Mbowe afuta UKUTA, aibukia taifa

Mbowe afuta UKUTA, aibukia taifa

Kabla ya kitendo kilichowanyong'onyesha wafuasi wa chadema cha kufuta ukuta,bila sababu za kueleweka huku akiwa ametoa maagizo mazito ya kuchangishana pesa ambazo wameliwa,hakijapoa,,
Kamera za televisheni ya Azam,zimemmulika akiwa uwanja wa taifa,kapiga nne,akiongea kwa bashasha na Mwigulu Nchemba kama sio yeye alietoa amri ya kuwasusia wabunge wa ccm popote pale

Ushauri wangu
Chadema sio kila mnachoambiwa na viongozi wenu mnafuata mkumbo bila ya kupima
kitendo cha mbowe kukaa karibu na mwigulu na wakapiga story ni cha kupongzwa. hasa kwa siku za hivi karibuni mvutano uliokuwepo kati ya upinzani na vyombo vya dola ambavyo waziri wake ni mwigulu. ni ishara tosha kuwa hayo yamepita, tunasonga mbele kujenga inch yetu. Safi sana mh Mbowe.
 
Umemfananisha, Mbowe hawezi kukaa karibu na Mwigulu! Khaaaaah, haiwezekani mwenyekiti akalamba matapishi yake!
Wewe ni kama mimi...nilipowaona kwenye TV uwanja wa Taifa sikuamini nikazima TV kwanza.
 
Umemfananisha, Mbowe hawezi kukaa karibu na Mwigulu! Khaaaaah, haiwezekani mwenyekiti akalamba matapishi yake!
Ndio keshamba hivyo kama alivyobadili gia angani na kumwita lowassa mungwana badala ya fisadi.
 
Hapa namuunga mkono mleta mada kwa asilimia 100 %, huyu mwigulu ndio aliemvalisha mbwa bendera ya chadema, huyu ndio aliesoma chadema Arusha wamejilipua, huyu ndio aliekuwa anawadhalilisha wabunge wa Chadema bungeni! Siasa tunakubali sio uadui ila ukidhalilishwa nawe unaendelea kukaa na kuongea na aliekudhalilisha kana kwamba hamna kilichotokea Unataka tuamini nini? Ni ujinga uliopitiliza! Sijawahi kumkashfu Mbowe ila kama kuna ukweli basi Mbowe kufikia ukomo wa kukiendesha chama! Na lazima tukubali ukweli huu!
 
Mbowe na maalim seif...kwenye mpira wanashikana mikono ila kwemye misiba hawashikani mikono..Siasa ya Tanzania ni zaidi ya uijuavyo
 
Leo nimemuona kwa macho yangu, akiwa na mwingulu wakishangilia timu yao ya CCM Dah kweli siasa hizi, pasua kichwa.
Haya bwana ila sisi hatudanganyiki na hatufungiki kirahisi. Team profesa
Mbona we una akili za zumbu kuku!Juzi tumeona mechi ya wabunge mashabiki wa yanga na simba tukaona wabunge wa ccm wakikipiga yanga na waupinzani wakikipiga simba
 
Kitendo cha kushangaa Mbowe kujadili mawili matatu na Mwigulu, wakiwa michezoni, uwanjani, si dalili njema.

Taafiti mbalimbali za kisayansi zimetufunza kwamba kuna tatizo kubwa miongoni mwa watu wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea mpaka kuelekea uzee. Ni tatizo la watu kupatwa na mishangao ya kipumbavu.

Utafiti wa hivi karibuni umefanywa na shirika la kitaaluma na kitabibu la Psychodoc Frontiers la nchini Marekani.

Kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa na shirika hilo katika nchi 10 zikiwemo za Afrika na Asia, watu waliofanyiwa utafiti huo (sample population) walikuwa 701,025. Matokeo ni kwamba zaidi ya 42.03% ya watu hao walikutwa na tatizo la mshangao wa kipuuzi.

Na pia 91.67% ya wale waliokutwa na tatizo hilo la mshangao wa kijingaa waligundulika kuwa ni watumiaji wakubwa wa ugoro (wa kuvuta kwa pua na hata wa kuvuta kwa kinywa).

Kwa hiyo hawa watu wanaotiririka hapa kutoa hoja za kuponda tendo la kiungwana na la kimichezo kama hili la Freeman, wanadhihirisha to ukubwa wa tatizo hili.
Vipi kuhusu kitendo cha mbowe kuwapiga marufuku wabunge wa ukawa kuwajongea wale wa ccm,na kuwapiga marufuku mameya wa chadema kuhudhuria hafla atakazokuwepo magufuli,tafiti yako inasemaje
 
Back
Top Bottom