Mbowe, mkanye Lissu

Labda iwe ulikuwa unaishi kijijini ila TL ni maarufu sana hata kabla ya JPM.
Tatizo ni historia yake iliyopinda. Alikuwa mtetezi wa wananchi migodini. alipopata unachokiita umaarufu, akawageuka na kuanza kupigia kampeni migodi eti wako sahihi, ooh tutashitakiwa, oooh mikataba ya kimataifa, oooh sheria inawalinda, na uozo mwingi! Umaarufu tukaudhalau!. Kumbuka ujinga pia humfanya mtu akawa maarufu.
 
Watajua wenyewe bhana mbona musiba aliongea mambo ya ajabu sana hakuna aliesema asiongee mimi musiba aongee kipindi hiki na makonda aende clouds tena...
 
Ushauri mzuri!
Tamaduni zetu ni kuheshimu maiti na wafiwa.
Alipaswa kutoa pole na kukaa kimya.
Nilishangaa zaidi alipoendelea kung'ang'ana kwenye vyombo vya nje kuwa corona ndio imemuondoa Magu na kwamba alifariki trh 09.
Sikuona mantiki yake.
Ni kweli aliumizwa lakini inabidi asamehe ama akae kimya.
Bado hajatufahamu watz vizuri?
Tayari ameshaharibu reputation yake.
Siasa inahitaji akili kubwa sana hasa kwa Tanzania.
Yaani Roma mkatoliki kamzidi saikolojia Lissu?
Kwani Lissu ni Mkenya asiwafahamu vizuri Watanzania? Marehemu anapaswa kuorodheshewa maovu yake yote ili liwe somo kwa wanaobaki!
 
Kwani Lissu anawaumiza nini? Muendelee na ratiba zenu, naye muacheni ya post zake!

Naona baba amefariki hasira zinataka kuhamia kwa Lissu.

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
JF iko miaka mingi na mambo ya hovyo huwa yanalaaniwa. Siyo Lissu siyo, Magufuli (RIP), siyo Kikwete, siyo Mbowe. JF haiko hapa kwa ajili ya wanasiasa tu! Ila hatutaki nchi kugeuzwa brothel na mtu asiyejitambua kama Lissu. Yaani ijulikabne eti huyo ndo mtu wa maana upinzani! Foooool!
 
Walaaa aachwe tuu aongee kilichoko moyoni kitulie as long as havunji sheria,nadhan kama ingekua ni wewe umemininiwa risasi zote zile ungeona ni kwa nini nasema aachwe tu aongee
 
Viongozi wa aina ya TL ni wachache sana, wana akili, hawana uwoga na hawana cha kuficha au kuremba maneno. Na huyu bila wizi mwingine wa kura uchaguzi atashinda.
AShinde kwa kura gani? Nawe unaamini aliibiwa? Umeona umati unaomuaga Magufuli? Umati kama huo unahitaji kuambiwa kwamba alishinda kwa haki? Muulize Lisu leo hii alikuja na ajenda gani ktk uchaguzi, hajui! Ila alikuwa majukwaani akitaka kusimulia idadi ya risasi na matusi. Alianzia Nairobi akinadi corona ya Tanzania, ikashindikana. Akaja na kuanza kupiga miayo mitaani bila hata viongozi wa CHADEMA kumpa support. Kajidai yuko hatarini wakati safari ilijulikana kabla ya uchaguzi. Lema kafuata kichwa kichwa, leo anahangika Canada bila elimu. Nyarandu kajiunga na maigizo akazuiliwa mpakani, yuko nyumbani hata hatuoni hatari hiyo iko wapi! They are comedians.
 
Pengine alitegemea Siku marehemu angemuomba msamaha kwa zile risasi alizo vulumishiwa,ana uchungu marehemu kasepa vila kumuombea msamaha
 
Mimi nimeongolea zilizomfika mwlini mwake, jumla 32. Una swali lingine??, Wewe unayeiliza hivi ukiletewa mjusi unajiharishia na kujinyea Bado una swali??
Mjusi naogopa nikimuona lkn siharishi wala sijinyei.

Halafu mbona umenijibu kwa jazba wakati ni kweli nataka kujua.

Maana hii idadi ya risasi alizopigwa Lissu inabadilika badilika mara kadhaa hii issue ikiwa mentioned. So I really wanted to know
 
Eti nini? malaya imekujaje hapa? Sikuzuii kumfuata huyo Lissu na akili yake. Endelea ila ujue huyo ni mbwa kichaa, wewe unafuata mkia wake! Utachoka tu maana huo mkia sijui utatulia lini! Mi nina kichwa changu bhana, tena asiniambie kitu sijui risasi zilipita makalioni, so what? I was a kid and now I am a potential voter. Nilichokiona mbele yangu ni flyover, SGR, umeme, Bodi ya mikopo and the likes!
Wewe ni kati ya wapuuzi nchi hii imejaaliwa kuwa nao. Huwezi kuhalalisha mateso ya wapinzani eti kisa sijui Flyover, Stygler gauge, Ndege na madaraja . Vinakuwa na faida gani kama ndiyo ticket ya mateso.
 
Popote ulipo mwenyekiti wa chama.

Tunakufikishia salamu hizi sisi watanzania tusio na chama na wanachama wa CHADEMA.

Mwambie Tundu Lissu akae kimya wakati huu, aache tabia za kuropoka ropoka na kujibishana asiye jibishane naye.

Mwambie kwenye msiba tamaduni zetu ni kuungana na kua wamoja huo utofauti anaoulazimisha utazidi kumuumbua na kukiumbua chama chenu.

Mwambie atakama anauchungu na kisasi kwa Yale aliyofanyiwa mwambie kwa nafasi yake hastahili kufanya anayoyafanya labda kama hana mpango wakugombea.

Mwambie anaharibu image ya chama, kama anajua hatarudi wala kugombea mwambie anawaponza wenzake. Mbona wewe (Mbowe) hupost post au anadhani huna bando au smartphone?

Mwambie au mumkanye adharani au mumfute uanachama. Tundu Lissu behave like gentalman.
Nani atamzuwia Lissu kuropka? hiyo ni ada yake, iko kwenye damu.
 
True pamoja na maumivu na ubaya aliotendewa Lisu anajiharibia credit na cv yake marehemu asemwi kwa mabaya.
 
Popote ulipo mwenyekiti wa chama.

Tunakufikishia salamu hizi sisi watanzania tusio na chama na wanachama wa CHADEMA.

Mwambie Tundu Lissu akae kimya wakati huu, aache tabia za kuropoka ropoka na kujibishana asiye jibishane naye.

Mwambie kwenye msiba tamaduni zetu ni kuungana na kua wamoja huo utofauti anaoulazimisha utazidi kumuumbua na kukiumbua chama chenu.

Mwambie atakama anauchungu na kisasi kwa Yale aliyofanyiwa mwambie kwa nafasi yake hastahili kufanya anayoyafanya labda kama hana mpango wakugombea.

Mwambie anaharibu image ya chama, kama anajua hatarudi wala kugombea mwambie anawaponza wenzake. Mbona wewe (Mbowe) hupost post au anadhani huna bando au smartphone?

Mwambie au mumkanye adharani au mumfute uanachama. Tundu Lissu behave like gentalman.
Ni nini alichoposti kilichokuvuruga kiasi hiki mkuu!

Hivi hadi sasa bado machungu hayajapungua tu na kukubali aliyofanya Mwenyezi Mungu?

Achana na Lissu, hatakusaidia lolote katika maumivu yako.
 
AShinde kwa kura gani? Nawe unaamini aliibiwa? Umeona umati unaomuaga Magufuli? Umati kama huo unahitaji kuambiwa kwamba alishinda kwa haki? Muulize Lisu leo hii alikuja na ajenda gani ktk uchaguzi, hajui! Ila alikuwa majukwaani akitaka kusimulia idadi ya risasi na matusi. Alianzia Nairobi akinadi corona ya Tanzania, ikashindikana. Akaja na kuanza kupiga miayo mitaani bila hata viongozi wa CHADEMA kumpa support. Kajidai yuko hatarini wakati safari ilijulikana kabla ya uchaguzi. Lema kafuata kichwa kichwa, leo anahangika Canada bila elimu. Nyarandu kajiunga na maigizo akazuiliwa mpakani, yuko nyumbani hata hatuoni hatari hiyo iko wapi! They are comedians.
Kwa sasa angalau ana ushahidi mzuri zaidi, alipowaambia watu corona ni hatari aliambiwa ni wakala wa wazungu, sasa corona imekata mpaka kichwa. Tundu alikuwa na hoja tu tena nzito, zaidi ya mtu kulalamika kwa nini na yeye asipewe miaka mingine mitano kama watangulizi wake, kulikuwa hakuna jipya. Kuhusu wizi wengine hata jukwaani hapa walikuwa wasimamizi wa uchaguzi na wana cha kueleza kuhusu uchaguzi uliopita.
JPM ameagwa na watu wengi kama ilivyo kawaida ya raisi wa nchi, kuna wanaolia (akina Sabaya) kwa sababu mentor wao kafariki, kuna wanaolia kwa kuwa walikula na kunywa chini yake na sasa bado haijulikani itakuwaje. Kuna wanaolia kwa sababu mtu anapofariki hutia uchungu hata kama alikuwa adui wako.
 
Back
Top Bottom