Swali la muhimu ni nani yupo nyuma ya kutaka kusababisha vurugu?
Hivi Magufuli aliposema tuache siasa tulimuelewaje?
Kwa nini kauli ya Rais iliyokuwa inatengeneza harmony kwa wanasiasa ilipotoshwa kwa makusudi?
Hivi ni kweli kuna mtu anataka tuendelee na siasa za kiuanaharakati au kama vile tuko kwenye kampeni badala ya kujenga nchi?
Ukawa imeshikilia majiji muhimu
..hii ikiwa ni step muhimu kuelekea Ikulu kwa nini wasijikite kwenye maendeleo makubwa katika hayo majiji ili tuone utofauti wao na CCM?
Magufuli aliachana na siasa kwa kukubali uchaguzi wa meya ufanyike Dar na atakayepata apate kwa nini UKAWA hawaliheshimu hili?
Magufuli amesisitiza kuwa tuache siasa tufanye kazi na ifukapo 2020 watanzania watuhukumu kwa haki.
Ukawa ilikuwa inalia na ufisadi na leo hii Magufuli anapambana nao ...kwa nini ukawa wanakuwa ni obstacle?
Kuna hoja nyeti sana za kuibana serikali ya Magufuli mfano Kwenye Afya elimu ajira n.k kwa nini sisikiii uhamasishaji wa maandamano kuhusu haya maswala ya kitaifa??
Ni nani huyu anayejaribu kuwapoteza vijana na kuwaondoa kwenye mstari wa fikra na badala yake anawaimbisha nyimbo mbaya kama kasuku??