Mbowe awazuia BAVICHA kwenda Dodoma

Mbowe awazuia BAVICHA kwenda Dodoma

Nilikua na hamu nione mechi ya State Army vs BAVICHA
 
Advanced Modern Mathematics:

Wrong + Wrong = Right

6d7a2662a447a177b76bf780e54cc928.jpg
 
Kama Serikali hii ya Magufuli haitapata somo kwa kilichotokea kwa Kikwete itaishi kwa taabu sana. Kikwete alijaribu kuwa weka hawa karibu, wakilalamika kidogo kawaita ikulu. Wakapiga kelele kuhusu ufisadi, jina likakatwa ilikuliponya taifa kuangukia kwa kiongozi wa aina hiyo. Kilichotokea sasa ni historia.

Wale huko nyuma walioandika katiba ya nchi hii kwa busara zao kuona kumfanya Rais kuwa na nguvu zilizo pitiliza, pengine walijua hulka ya watu wa nchi hii. Sasa mpira uko kwa JPM ni jukumu lake kuamua anavyo ucheza.


Swali la muhimu ni nani yupo nyuma ya kutaka kusababisha vurugu?

Hivi Magufuli aliposema tuache siasa tulimuelewaje?

Kwa nini kauli ya Rais iliyokuwa inatengeneza harmony kwa wanasiasa ilipotoshwa kwa makusudi?

Hivi ni kweli kuna mtu anataka tuendelee na siasa za kiuanaharakati au kama vile tuko kwenye kampeni badala ya kujenga nchi?

Ukawa imeshikilia majiji muhimu
..hii ikiwa ni step muhimu kuelekea Ikulu kwa nini wasijikite kwenye maendeleo makubwa katika hayo majiji ili tuone utofauti wao na CCM?

Magufuli aliachana na siasa kwa kukubali uchaguzi wa meya ufanyike Dar na atakayepata apate kwa nini UKAWA hawaliheshimu hili?

Magufuli amesisitiza kuwa tuache siasa tufanye kazi na ifukapo 2020 watanzania watuhukumu kwa haki.

Ukawa ilikuwa inalia na ufisadi na leo hii Magufuli anapambana nao ...kwa nini ukawa wanakuwa ni obstacle?

Kuna hoja nyeti sana za kuibana serikali ya Magufuli mfano Kwenye Afya elimu ajira n.k kwa nini sisikiii uhamasishaji wa maandamano kuhusu haya maswala ya kitaifa??

Ni nani huyu anayejaribu kuwapoteza vijana na kuwaondoa kwenye mstari wa fikra na badala yake anawaimbisha nyimbo mbaya kama kasuku??
 
Hizo hela mlizochanga kuendea dodoma changieni madawati.
Mkumbuke watoto wa wapiga kura kwenye majimbo yenu wanakaa chini.@ chadema
Halimashauri zinazoongozwa na ukawa hakuna kabisa shida ya madawat

Kwasasa wanahangaikia laptop kila mwanafunzi
Mfano kule mbeya mh. mbilinyi anagawa laptop kila kukicha
 
Halimashauri zinazoongozwa na ukawa hakuna kabisa shida ya madawat

Kwasasa wanahangaikia laptop kila mwanafunzi
Mfano kule mbeya mh. mbilinyi anagawa laptop kila kukicha
Acha utani kwenye mambo serious.

Kama hapa dar majimbo ya ukawa watoto wanakaa chini ,sembuse huko vijijini??
 
Bogus, maskini watoto hawakujua kuwa wanachuuzwa. Wajinga ndio 'WALI WAO'
 
Nilisema zilikuwa porojo tu
Wangethubutu wakaona hahaha
 
Mbowe ana akili sio sawa nanyi Lumumba, Dodoma lazima ulinzi shirikishi uwepo. BAVICHA tutaisaidia polisi
 
Nakubaliana na Mbowe, Polisi sio watu wa huruma, watawaua vijana. Kuna njia zingine za kudai haki hiyo, hazijashindikana. Try those first!
Hehehe sasa kama wametaka wenyewe kufa unategemea nini
Wanabahati hawa
 
Amesema kuwa CCM iachwe ifanye mkutano wake, na wao watatumia mikondo yote ya sheria iliyo nchini na nje ya nchi kupigania haki za vyama vya siasa.

Pia amezungumzia suala la vijana waliokamatwa na polisi kuwa wana haki ya kupewa dhamana kwani sheria ipo wazi juu ya hilo, huku akisisitiza kuwa hawaogopi kulala ndani.

AZAM TWO TV
Mbowe hausiki na BAVICHA poleni kwa uongo wa bila kuvaa nguo
 
Amesema kuwa CCM iachwe ifanye mkutano wake, na wao watatumia mikondo yote ya sheria iliyo nchini na nje ya nchi kupigania haki za vyama vya siasa.

Pia amezungumzia suala la vijana waliokamatwa na polisi kuwa wana haki ya kupewa dhamana kwani sheria ipo wazi juu ya hilo, huku akisisitiza kuwa hawaogopi kulala ndani.

AZAM TWO TV
Mwenye chama kaongea unadhani vibarua watafanya nini wajaribu waone
 
Back
Top Bottom