Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe, ametangaza kuongoza maandamano ya taifa ya amani Jijini Mwanza.
" Kwa mapenzi ya Mungu, nitaongoza maandamano ya Taifa ya Amani Jijini Mwanza, Alhamisi 15 February 2024 Taifa likiwa katika maombolezo ya Hayati Edward Ngoyai Lowassa.
Lowassa aliamini sana katika kazi na alisisitiza salaam za Hongera kwa kazi badala ya pole kwa kazi.
Tunamuenzi kwa kuendeleza maombolezo pamoja na kazi …. aliyoijaribu kwa kuungana nasi 2015, akawa Mgombea wetu wa Urais na akawa mhanga wa wizi wa kura na mifumo isiyo ya haki katika uchaguzi.
Taifa bado linalilia Katiba mpya na mifumo huru na ya haki ya Uchaguzi.
Taifa lina vilio vingi. Watawala wanapaswa kulitambua hili. Ni wajibu wetu kwa pamoja tupaze sauti zetu usiku na mchana hadi wenye mamlaka watambue hali halisi ya hisia za Umma wa Watanzania.
Maumivu yetu makubwa ni umasikini unaotesa maelfu kwa maelfu ya Watanzania kunakosababishwa na kupanda kwa viwango visivyohimilika vya gharama za maisha ikiwemo chakula, pembejeo, nauli, mgao mkubwa usioelezeka wa umeme nk
Watanzania wote tukutane Mwanza tukaandike historia." - Freeman Mbowe
Written by Mjanja M1 ✍️
Chanzo: Mtandao wa X
" Kwa mapenzi ya Mungu, nitaongoza maandamano ya Taifa ya Amani Jijini Mwanza, Alhamisi 15 February 2024 Taifa likiwa katika maombolezo ya Hayati Edward Ngoyai Lowassa.
Lowassa aliamini sana katika kazi na alisisitiza salaam za Hongera kwa kazi badala ya pole kwa kazi.
Tunamuenzi kwa kuendeleza maombolezo pamoja na kazi …. aliyoijaribu kwa kuungana nasi 2015, akawa Mgombea wetu wa Urais na akawa mhanga wa wizi wa kura na mifumo isiyo ya haki katika uchaguzi.
Taifa bado linalilia Katiba mpya na mifumo huru na ya haki ya Uchaguzi.
Taifa lina vilio vingi. Watawala wanapaswa kulitambua hili. Ni wajibu wetu kwa pamoja tupaze sauti zetu usiku na mchana hadi wenye mamlaka watambue hali halisi ya hisia za Umma wa Watanzania.
Maumivu yetu makubwa ni umasikini unaotesa maelfu kwa maelfu ya Watanzania kunakosababishwa na kupanda kwa viwango visivyohimilika vya gharama za maisha ikiwemo chakula, pembejeo, nauli, mgao mkubwa usioelezeka wa umeme nk
Watanzania wote tukutane Mwanza tukaandike historia." - Freeman Mbowe
Written by Mjanja M1 ✍️
Chanzo: Mtandao wa X