Kama kawaida ya watanzania kila kunapotokea jambo nilalotulazimu kujikumbusha wosia wa mpenwa wetu Nyerere hatuna budi kujikumbusha baadhi ya maneno yake ya busara kwa sababu ni kiongozi wa kitaifa anayeheshimika hapa Tanzania.
Pia kwa sasa hatuna budi kujikumbusha wosia wa Ndugu Mbowe kwa watanzania ili kuchagua kiongozi mzuri kwa maana ya utendaji, maadili na mwadilifu
Quotes;
"Wanajidanganya, Lowassa ni dhaifu sana. Amekaa serikalini zaidi ya miaka 30 na hakuna maendeleo yanayoonekana ndani ya serikali zaidi ya kila siku wizi na ubadhirifu kuongezeka," Freeman Mbowe.
"Hao wanaomtaka Lowassa ni wale wanaojua kuwa watanufaika binafsi akipita kwenye urais lakini kimsingi huyu jamaa ni dhaifu sana na hafai kuongoza Tanzania ya sasa yenye changamoto lukuki. Wapambe wake wanasema si msemaji bali mtendaji, hivi nani atakubali porojo hizo wakati tunajua akiwa Waziri Mkuu hakufanya lolote kukemea wizi, ubadhirifu na ufisadi? Richmond ilikuja akiwa wapi?," Mbowe.
"Sina ugomvi wala simchukii Lowassa binafsi, lakini ni vema hawa wanaosema ni mtu wa maamuzi magumu wakaueleza umma wakati watendaji wa serikali wakitafuna mabilioni ya fedha, CCM wakipitisha Katiba inayopendekezwa ya hovyo pale Dodoma wakitetea kwa wizi...yeye alisema au kufanya nini?," Mbowe.
"Huyu mtu yumo ndani ya mfumo wa ufisadi ulioiharibu nchi kwa takriban miaka 50 halafu mnataka kutuaminisha ni mchapakazi, tuwe serious jamani, nchi inahitaji mabadiliko ambayo yanapatikana UKAWA," Mbowe.
"Msipate shida, UKAWA ni kiboko ya Lowassa na CCM yake, ikifika Oktoba wananchi watuchague tuwakwamue kutoka hapa tulipo, haiwezekani miaka 50 sisi tungali maskini wa kutupwa ilhali tuna rasilimali lukuki," Mbowe.
"Sasa tutapambana na CCM jino kwa jino mpaka kieleweke, wao walikuwa wakishinda kirahisi kwa sababu walikuwa na wenyeviti wa vijiji, lakini sasa wataonja nguvu yetu,"