Jack Daniel's
JF-Expert Member
- May 18, 2015
- 1,008
- 840
CHADEMA wanamuongelea mtu ambae hata hajateuliwa na chama chake kugombea, ni dalili ya kumuogopa.
Ungetegemea wapinzani wajikite kutafuta mgombea wao, au kama wa kwao ni wale wale wanajulikana miaka na miaka basi wakae kimya badala ya kufanya siasa zinazochagizwa na kinachoendelea kwenye siasa za ndani za C.C.M.
Kwa sababu kama Lowassa ni dhaifu na bubu kwa nini usikae kimya uombee ateuliwe ili uje umshinde? Hofu imetamalaki upinzania kwamba Lowassa ambae "anaeakisi mambo yanayowachukiza watu" akivuka tufani la upinzani ndani ya chama chake halafu akaja akatumia bendera ya C.C.M. kushinda Urais basi ndio mwisho wa upinzani nchini.
Tumia fikra kabla ya kuandika. Hao CCM mara ngapi wameongelea kuhusu wagombea wa UKAWA na kuwatukana pamoja na mambo mengine? ACT haijawahi kuongelea kuhusu Lowassa kujiunga nao? Uwe na tabia kufuatilia siasa zinazovyoendelea sio unapayuka tu bila kufikiri. Pia ,Mbowe aliulizwa hilo swali ulitaka akae kimya?