“Napata mashaka katika jina la kampeni hii, sielewi ni kwa jinsi gani jina hili la kampeni litaweza kuendana na aina ya siasa zilizopo katika Tanzania ya sasa ambayo kwa kiasi kikubwa ni tofauti sana na Tanzania ile ya kipindi cha JK ambayo kila mwanasiasa alikuwa na fursa kubwa ya kuongea anavyotaka usiku na mchana.
Kwa mfano unazaa mtoto unamwita Shida, Majuto, masikini, Ugomvi, maradhi n.k utakuwa unategemea aje kuwa mtu wa aina gani hapo badae?”
Kata funua linaweza kuonekana kama jina la kihuni, jina flani la mtaani mtaani ambalo kwa upande wa operation za kisiasa ambazo zinabeba makundi mbali mbali ndani ya jamii kama vile wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, wanazuoni, viongozi wa dini, wazee, vijana, mabibi na mabwana n.k inaweza kutafsiriwa kama operation ya fujo fujo, operation ya kihuni na mambo mengine yanayo fanana na hayo.
Unaweza kuzani kwamba watanzania wengine hawapendi kwa makusudi mipango na operation zinazo anzishwa na vyama vyetu vya upinzani kwa sababu ya kuvichukia vyama hivyo kwa kuwa na chuki binafsi.
lakini suala la msingi katika mada hii ni kuangalia aina ya operation inayoanzishwa na chama flani cha upinzani na uhalisia wa kampeni hiyo katika kuondoa kero na changamoto mbalimbali zinazo wakabili wananchi kwasasa.
Ni kweli kwamba kazi ya upinzani ni kupinga shughuli zinazo fanywa na serikali iliyoko madarakani ili kupata uungwaji mkono kutoka kwa wananchi ambao ndio msingi mkuu wa upatikanaji wa serikali katika nchi zinazo tawaliwa na mifumo ya kidemocrasia.
Operation au kampeni kwa upande wa vyama vya siasa ndio njia pekee inayoweza kujenga misingi thabiti kwa wananchi na wapiga kura kwa ujumla ikiwa tu kampeni husika inayofanywa na chama chochote cha siasa itakuwa na mashiko ama inatoa muelekeo chanya ambao wananchi wengi wanaweza kuona kwamba utakuwa na manufaa kwa maisha yao ya badae.
Kama jina la operation husika inayopangwa kuendeshwa na chama flani cha siasa halitoi picha sahihi ya nini itakuwa faida kwa wananchi kutokana na kampeni hiyo itakayofanyika basi kampeni hiyo kuanzia hapo inakuwa imefeli hata kabla haijaanza.
Operation yoyote ufanisi wake unategemeana sana na jinsi jina la kampeni hiyo litakavyo weza kuamsha hisia kwa wananchi wa makundi yote katika jamii hivyo katika kupata jina la kampeni flani ni vyema sana watu makini na wenye uelewa mpana wa wananchi wakatumika kuliko kutumia ujanja ujanja na haraka haraka kwa ajiri tu yakutengeneza taarifa katika vyombo vya habari kwa jambo ambalo halitakuwa na faida kwa wananchi wa kawaida.
Kwa mfano ACT Wazalendo walitangaza operation linda democrasia, ukiangalia jina la kampeni hii unaweza kuona kitu flani cha msingi ndani yake unaweza hata kupata maudhui ya kampeni hiyo kwa kuangalia msingi na umuhimu wa kulinda democrasia katika jamii yoyote hapa duniani.
Kwa maana hiyo mtu yoyote anaweza kuona umuhimu wa kushiriki katika kampeni kama hiyo kwasababu anakwenda kulinda democrasia ya nchi yake isichezewe na watu au kikundi flani cha watu wasio penda democrasia katika nchi yao.
Operation KATA FUNUA ni nini sasa katika Tanzania ya sasa? Itakuwa na faida gani kwa wananchi wa kawaida? Itakuwa na faida gani kwa chama cha CHADEMA? Ina maudhui gani ambayo yanaweza kuwajenga vijana wa makundi yote kushiriki na hivyo kuifanya iwe na mafanikio makubwa na chanya kwa maendeleo ya democrasia hapa nchini?
Kwa kuwa bado nimapema sana inaweza kuwa vigumu kuizungumzia kwa undani kampeni hii labda mpaka hapo elimu kwa umma itakapo tolewa ili tupate muda wa kuisoma na kuielewa vizuri kabla hatujaanza kushiriki katika kuioperate.
“Napata mashaka katika jina la kampeni hii, sielewi ni kwa jinsi gani jina hili la kampeni litaweza kuendana na aina ya siasa zilizopo katika Tanzania ya sasa ambayo kwa kiasi kikubwa ni tofauti sana na Tanzania ile ya kipindi cha JK ambayo kila mwanasiasa alikuwa na fursa kubwa ya kuongea anavyotaka usiku na mchana. Kwa mfano unazaa mototo unamwita Shida, Majuto, masikini, Ugomvi, maradhi n.k utakuwa unategemea aje kuwa mtu wa aina gani hapo badae?”
Itaendelea