Mbowe na Chadema, mmeshindwa na mtashindwa tena!

Mbowe na Chadema, mmeshindwa na mtashindwa tena!

Nimesomaaa, lakini nilichogundua ni kwamba, wewe ni mwanachadema tena mwenye imani kali!

Ulichokikosa ndicho unachokihimiza kirudishwe haraka na chama chako, na ulichokosa ni ile mikikimikiki ya chadema enzi zilee za kina Doct Slaa
Mkuu, sinaga chama mimi, nakuwa mshabiki wa mtu jasiri kama ilivyokuwa kwa JPM, hao ndio napenda kuwashabikia na huwa sijifichi, stakagi watu wanafiki mimi, waoga waoga na wakati mtu umezungukwa na kila kitu,
 
Ni lini mh Mbowe na Chadema wameitisha mandamano ya kwenda kuwang'oa wabunge wake walioko bungeni,ambao anasema hawapo kisheria kwa mjibu wa katiba ya Chama anachokiongoza?

Ni kivipi suala la katiba analishikia bango na kwa sauti kubwa ili hali sauti na nguvu kama hii anayotaka kuitumia hajawahi kuionesha kwa wanaojinufaisha kupitia chama chake?

Tukisema anavuta mpunga kutoka kwa wabunge wasiotambuliwa na chama (Kimagumashi) huku yeye akiwatambua na kufanya jambo hili kuwa la siri siri ili yeye kuendelea kuvuta mpunga ni kosa?

Kama kweli Mh Mbowe na chama chake wamedhamilia kudai katiba mpya tena kwa vitisho na mikutano kila pahala, waanze kwanza kufanya hivyohivyo kwa kuwatoa wabunge wanaoendelea kutumia jina la chama chao ili hali Chama kinadai hakiwatambui

Watanzania, hivi ni kwa nini tusiwapuuze Chadema kwa hadaa hizi,

Kama chama chenyewe kwa chenyewe kinashindwa kufanya mambo yake kwa ukamilifu, inakuwaje watusumbue kuhusu katiba tena ya nchi ambayo inahitaji uadilifu mkubwa katika kuisimamia?

Mbowe na Chadema mmeshindwa kuisimamia katiba na mambo yenu, mtaweza kuisimamia Katiba ya nchi na kuitendea haki?

Sisi wazalendo tunasema! Masilahi kidogo mnayoyapata kwenye kuivunja katiba ndogo ya chama chenu, sasa mnatafuta masilahi makubwa katika Katiba ya nchi, Mtashindwa!

Tunataka katiba, ila ni vyema tuonyeshe uwezo wa kusimamia katiba ndogo za vyama vyetu kwa hali na mali, kwa nguvu na jasho, ndipo tuitafute katiba ya nchi tukiwa na ujasiri mkubwa!
Tunataka katiba tutamuunga mkono yeyote kudai katiba, kumshambulia mbowe na chadema haitasaidia
 
pumbavu! Kamuulize, dungai, Samia na na lile bwege la nec
Taratibu mkuu, matusi ya nini sasa?

Kuandamana na kufanya ukaidi mbele ya amiri jeshi kudai katiba bika kufuata sheria, je ni kosaa au sio kosa?

na kama ndivyo, kwa nini msifanye hivyohivyo kwa wabunge wenu uchwara, Msimtishe Rais, Mfahamu tuliapa kumlinda
 
Back
Top Bottom