Mbinu mpya kujiuza imegundulika, waathirika na wateja wakubwa ni waume za watu

py thon

JF-Expert Member
Sep 11, 2016
2,471
4,424
Leo katika pita pita zangu maeneo ya gym khana, Aga khan nilimuona mdada/mama mwenye umri kati ya 39,38 amebeba beseni la mihogo kichwani na mfuko wa maembe na ukizingatia siku kama 3 au 4 zilizopita nilikutana na uzi inayowasema vibaya wajasiriamali hawa wanaoshamiri kwa wingi sasa hivi jijini hivyo nikawa nampiga jicho kwa kuwa alikuwa mbele yangu na barabarani palikuwa na foleni cha kizushi

Mara kidogo nikamuona akielekea kwenye moja ya gari bila shaka aliitwa, mimi nikamkata jicho na kwakuwa nilikuwa kama mita 20 nyuma yake hivyo nilikuwa na advantage ya kuusoma mchezo wote kama atakuwa anafanya kazi yake ya kuuza mihogo au kazi nyingine ambayo wanashutumiwa nayo.

Hilo gari ilifunguliwa mlango na muuza mihogo akatwisha beseni lake chini na kama sekunde kadhaa akaingia ndani ya ile gari, nikafanikiwa kulifikia lile gari na mlango ulikuwa bado upo wazi yule mdada alikuwa anacheka /tabasamu tu na ndani ya ile gari walikuwepo njemba watatu.

Nikalipita lile gari na idea ikanijia ya kupiga picha ila bahati mbaya foleni ikawa inatembea nikashindwa kupata angle nzuri ya kupata picha murua lile gari ikasepa.

Nikaendelea na safari zangu lakini mbele kidogo nikakutana na mtu ninaye mfahamu tukapiga soga mbili tatu na kama 30mins namuona yule muuza mihogo akitembea na kuelekea sehemu ambayo ile gari ilimzuia asiende.

NB: Ile nyuzi iliyotolewa siku kadhaa nyuma kuhusu hawa wajasiriamali watembeza mihogo, ndizi naiamini 100% kuanzia leo.

Nilichogundua

1.Hawa akida dada wanatoa huduma ya chap chap.

2.Lakini najiuliza huwa wanatembea na condoms? Kama hawatembei nazo basi tishio la kuongezeka maambukizi ya VVU ni kubwa.

3.Nyie wanawake mliolewa na wanaume/ akina baba wanaofanya kazi Posta , kazi mnayo kwa niliyoshuhudia Leo.

4.Kama dada yako, mke wako anafanya biashara hiyo nakushauri mrudishe kijijini, ipo siku utatumia gharama kubwa hospitali.

Nawakumbusha: UKIMWI upo jihadharini


ac1768ce0169001e7249e6fe5f240ea2.jpg
 
Hali ngumu wanajiongezea kipato aidha wale machangu professional ni ghali
 
JAMAA MMOJA KATONGOZA WEEE WAUZA MIHOGO KATOSWA BASI KAJA NA KASHFA DHIDI YAO. LEO KWA WAUZA MIHOGO NA MATUNDA KESHO ITAKUA KWA WAUZA VITUMBUA NA MAANDAZI,KESHO KUTWA WAUZA MAGAZETI WANAWAKE ILI MRADI TU KUWAKATISHA TAMAA YA UJASIRIAMALI.
 
Mbona hawa wadada hawana mvuuto kivilee au ndokusema wanaume hatuangalii ubora wa bidhaaa
Ndg yangu hata mimi ninashangazwa sana.
Lakini sikumoja, nilipata simulizi toka kwa kada wa hayo mambo.
Alikuwa wa jinsi ya 'me', akadai kuwa yeye hujisikia huru na raha sana kuulizwa na mwanamke kuwa "kwani utanipa shilingi ngapi?" Huelewana na kuondoka kwenda kumaliza matatizo yao. Kuliko kufanya penzi la kibubububu ambalo baadae huzaa lawama na utovu wa amani. Huenda kulifanya tendo kwa raha na kujiamini kwa jeuri ya pesa yake.
Na wanapimalizana hawezi kuvurugwa kisaikolojia ya kuachana kwa lawama kwamba hajatoa chochote, ama katoa chini ya matarajio.
Pia akasema 90% ya wanawake wenye sura mbofumbofu, kiuhalisia ni wazuri sana kimapenzi kuwazidi mno wanawake mishepu.
Kama ni cheo, basi wanawake wasio na sura ya kuvutia, kitandani ni maboss halafu wenye sura za kuvutia ni wafagizi tu.
Yawezekana mtoa mada kaleta uzi wenye mashiko.
 
JAMAA MMOJA KATONGOZA WEEE WAUZA MIHOGO KATOSWA BASI KAJA NA KASHFA DHIDI YAO. LEO KWA WAUZA MIHOGO NA MATUNDA KESHO ITAKUA KWA WAUZA VITUMBUA NA MAANDAZI,KESHO KUTWA WAUZA MAGAZETI WANAWAKE ILI MRADI TU KUWAKATISHA TAMAA YA UJASIRIAMALI.


hivi mdada aingie kwenye gari tinted waondoke

achukuliwe tu na mtu asiyemfahamu

wewe utafikiria vipi
 
JAMAA MMOJA KATONGOZA WEEE WAUZA MIHOGO KATOSWA BASI KAJA NA KASHFA DHIDI YAO. LEO KWA WAUZA MIHOGO NA MATUNDA KESHO ITAKUA KWA WAUZA VITUMBUA NA MAANDAZI,KESHO KUTWA WAUZA MAGAZETI WANAWAKE ILI MRADI TU KUWAKATISHA TAMAA YA UJASIRIAMALI.
wana roho mbaya sana hawa watu Mungu anawaona ipo siku mkuu
 
Back
Top Bottom