe hawana habari au labda wanafikiri hali itabadilika bila kudai ratification na utekelezaji wa CCPR hapa Tanzania na Africa kwa ujumla. Ujinga wa watawala wa Africa wa kukataa kusaini convention hii ni kwamba kuna siku watatoka madarakani, hivyo bila convention hii siku moja watajikuta wameshika kwenye makali panga lilelile wanalolitumia leo dhidi ya wapinzani wao wa kisiasa. Katika nchi zilizokubalia CCPR ni nadra sana kuona au kusikia waandishi wa habari, wanasiasa, wanafunzi, wastaafu, wafanyakazi, waandamanaji, na watu au vikundi mbalimbali wanapigwa au kukamatwa na kuteswa kiholelaholela kama Tanzania na nchi nyingi za Africa. Naamini sisi wananchi sote wa chama tawala na wa upinzani tukiisoma na kuielewa CCPR tutaondokana na uadui wa kisiasa usio na faida kwa ustawi wa Taifa letu. Kama kweli sote tunawapenda watanzanià wenzetu na tunaipenda Tanzania basi tuwatake wabunge wetu watunge sheria ya kutambua na kuheshimu haki zetu za kiraia na kisiasa chini ya CCPR. Vinginevyo wabunge wa upinzani wao wenyewe wataendelea kukamatwa na kuwekwa ndani na hata kupigwa, wakiwa bungeni na uraiani. Ni muhimu wabunge wa chama tawala na serikali yao walielewe jambo hili kwakuwa wakilipuuza saw a, mkuki mtamu kwa nguruwe; lakini Mungu si athumani, iko siku watakuja kujuta.
 
Alichokifanya ni sawa? Kudanganya kuna zuio la mahakama kubwe sio kweli, mbona anaogopa kivuli chake
Kama kadanganya basi kwa watu wenye akili timamu wangeenda mahakamani kuthibitisha kama hati ni ya kweli au lah ila yawezekana Wabunge wengi hasa wa upinzani yawezekana ni watumia madawa ya kulevya au bangi.
 
Siku watanzania watakapo Badilika utajuta wewe chizi huwezi kujilinganisha na Mbowe wewe
Acha ukilaza hizo ni siasa tu, ila haki lazima iachwe kuwa haki isichezewe unaleta ushabiki hapa?
askari wako wewe una Askari?
 
Siku watanzania watakapo Badilika utajuta wewe chizi huwezi kujilinganisha na Mbowe wewe
Acha ukilaza hizo ni siasa tu, ila haki lazima iachwe kuwa haki isichezewe unaleta ushabiki hapa?
askari wako wewe una Askari?
Mpe za macho huyo, maana anatumia kamasi kuwaza badala ya ubongo
 
Sasa kama Mwenyekiti wetu anaishia kulalamika, sisi mashabiki tutafanyaje? Haya ndo madhara ya chama chetu kuongozwa na mtu ambaye hajapevuka kisiasa. Bora Mwenyekiti awe Lowasa, mzee wa maamuzi mahumu
Mahumu
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Kwa kweli wamechoka,wapumzike tu.
 
Mbowe amekuwa dhaifu mno, kama uongozi wa chama umemshinda aachie damu changa akina Mnyika. Kiongozi wa chama cha upinzani hatakiwi kuwa anakubali kila dhuluma anayofanyiwa na chama tawala na polisisiemu na kuishia kutoa matamko yasiyo na tija.

Itisha maandamano Mbowe, Lijualikali amekataliwa kupiga kura, huku Dar wabunge wanadhalilishwa wewe unaleta matamko yasiyo na tija. Hakuna hata tamko moja limeleta faida. If you cant beat them join them achia chama watu wa kazi
Unaaongea kama umimeza kokoto
 
hivi mtu ukipewlekwa kituoni kwa fujo ulizofanya ni udhalilishaji...

kama hutaki kudhalilika tii sheria ... usipige mtu... wamekimbilia mahakamani na nyinyi kimbilieni hukohuko si mnawanasheria..?
Nyumbu wa lumumba
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA,Freeman Mbowe amesema chama chake kimechoshwa na kukamatwa kwa Wabunge wake kwa hila za kisiasa. Akihojiwa na ITV,Mbowe amesema chama chake kinalaani kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wabunge wake.

Mbowe amesema chama chake kinalaani hila zote na kuitaka Serikali itende haki hasa kwenye uchaguzi wa Meya wa Dar es Salaam. Leo nyumba ya Mbunge wa Kawe Halima Mdee imekaguliwa na polisi wanaosemwa kuwa walikuwa wakisaka nyaraka.

Mbunge Mdee amedai kuwa Mbunge wa Ukonga,Mwita Mwikwabe amekamatwa na polisi. Pia,Mbunge Lijualikali wa Kilombero amekamatwa na polisi.
Yote tisa kumi kanichosha alivyogeuza kibao eti anamshanga MH:MAGUFURI kufukuza watu pasipo kuwapa nafasi ya kujitetea...
 
Kuweni na hekima na kujua kuwa Mbowe anajaribu kuonyesha kuwa wamechoka na maonevu hivyo busara itumike kuepusha mabaya.
Hivi akihamasisha watu wajitokeze kudai haki yao ya waliowachagua itakuwaje? Fikiria watu kama wale waliomsindikiza Lowasa wakiandamana kuna POLICE wa kuzuia hayo? Hata kama watayatawanya jiji litapona kweli? Nafasi hiyo itatumiwa na wezi na majambazi na vifo havitakuwa na idadi.
Tujifunze kuhurumia wengine kwa kukwepesha maafa yasiyo sababu. Hongera Mbowe kwa kuliona hilo, ila kwa vile wamejaa upofu yakitokea wewe hauhusiki
 
Sasa kama Mwenyekiti wetu anaishia kulalamika, sisi mashabiki tutafanyaje? Haya ndo madhara ya chama chetu kuongozwa na mtu ambaye hajapevuka kisiasa. Bora Mwenyekiti awe Lowasa, mzee wa maamuzi mahumu
Sasa kama Mwenyekiti wetu anaishia kulalamika, sisi mashabiki tutafanyaje? Haya ndo madhara ya chama chetu kuongozwa na mtu ambaye hajapevuka kisiasa. Bora Mwenyekiti awe Lowasa, mzee wa maamuzi mahumu

Huna uhusiano wowote na huo ukada wa Chadema wewe ni kamba halisi.
 
Kama kadanganya basi kwa watu wenye akili timamu wangeenda mahakamani kuthibitisha kama hati ni ya kweli au lah ila yawezekana Wabunge wengi hasa wa upinzani yawezekana ni watumia madawa ya kulevya au bangi.
Duh! Makubwa haya. Mbona na wewe unaandika kama unatumia ........................
 
Back
Top Bottom