macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 21,804
- 39,619
Mkuu unajua kuna watu wengi tu ambao kula yao inategemea migogoro kama hii. Wanajua bila Rais Samia kufanya mapambano na Upinzani ili wao wajifanye kuwa upande wake hence awalipa ujira, maisha kwao yatakuwa magumu. Ndiyo kina Slaa hao na wengine wengi tu wako CCM.Mh. Mbowe yuko huru kama ilivyosemwa kwenye hukumu, "bila ya masharti yoyote."
Iwe ni kwa uamuzi huru wa mahakama au kuna mkono wa mama ndani yake, pana watu wamechanganyikiwa wasijue kulikoni.
"Kwamba, ni mwiba mchungu mno kwa wasiotutakia mema kama nchi."
Wasikie sasa wale manguli wa kile chama waliokuwa kutwa kujiapiza kuwa Mbowe ni gaidi:
View attachment 2139895
Sasa imekuwa:
"Mbowe CCM B. Mbowe System. Mbowe kasaliti Chadema. Mbowe hana tofauti na Zitto. Mbowe mwuungwana kuliko Lissu. Alichofanya Mbowe na Lissu ni sawa na alichofanya Zitto au Sheikh Zuberi, nk nk."
Kwamba kila mmoja na lake, ila kimsingi ni full kuchanganyikiwa. Nani hakujua hii nchi ilihitaji maridhiano? Maridhiano yanapatikana vipi bila mazungumzo?
Misahafu inasema si kila aitaye "bwana, bwana .. kuwa atauona ufalme wa mbinguni."
Mama na awajue sasa wamlao nguoni mwake.
Kwamba mama Samia hatimaye kaongea ana kwa ana na Mh. Mbowe na pia Tundu Lissu, yumkini kama hakuwahi kuhusika atakuwa sasa kaipata tafsiri halisi ya picha hii:
View attachment 2139885
Kwamba pana watu hawaitakii mema nchi hii. Kwamba baadhi yao hata wanajua waliko Moses Lijenje, Ben Sanane, Azory au nani waliokuwa kwenye viroba?
Yetu sasa macho.
Kwamba sasa tunajua anajua. Kutokea hapa mikutano ya siasa inakwenda je, vipi kuhusu katiba mpya, vipi kuhusu uwajibikaji, na yote ya namna hiyo?
Ni muda muafaka kwake wa kujitenga na hayo ya nyuma.
Yumkini inafahamika vyema sasa - "kikulacho ki nguoni mwako."