Mbowe kuachiliwa, pigo kubwa kwa wasiotutakia Mema kama Nchi

Mh. Mbowe yuko huru kama ilivyosemwa kwenye hukumu, "bila ya masharti yoyote."

Iwe ni kwa uamuzi huru wa mahakama au kuna mkono wa mama ndani yake, pana watu wamechanganyikiwa wasijue kulikoni.

"Kwamba, ni mwiba mchungu mno kwa wasiotutakia mema kama nchi."

Wasikie sasa wale manguli wa kile chama waliokuwa kutwa kujiapiza kuwa Mbowe ni gaidi:

View attachment 2139895

Sasa imekuwa:

"Mbowe CCM B. Mbowe System. Mbowe kasaliti Chadema. Mbowe hana tofauti na Zitto. Mbowe mwuungwana kuliko Lissu. Alichofanya Mbowe na Lissu ni sawa na alichofanya Zitto au Sheikh Zuberi, nk nk."

Kwamba kila mmoja na lake, ila kimsingi ni full kuchanganyikiwa. Nani hakujua hii nchi ilihitaji maridhiano? Maridhiano yanapatikana vipi bila mazungumzo?

Misahafu inasema si kila aitaye "bwana, bwana .. kuwa atauona ufalme wa mbinguni."

Mama na awajue sasa wamlao nguoni mwake.

Kwamba mama Samia hatimaye kaongea ana kwa ana na Mh. Mbowe na pia Tundu Lissu, yumkini kama hakuwahi kuhusika atakuwa sasa kaipata tafsiri halisi ya picha hii:

View attachment 2139885

Kwamba pana watu hawaitakii mema nchi hii. Kwamba baadhi yao hata wanajua waliko Moses Lijenje, Ben Sanane, Azory au nani waliokuwa kwenye viroba?

Yetu sasa macho.

Kwamba sasa tunajua anajua. Kutokea hapa mikutano ya siasa inakwenda je, vipi kuhusu katiba mpya, vipi kuhusu uwajibikaji, na yote ya namna hiyo?

Ni muda muafaka kwake wa kujitenga na hayo ya nyuma.

Yumkini inafahamika vyema sasa - "kikulacho ki nguoni mwako."
Mkuu unajua kuna watu wengi tu ambao kula yao inategemea migogoro kama hii. Wanajua bila Rais Samia kufanya mapambano na Upinzani ili wao wajifanye kuwa upande wake hence awalipa ujira, maisha kwao yatakuwa magumu. Ndiyo kina Slaa hao na wengine wengi tu wako CCM.
 
Mkuu unajua kuna watu wengi tu ambao kula yao inategemea migogoro kama hii. Wanajua bila Rais Samia kufanya mapambano na Upinzani ili wao wajifanye kuwa upande wake hence awalipa ujira, maisha kwao yatakuwa magumu. Ndiyo kina Slaa hao na wengine wengi tu wako CCM.

Unasomeka vyema mkuu.

Ndiyo wanyoa viduku na watupia jezi za timu ya wananchi hao:

IMG_20220305_151655_415.jpg


Kwamba mama kaongea na Lissu na Mbowe. Wote hao ana kwa ana na one to one?

Hamna shaka ndiyo sababu ya nyuso ndefu hizi:

IMG_20220306_053509_333.jpg


Matumaini yetu kwa mama Tanzania mpya yenye maridhiano ya kweli ndicho iliyokuwa kilio cha wengi iko njiani.

Tunaamini kuwa hatimaye baada ya maumivu sana, tunarudi kwenye njia iliyo sahihi.
 
Mkuu unajua kuna watu wengi tu ambao kula yao inategemea migogoro kama hii. Wanajua bila Rais Samia kufanya mapambano na Upinzani ili wao wajifanye kuwa upande wake hence awalipa ujira, maisha kwao yatakuwa magumu. Ndiyo kina Slaa hao na wengine wengi tu wako CCM.
Wakwanza anaweza kuw ani Mtungi na maDED
 
Unasomeka vyema mkuu.

Ndiyo wanyoa viduku na watupia jezi za timu ya wananchi hao:

View attachment 2140701

Kwamba mama kaongea na Lissu na Mbowe. Wote hao ana kwa ana na one to one?

Hamna shaka ndiyo sababu ya nyuso ndefu hizi:

View attachment 2140703

Matumaini yetu kwa mama Tanzania mpya yenye maridhiano ya kweli ndicho iliyokuwa kilio cha wengi iko njiani.

Tunaamini kuwa hatimaye baada ya maumivu sana, tunarudi kwenye njia iliyo sahihi.
Mimi nazicheki hizo nyuso tu.
 
Kuna watu wakiona wapinzani wanafurahi hivi wakiwa kwenye jengo ambalo nao wanalihudumia kupitia kodi zao nya inagonga pichu, Bwana yule nadhani alipandikizwa na maadui ili kuvuruga amani ya nchi, mambo aliyokuwa anafanya siyo ya kitanzania kabisa, hivi vifuasi vyake uchwara vimebaki kutapatapa tu kwa ID fake....Ni heri njama zake zilitambulika mapema before hajaharibu zaidi.....

1646552545402.jpeg
 
Sidhani kama kuna mwana CDM anataka haya:

"Siasa za kununiana, kuwindana, kufungwa kwa uongo."

Labda kama ni mamluki.

CDM iliandika barua kuomba mazungumzo. Imekuwa ikiomba maridhiano. Kikwazo cha yote nani asiyekijua?

View attachment 2140604

Wasiotaka mazungumzo, wenye kupinga mama kufanya mazungumzo na CDM na wasiotaka maridhiano - wamenyoa viduku na wamevalia kama timu ya wananchi.

Zaidi sana vibaraka wao wako hapa:

View attachment 2140612
Haya mambo wakati mwingine nikiangalia chanzo chake ni propaganda nyepesi za lumumba tu zinawayumbisha wasiojiamini.

Maneno kama Mbowe amesalimu amri, amenunuliwa, ni afisa wa TISS, na mengine ni vitu vya kuchekesha sana.

Kila mtu anafahamu msimamo wa Mbowe akiwa gerezani mpaka alipotoka, nani waliomtoa na walimtoa akiwa na msimamo upi, sasa pressure ya kuogopa mazungumzo inatoka wapi?

Oooh Mbowe ni TISS, sasa kama angekuwa mwenzao wangehangaika kumfunga kila wakati si wangempa maelezo tu afanye nini? na kwa kizazi hiki sio rahisi kuwadanganya wengi kwa wakati mmoja, atashtukiwa tu.

Mazungumzo muhimu yawepo, kuanzia hapo ndio ramani nyingine ianze kuchorwa, hapo ndipo mwanasiasa atakuwa na "guts" za kwenda kwa wananchi awaambie kwa upande wangu nilifanya moja, mbili, tatu, hawakujibu; sio kususa, unasusa halafu wananchi wakikuuliza ulifanya nini utawajibu kitu gani?

Kususa ni siasa za kioga, za wasiojiamini na waviziaji, wanaotaka kutumia kila jambo kwa manufaa yao binafsi badala ya manufaa ya watanzania kwa ujumla wao.
 
Kuna watu wakiona wapinzani wanafurahi hivi wakiwa kwenye jengo ambalo nao wanalihudumia kupitia kodi zao nya inagonga pichu, Bwana yule nadhani alipandikizwa na maadui ili kuvuruga amani ya nchi, mambo aliyokuwa anafanya siyo ya kitanzania kabisa, hivi vifuasi vyake uchwara vimebaki kutapatapa tu kwa ID fake....Ni heri njama zake zilitambulika mapema before hajaharibu zaidi.....

View attachment 2140712
Mshindi kabeba na kikombe Cha dhahabu Nini nakiona meza iliyo kushoto kwake⛹️
 
Kuna watu wakiona wapinzani wanafurahi hivi wakiwa kwenye jengo ambalo nao wanalihudumia kupitia kodi zao nya inagonga pichu, Bwana yule nadhani alipandikizwa na maadui ili kuvuruga amani ya nchi, mambo aliyokuwa anafanya siyo ya kitanzania kabisa, hivi vifuasi vyake uchwara vimebaki kutapatapa tu kwa ID fake....Ni heri njama zake zilitambulika mapema before hajaharibu zaidi.....

View attachment 2140712

Umeanza vizuri lakini kama kawaida ya ile mimburumundu mingine, na kama ilivyo kuwa ada, mwishoni nnya ikaanza kugonga pichu.

Yale yale, ukitapatapa na ki fake ID chako:

"Mbowe CCM B. Mbowe System. Mbowe kasaliti Chadema. Mbowe hana tofauti na Zitto. Mbowe mwuungwana kuliko Lissu. Alichofanya Mbowe na Lissu ni sawa na alichofanya Zitto au Sheikh Zuberi, nk nk."


Kisa na mkasa? Haiwangii akilini kulikoni mwamba yuko huru.

IMG_20220305_151655_415.jpg


Yumkini wewe ni mmoja wa wenye viduku hao au umetupia jezi rangi ya timu ya wananchi hapo juu au ni rasmi kwenye timu hii hapa chini:

IMG_20220306_053509_333.jpg


Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Kuna watu wakiona wapinzani wanafurahi hivi wakiwa kwenye jengo ambalo nao wanalihudumia kupitia kodi zao nya inagonga pichu, Bwana yule nadhani alipandikizwa na maadui ili kuvuruga amani ya nchi, mambo aliyokuwa anafanya siyo ya kitanzania kabisa, hivi vifuasi vyake uchwara vimebaki kutapatapa tu kwa ID fake....Ni heri njama zake zilitambulika mapema before hajaharibu zaidi.....

View attachment 2140712
Enenda mkandamizaji, bingwa wa chuki na visasi

1646553916964.png
 
Ila Samia anajua kuwapoteza aiseee
Mama Samia kategua kitendawili chake alichotupa toka mwanzo,na wote tulishindwa kumuelewa!! "Kuna Kijungu chapwaga bila ya Moto Jikoni" naona sasa hicho Kijungu hakitapwaga tena!!
 
Hayo katamka wazi wazi mbele ya camera mkuu
Basi inawezekana anaipenda Bado chadema, ila Kwa alichokifanya anakuwa mnyonge, atawezaje kurudi akaaminika na kukubalika Tena, naomba Wana jf kwa umoja wetu na kwa wote tunaopenda na kuamini katika haki, uhuru was maoni na mshikamano wa kitaifa tumuombe popote alipo aungane nasi kwenye kampeni ya join the chain , kwa kutoa mchango wake ili maisha yaendelee huku tukiyafikia malengo yaliyo mema.
 
Basi inawezekana anaipenda Bado chadema, ila Kwa alichokifanya anakuwa mnyonge, atawezaje kurudi akaaminika na kukubalika Tena, naomba Wana jf kwa umoja wetu na kwa wote tunaopenda na kuamini katika haki, uhuru was maoni na mshikamano wa kitaifa tumuombe popote alipo aungane nasi kwenye kampeni ya join the chain , kwa kutoa mchango wake ili maisha yaendelee huku tukiyafikia malengo yaliyo mema.

Mkuu tulipo tunasubiri matamko muhimu:

1. Lissu anaingizana lini JKNIA?
2. Katiba mpya tunatoka vipi?
3. Lini rasmi mazungumzo CDM na mama?

Slaa kama Waitata na Mashinji hao hatudaiani.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Mh. Mbowe yuko huru kama ilivyosemwa kwenye hukumu, "bila ya masharti yoyote."

Iwe ni kwa uamuzi huru wa mahakama au kuna mkono wa mama ndani yake, pana watu wamechanganyikiwa wasijue kulikoni.

"Kwamba, ni mwiba mchungu mno kwa wasiotutakia mema kama nchi."

Wasikie sasa wale manguli wa kile chama waliokuwa kutwa kujiapiza kuwa Mbowe ni gaidi:

View attachment 2139895

Sasa imekuwa:

"Mbowe CCM B. Mbowe System. Mbowe kasaliti Chadema. Mbowe hana tofauti na Zitto. Mbowe mwuungwana kuliko Lissu. Alichofanya Mbowe na Lissu ni sawa na alichofanya Zitto au Sheikh Zuberi, nk nk."

Kwamba kila mmoja na lake, ila kimsingi ni full kuchanganyikiwa. Nani hakujua hii nchi ilihitaji maridhiano? Maridhiano yanapatikana vipi bila mazungumzo?

Misahafu inasema si kila aitaye "bwana, bwana .. kuwa atauona ufalme wa mbinguni."

Mama na awajue sasa wamlao nguoni mwake.

Kwamba mama Samia hatimaye kaongea ana kwa ana na Mh. Mbowe na pia Tundu Lissu, yumkini kama hakuwahi kuhusika atakuwa sasa kaipata tafsiri halisi ya picha hii:

View attachment 2139885

Kwamba pana watu hawaitakii mema nchi hii. Kwamba baadhi yao hata wanajua waliko Moses Lijenje, Ben Sanane, Azory au nani waliokuwa kwenye viroba?

Yetu sasa macho.

Kwamba sasa tunajua anajua. Kutokea hapa mikutano ya siasa inakwenda je, vipi kuhusu katiba mpya, vipi kuhusu uwajibikaji, na yote ya namna hiyo?

Ni muda muafaka kwake wa kujitenga na hayo ya nyuma.

Yumkini inafahamika vyema sasa - "kikulacho ki nguoni mwako."
Amini usitake kuhakikisha shetani ana nguvu kuliko unavyodhania au kufikilia Kuna watu wanateseka kuona Rais wa sasa anaijenga nchi kwa upendo mkubwa, kujali utu na kusikiliza wapinzani wake kisiasa wanasemaje? Hakika Mwenyezi Mungu ambariki Mama kwa mpa afya njema daima. kazi iendelee.
 
Back
Top Bottom