Mbowe katika picha Bukoba

Mbowe katika picha Bukoba

Wakuu,
Leo na sasa hivi mzee wa anga na mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe yupo Mjini Bukoba akiendesha operation ya kufungua matawi na kufunga bendera katika maeneo ambayo awali wenye kumiliki maeneo hayo walikuwa wana CUF.

Hadi sasa hivi nipo hapa kwenye cafe na nje pamefurika watu wakishuhudia Mbowe akivunja vijiwe vyote vya CUF na kusimika CHADEMA.

Anaongozana na mwanachma wake mpya Lwakatare.

Lakini kikubwa ninachokina hapa ni kuwa kuna maandamano pia ya wana CCM eti wanapokea Beno Malisa, yani hapa ni SIASA kwa mtindo mmoja jamani waombee wana Bukoba

Chao
 
That is politics at work, mwisho wa siku kodi ya meza kwa mama Chanja lazima iwekwe.
 
eleza undani kama kweli upo hapo mbona unadonyoa na wanajamvini hadi huku majuu tunanataka khabari kama hizi jamani; go detail a bit pls
 
Kuzika CUF?? haya ndio matunda ya kuwa na vyama zaidi ya 20 na mimi nilishasema kuwa utafika wakati vyama hivi nitakufa natural death
 
Mbowe endelea kufungua matawi Mzee kuandaa viwanja vya 2010.Pia fuatilia kichwa kingine Hamad Rashid kutoka CUF(CCMb) ili kuimarisha timu yetu ya kuinyoa CCM 2010.
 
Wakuu leo mchana Mh. Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA, akiwa njiani kuelekea Biharamulo amefanya ziara ambayo haikutangazwa ili kufungua matawi mapya ya chadema hapa mjini Bukoba na kutoa kadi kwa wanachama wapya.

Amepita maeneo mengi kwa miguu akifanya zoezi hilo la kufungua matawi, akigawa kadi mpya za wanachama na kutoa hotuba ndogo kila mahali huku akikuta umati mkubwa wa watu ukimfuata.

Baada ya hapo ameondoka kuelekea Biharamulo kwa ajili ya kuungana na wana Dr Slaa ambao tayari wako katika kampeni ya uchaguzi wa jimbo la Biharamulo.

IMG_0989 i.jpg
Wananchi wakimsikiliza Mbowe

IMG_0993 i.jpg
Wananchi wakimfuata Mbowe katika safari za kwenda kufungua
matawi.

IMG_0995 i.jpg
Akipandisha Bendera ya Chadema kwenye tawi jipya

IMG_0996 i.jpg
Hapa akipandisha bendera ya Chadema huku akishusha bendera ya chama kingine......😀😡🙁

IMG_0999 i.jpg
Akitoa kadi kwa mwanachama mpya wa chadema

IMG_1000 i.jpg
Akitoa kadi kwa mwanachama mpya wa chadema

IMG_1003 i.jpg
Mbowe akihutubia katika moja ya hafla za kufungua matawi

IMG_1005 i.jpg
Mbowe akihutubia katika moja ya hafla za kufungua matawi
 
Mimi sina cha kusema tunashukuru kwa mchango huu na pia umefika watu makini sana kuongoza na kuunga mkono mapambano haya
 
Hakuna kulala mpka kimeeleweka, maana kama ukifungua matatu itakuwa vizuri sana kuungana na watu wengine nao makini sana
 
Kumbukeni methali isemayo'ukubwa wa pua si wingi wa kutoa makamasi'.
 
Sasa jamani hii news inakuwaje 'breaking news'?

Na kama anafungua matawi ya chadema, sawa lakini anajua kuwa Biharamulo wamejiandikisha wapiga kura wangapi na ni wangapi actually watakipigia kura chama chake ili kupata ushindi?

kwa maoni yangu ushindi wa Biharamulo ungewaboost kweli wana Chadema, lakini kama wataishia tu 'kuizika CUF' bila kuwa na mikakati ya ushindi, walau kwa jimbo hilo, basi wasitegemee maajabu 2010.
 
Nashangaa kwa karne hii duuu...??

Ama kweli mwenye shibe hamjui mwenye njaa!

Bravo Mbowe bigup! Endelea kuamsha walio lala, nani ajuaye? huenda wewe ndiye mkombozi mpya wa kututoa katika makucha ya mkoloni mweusi CCM!

Ama kweli tumechoka kukaa kifungoni tunataka kuwa huru sasa. Yatosha!
 
NOOOOOOOO, CCM wanaandamana kumpokea Beno Malisa???????????????
for what??????
 
Hata Sisi Wana JF tuanzishe harakati za ukombozi wa kweli katika Taifa
 
na mwaka lwakatare akihama chadema .......vijiwe vitabadilishwa kuelekea chama atakacho kwenda.

lwakatare hakupigia debe chama, hujipigia mwenyewe tu.........bora kuruhusiwe mgombea binafsi tujue moja
vyama vya siasa tanzania bado vina safari ndefu.
 
Hii inanikumbusha jambo!
Nani aliangalia kipindi maalum cha ITV jana usiku jinsi watu wanavyofukuzwa kwenye vijiji? Yaani vijiji vinafutwa just like that, kupisha ardhi itumiwe na wawekezaji. Nilidhani kipindi kitakuwa kifupi kama ilivyo kawaida, ila nilishangaa wanatueleza yanayotokea Moro, inafuata Mtwara, mara huku.... Duh!

Kama Kikwete alikuwa anaangalia hicho kipindi nadhani alifunga TV.
It is my hope that ITV would put these important footage on the Internet soon.
 
BRAVO CHADEMA; Mkakati wa ndege upo? maana muda umeisha na tunataka mapambazuko zaidi; hongera kuwafikia wanakijiji zaidi
 
Ndio kuna kesi mahakamani na sio kwa hali jinsi ilivyo serikali itabidi kushinda mpaka uchaguzi mwakani tena
 
Kazi kweli kweli mods ziwekeni picha hizi ziwe kubwa wakuu tufaidi zaidi.
 
Back
Top Bottom