Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,372
Mwenyekiti Mbowe, kwa yanayoendelea nchi hii na kwa reaction ya wana-CHADEMA kufuatia maamuzi ya Spika kuwalinda Mdee na Wenzake, naiona hatari ya Rais Samia kukugombanisha na viongozi wenzako wa CHADEMA pamoja na wafuasi na mashabiki wa chama hiki.
Hizi ni tweets za Martin Maranja Masese aliyejitoa kuripoti kesi yake ile ya mchongo.
Hizi ni tweets za Martin Maranja Masese aliyejitoa kuripoti kesi yake ile ya mchongo.
By Martin kupitia twitter:
Mwenyekiti, Freeman Mbowe aachane na mpango wa kupeleka ujumbe wa CHADEMA ikulu katika mazungumzo. Ni dhihaka mtu mzima kudharauliwa hadharani. Wao wanapenda picha zetu tukiwa Ikulu na wanazitumia kwa maslahi yao lakini hawaheshimu makubaliano ya pande mbili. Ni watu wabaya.
Mwenyekiti @freemanmbowetz SSH ni kiongozi wa CCM, hawajawahi kuwa na dhamira njema na sisi, hili la leo bungeni kuwakumbatia COVID-19 nadhani linapaswa kuwa taa nyekundu kwako. Tunaweza kuachana sasa na siasa zao za ulaghai mezani kwa kichaka cha maridhiano. Shtuka mwenyekiti!