Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Hakuna siku ambayo itanifanya niichukie chadema nikiwa miongoni mwa wanachadema wazalendo kama Siku nitakayosikia Kuwa bwana Lowassa ni mwanachama mwandamizi wa chama chetu kinachojipambanua kwa kupinga ufisadi kama chama kitampokea lowassa Mimi lasmi nitaachana na siasa kwa sababu chama kitakuwa kimekiuka itikadi na falsafa yake na hilo ndilo litakuwa kaburi la chadema, tutafakari pamoja swala hili wana jukwaa.

Wewe ukihama pekee,kuna wanaoingia ndani ya chama 1000 kila siku,
 
Maadili gani Sisiem Wanayo... Kwanza Hakuna Demokrasi Ndani ya CCM: Demokrasi ni Kwa ajiri ya Watu na ni ya Watu Wenyewe. Sasa

Kama KITENGO Kinapoka Maamuzi ya wengi halafu Unahita Maadili. Poleni Sana Kwa Kuweka Personal interest rather than Party Interest.

Naamini Kuna Wagombea Wengi tu Hawakufurahiswa na Jins KITENGO Kiliwafanya. Eti Kamati ya Maadili .

Naona mwaka huu kitengo ndio kimewasababishia maccm kuondoshwa ikulu
 
Ninachokiona ni ule usemi usemao adui muombee njaa, Siamini kama Kuna kipenzi cha chadema ambaye anamhitaji lowasa kuhamia chadema wanachadema wanachotaka ni lowasa awavuruge Ccm ili hstimaye kura Za Ccm zigawanyike na kurahisisha ushindi wa chadema au ukawa ikiwa watasimamisha mgombea mmoja. Nawasilisha.

Ccm ndio inaendelea kukata roho taratibu na kuungana na kina KANU,na upc
 
Tatizo la Watanzania tunaitikiaitikia tu kila wimbo wanaouimba watawala !Leo wanatuaminisha kuwa lowassa ni fisadi, cha kushangaza hawampeleki mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.Ninaamini wimbo huu wa ufisadi umewalenga wale wote wasiopendwa na watawala. Mbona walioiba pesa za escrow wakachukua pesa kupitia benki ya stanbic hawatajwi?Watawala wasitufanye sisi ni wajinga.

Halafu kibaya na dhambi ni pale hao hao wanatumia muda mwingi kumtukana mtu huyo kuwa ni Fisadi, wanatumia mikutano na media kumtusi kwa matusi yote ya duniani na baada ya muda wanasahau wanaanza kumsifie tena kuwa sio Fisadi ni mtu mwema wa kupigiwa mfano na tena ni kamanda daaaaaaa nahisi kizunguzungu daaaaaaaaa!!!
 
Mimi sioni ubaya wa Lowasa kuamia Chadema ...
Kama atafata taratibu za Chama basi nakukaribisha Tena kwa mikono miwili..
Tatizo sio Lowasa tatizo ni Ccm..
Hata Kikwete akikubalia na taratibu za chama tunamkaribisha Chadema

Hiyo ndiyo siasa
 
Hiyo ndiyo siasa

He he he he he!!!!! Wewe inabidi turudie michango yako ya matusi juu ya huyu tuipost hapa ili tuone kama akili yako iko sawasawa! Je unachokisema kinafanana na akili yako?una bahati hauonekaninungejuta kuzaliwa wewe!
 
mmeongea mengi sana maneno matupu hayavunji mfupa, huyo ni mgombea wao leteni mgombea wenu. UKAWA wamefanya kosa kubwa sana kutokumtaja mgombea wao mpaka sasa na kuwapa CCM nafasi kubwa ya kumtambulisha na kufanya kampeni kabla ya wakati, ni maoni yangu kwamba kwa nafasi hii UKAWA wasubiri 2020
Kwaiyo kwakua Ccm wamemtaja makomeo basis na UKAWA wamtaje sio...!!??
Acha kukaririshwa mambo...!!!
Usipanic Jombaa take a time and relax your birthday is coming..
Tutakuimbia tu..
 
Huo ndo msemo tangu enzi, na hii inatokana na historia ambayo mababu zetu wameshuhudia kutoka enzi na enzi.
kwamba kimya kingi kinamshindo mkuu na mshindo wake hauvumiliki,.
kuongea sana wakati mwingine kunaonyesha udhaifu wako.
EDWARD NGOYAI LOWASSA ukimya wake takribani miaka saba ndio uliyemuweka akawa juu zaid ya chama, kwani baada ya kumhujumu kwa muda mrefu kuwa ni fisadi, gamba lakini hatimae wananchi wamejiuliza kwanini ni LOWASSA tuu, kwanin mtu huyu atupiuwe lawama zote hizi, ndipo wananchi walipochoka kusikia sauti hizo nakuamua kuungana nae kwenye safari ya matumaini.
sio kwasababu wananchi waliamua kumuunga mkono kwamba LOWASSA sio fisadi au sio msafi, bali ni ukimya wa LOWASSA ambao uliwaeka wananchi njia panda nakuona kuwa LOWASSA kasingiziwa. pamoja na kuwa jina lake limefanyiwa mizengwe na kukatwa na kamati ya maadili na kushindwa kufika Nec lakini bado LOWASSA kaendelea kuwa kimya mabapo bado kunawachanganya wananchi. Hii inamaana kwamba bado LOWASSA anawaaminisha wananchi kuwa alionewa na ndivyo wengi wanaamini mpaka sasa na hii imechangiwa na UKIMYA WA LOWASSA.
LOWASSA anazivuruga akili za watu, wananchi wanataka wasikie sauti yake, wajue anawaza nn, atoe tamko angalau hata salaam, wamuone hata kanisani, wanataka kujua anataka kufanya maamuzi gani, WANANCHI WANASUBIRI KWA HAMU KUBWAA..
Hata KIKWETE anahamu ya kujua LOWASSA anawaza nini, anataka nini, LOWASSA anamvuruga sana KIKWETE na timu yake, kiukweli LOWASSA ANAIVURUGA NCHI NZIMA.
 
Unaburuzwa wewe,miaka 53 ya uhuru bado mmeng'ang'ania madaraka wakati wananchi wanaendelea kuishi maisha ya dhiki hata mlo wa siku unawashinda
Tutakuwepo kwa miaka mingine 53, kwanza mpaka sasa nyie si washindani.
Hamna hata jina la rais wenu mtarajiwa, siye Magufuli tuna uhakika wa kushinda tena.
 
Jamani huyu mtu LOWASA ataongea lini tupumzike na hili jina tuanze mambo mengine......kila kona ni Lowasa, kila nyumba ni Lowasa, ukifika bar ni Lowasa, ukiingia ofcn ni Lowasa,nikienda kucheza draft kote ni Lowasa, nikiongea na mke wangu dakika tatu badae kamtaja Lowasa......duh!
 
Tutakuwepo kwa miaka mingine 53, kwanza mpaka sasa nyie si washindani.
Hamna hata jina la rais wenu mtarajiwa, siye Magufuli tuna uhakika wa kushinda tena.

Hongera sana kwa kuendelea kuweweseka baada ya kipigo cha 2-0 huko mwanza na musoma.
 
Tutakuwepo kwa miaka mingine 53, kwanza mpaka sasa nyie si washindani.
Hamna hata jina la rais wenu mtarajiwa, siye Magufuli tuna uhakika wa kushinda tena.

Hongera sana kwa kuendelea kuweweseka baada ya kucharazwa baada ya wana wa kanda ya ziwa kukataa kutumiwa na ccm
 
Hongera sana kwa kuendelea kuweweseka baada ya kucharazwa baada ya wana wa kanda ya ziwa kukataa kutumiwa na ccm
Mpaka sasa UKAWA/CHADEMA ni kama kuku asiye na kichwa, hongera zaidi zikujie wewe mwenyewe binfasi kwa kutolitambua hilo.
 
Mpaka sasa UKAWA/CHADEMA ni kama kuku asiye na kichwa, hongera zaidi zikujie wewe mwenyewe binfasi kwa kutolitambua hilo.

Asante sana na nakupongeza kwa kuendelea kufuatilia mchakato wa kumpata rais atakaye waongoza watanzania kwa hawamu ya 5 kupitia ukawa.
 
Jamani huyu mtu LOWASA ataongea lini tupumzike na hili jina tuanze mambo mengine......kila kona ni Lowasa, kila nyumba ni Lowasa, ukifika bar ni Lowasa, ukiingia ofcn ni Lowasa,nikienda kucheza draft kote ni Lowasa, nikiongea na mke wangu dakika tatu badae kamtaja Lowasa......duh!

duuuuuuuuh!!!! na wewe kumtaja mara saba si haba!!!
 
Back
Top Bottom