Mbowe: Lowassa ni dhaifu, ni bubu

Mbowe: Lowassa ni dhaifu, ni bubu

Status
Not open for further replies.
Chama sio kupanga kwenye liofisi la ghorofa au kuwa na ofisi kubwa, chama ni kuweza kuwajengea wananchi fikra ya kujitambua.Tukianza kuchunguzana matumizi ya ruzuku tutakimbiana humu.
 
Kwa hili Mbowe yupo sahihi
Unasema!!!, Hakika Magamba mbowe mnamkubali kiaina, bado Hamm dada, Simiyu yetu, Ritz chiz, GSU na nyau wengine wanaosuport mafisadi.

CCM mna mafisadi wengi, kuna mafisadi wa Elimu na mafisadi wa kuchuna taifa(Wizi)
 
Hebu tuangalie baraza la mawaziri la Edward Lowassa
  1. Waziri Mkuu Prof Juma Kapuya
  2. Waziri wa Sheria na katiba Andrew Chenge
  3. Waziri Nishati na Madini William Ngereja
  4. Waziri wa Uchukuji Nizar Karamagi
  5. Waziri wa jinsia na watoto Diana Chilolo
  6. Waziri wa Maliasili na Utalii. Mgana Msindai
  7. Waziri wa mambo ya ndani Hamis Mgeja
  8. Waziri wa Ujenzi Peter Serukamba

Hebu tiwe serious Watanzania, kwa baraza hili la mawaziri unategemea nini? Be the Juror Yourself
 
Hebu tuangalie baraza la mawaziri la Edward Lowassa
  1. Waziri Mkuu Prof Juma Kapuya
  2. Waziri wa Sheria na katiba Andrew Chenge
  3. Waziri Nishati na Madini William Ngereja
  4. Waziri wa Uchukuji Nizar Karamagi
  5. Waziri wa jinsia na watoto Diana Chilolo
  6. Waziri wa Maliasili na Utalii. Mgana Msindai
  7. Waziri wa mambo ya ndani Hamis Mgeja
  8. Waziri wa Ujenzi Peter Serukamba

Hebu tiwe serious Watanzania, kwa baraza hili la mawaziri unategemea nini? Be the Juror Yourself
itakuwa mashindano ya kupiga hela
 
....

Tumpe muda labda kuna siku atafunguka na kuweka yote wazi ambapo kila mtu atabaki kushangaa kumbe tumdhaniye ndiye siye.

Unakumbuka juzi jinsi alivyohamaki alipoulizwa urafiki wake na rais ukoje...!? Unadhani kwa nini alihamaki?
 
Hebu tuangalie baraza la mawaziri la Edward Lowassa
  1. Waziri Mkuu Prof Juma Kapuya
  2. Waziri wa Sheria na katiba Andrew Chenge
  3. Waziri Nishati na Madini William Ngereja
  4. Waziri wa Uchukuji Nizar Karamagi
  5. Waziri wa jinsia na watoto Diana Chilolo
  6. Waziri wa Maliasili na Utalii. Mgana Msindai
  7. Waziri wa mambo ya ndani Hamis Mgeja
  8. Waziri wa Ujenzi Peter Serukamba

Hebu tiwe serious Watanzania, kwa baraza hili la mawaziri unategemea nini? Be the Juror Yourself

Singh Sett mshauri uchumi na uwekezaji.EL bado nasaka utajiri Raia Mwema
 
Naskitshwa sana na wanao mpigia debe Lowasa nchi itaharibika kabisa, Kuna mifano ya nchi maskini duniani kama Haiti TZ itakuwa zaidi. Mwizi muongo wawazi mwemye jaziba kisasi, amejenga genge. Anataka kuwa Rais kwa lazima alijua tangu mwanzo ubaya uliokuwemo kwenye richmund alinufaika. Kwa nini hakujiuzuru mapema. Na alipo jiuzuru alifanya kitendo hicho kunusuru serikali ya majizi akiwemo yeye.
 
Wakati wa sakata la escrow angeweza kumsema swahiba wake na pacha mwenzake nyoka wa makengeza kweli?

Wakati anajua alikuwa akihemea kwenye fuko lao la kuhonga

Si ajabu chenge akaja kuwa PM baada ya EL kupata uprezida
na rostam waziri wa fedha
 
kwani yeye Lowasa alipomtaja Mbowe juzi kwenye press conference inamaana anamuogopa? Tumia ubongo unapotoa post.
Kwa hiyo anachofanya Lowassa lazima kiigwe na upinzani?

Tumia fikra kabla ya kuandika. Hao CCM mara ngapi wameongelea kuhusu wagombea wa UKAWA
Na hiyo hiyo ndio hoja yangu, wapinzani wanajikita kuwaigiza, kuwajibu, na kufanya yale yanayochagizwa na yanayotokea ndani ya C.C.M.

Mtapangaje agenda za kitaifa za upinzani kwa kujibu anachosema Nape, hamna lenu jipya?

Pia ,Mbowe aliulizwa hilo swali ulitaka akae kimya?
Unapota kauli kwa umma huwezi kuchemka halafu ukasema "niliulizwa, ulitaka nisijibu." Kwa hiyo Rais Mbowe ama Rais Slaa akiulizwa na mwanahabari, Tanzania ina silaha za aina gani za kujihami na inazinunua wapi, atajibu halafu aseme niliulizwa ulitaka nisijibu? Hebu jifunze misingi ya public speech, usitetee jambo kinazinazi tu.

Kama Lowassa ni dhaifu na ni bubu, kwa nini mnawashtua C.C.M, kwa nini msinyamaze kimya mumsubiri kwenye uchaguzi mumshinde? Kama sio kumuogopa?
 
Mbowe anakosea sana..muda huu ni wa kuimarisha chama chake na mgombea wao wa UKAWA sio muda wa kuanza kukosoa wengine..itafika october hapa ataanza kusema wameibiwa kura
 
Mbowe hana tofauti na vijana wa kitaa wanapokua wanamfukuzia demu mkali mtaani kwao,,,yahan kila mmoja kwa wakati wake ujitaidi kumpaka mpinzani wake kadiri awezavyo..
 
Mh.Mbowe amenukuliwa na Tanzania Daima akimchana Mh.Lowasa kuwa ni mgombea dhaifu na bubu wa kukemea ufisadi.

Amesema UKAWA hawawezi kuwa nae,hivyo asiwatishe CCM kuwa ana nafasi UKAWA.

Source:Tanzania Daima page no.5

Photo Fullname Party Name By this Mp
Lowassa Ngoyai Edward Chama Cha Mapinduzi
Questions(0)
Supplementary Questions (0)
Contributions(5)

Mchango wake ndani ya Bunge kwa kipindi cha miaka mitano.
 
Daaah, hivi ni Nani humu aliyemsafi na anahisi hawezi kuwa fisadi,

Rushwa ni Kama tabia yetu watanzania, na haitaisha kwa kuwa mtoaji na mpokeaji wapo, siku mmoja wao akikataa basi Tanzania itapona.
 
Wakuu mimi nina mawazo tofauti kidogo,

Inawezekana kabisa Lowassa wa sasa ni tofauti na wa miaka ileee na inawezekana pia na yeye leo ufisadi unamkera kama unavyokukera wewe na ameshagundua kuwa ndio utakaomfanya akose urais lakini anashindwa aanzeje kuukemea.

Tumpe muda labda kuna siku atafunguka na kuweka yote wazi ambapo kila mtu atabaki kushangaa kumbe tumdhaniye ndiye siye.

Aisee wewe una shida sana uumpe muda tena?lowasa ni fisadi na kwa upuuzi wa watz watampa uraisi hapo hata dunia itatushangaa alafu tunakazana kulalamika maisha magumu wakati nasisi ni chanzo cha haya maisha magumu sioni mtu msafi ccm wote ni wala rushwa wameifanya nchi ni km yao wao tu hii inaudhi sana watanzania tunadilike jamani
 
Pumba tupu.
Huna uwezo wa kujieleza una neno moja tu, pumba!

Eti Lowassa kafanya kwa hiyo upinzani nao ufanye, mnamuiga Lowassa? Don't be ridiculous, ndio matatizo ya kupenda kitu ama chama kinazi nazi tu, unakosa uwezo wa kufikiri.
 
Huna uwezo wa kujieleza una neno moja tu, pumba!

Eti Lowassa kafanya kwa hiyo upinzani nao ufanye, mnamuiga Lowassa? Don't be ridiculous, ndio matatizo ya kupenda kitu ama chama kinazi nazi tu, unakosa uwezo wa kufikiri.

Ukimuona mtu anamuunga mkono Lowasa ujuwe kuna mambo mawili 1. Anategemea kunufaika na uongozi wa Fisadi Lowasa yeye binafsi . (2) kundi lapili ambao ndio wengi ukiwa wewe ni mmoja wao ni bendera fuata upepo yani watu wajinga wasiojielewa basi tu kwa ushabiki wa kipumbavu.
 
ukiwa kiongozi ndio utajua ukawa ni wazush xana. bora lowasa

xana ndio nini? Ndio maana nasema nyie vijana hamjielewi zaidi ya ushabiki wa kijinga.yani ni bendera fuata upepo ukiulizwa unachompendea Lowasa ninini hujuwi.any way we dogo hata kura unaweza usipige ngoja nikuache uendelee kukomaa kiakili.
 
Ukimuona mtu anamuunga mkono Lowasa ujuwe kuna mambo mawili 1. Anategemea kunufaika na uongozi wa Fisadi Lowasa yeye binafsi . (2) kundi lapili ambao ndio wengi ukiwa wewe ni mmoja wao ni bendera fuata upepo yani watu wajinga wasiojielewa basi tu kwa ushabiki wa kipumbavu.
Sijamuunga mkono Lowassa, in fact nimesema "anaakisi mambo yanayowachukiza watu..."

Hoja yangu ni rahisi sana, inashangaza kwa CHADEMA kuanza kuongelea siasa za ndani za C.C.M. kuhusiana na kada mmoja wa C.C.M. ambae hata bado hajapewa tiketi ya kuwa mgombea wa C.C.M. CHADEMA hawana agenda inayojitegemea au hawana la kufanya zaidi ya ku respond kwa anachofanya na kusema Lowassa? Kama Lowassa ni dhaifu mngekaa kimya aje mumshinde, ni dalili dhahiri za kumuogopa!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom