Mbinguni ni wapi?

Mbinguni ni wapi?

USIPATE SHIDA SANA KUPATAFUTA MBINGUNI, MAANA NI HAPA HAPA TUNAMOISHI SISI WANADAM NA VIUMBE WENGINE!!

MBINGUNI KAMA MBINGUNI PAMEELEKEZWA PALIPO KUPITIA KITABU CHA MWANZO. SOMA HABARI ZA UUMBAJI MAANA HATA MBINGU ILIVYOUMBWA NA LOCATION ILIPO VYOTE VIMEELEZWA.

KWAHIYO NDUGU YANGU, SISI TULE BATA TUU MBINGUNI NI HAPA HAPA TULIPO SEMA TUPO SEHEMU YA CHINI YA MBINGU, YAANI ARDHINI.
 
Salute comrades,

Wakuu, naomba kufahamishwa, Mbinguni anapoishi Mungu ni wapi?

Ukisoma Biblia, Katekisimu etc zinasema Mungu yupo Mbinguni na mahali pote duniani. Je Mbinguni ni wapi?

Ni kule juu angani kwenye mawingu? Qur'an inasema zipo Mbingu saba na Mungu anaishi Mbingu ya saba, je Mbingu hiyo iko sehemu gani?

Pia tunaambiwa Nimrod na wenzie walijenga mnara ulikua unakaribia kufika Mbinguni kwa Mungu, je huko Mbinguni ni kule juu angani?

Kama Mbinguni ni huko juu angani mbona sasa hivi kuna vifaa mbalimbali ambavyo vinapita huko angani kwenda sayari zingine?

Mbona Mungu hayazuii kama alivyowazuia kujenga mnara wa Babeli sababu wanapita huko angani inaposadikika ndio Mbinguni.


Da'Vinci
Mbingu ni dhana ya kiroho Ila kwa mtazamo wa kibinadamu ni hili anga tunaloliona hapo juu.. Na kiuhalisia hiyo sio mbingu kwakuwa ukiwa angani unachoona ni upeo usio na mwisho
Dhana ya mbingu kuwa juu inatokana na dhana ya jehanum kuwa chini
 
mimi mwenyew na subiri majibu ya swali lako ...

maana tunasikia tu mbinguni mbinguni lakini hatujuibkuwa niwapi ..mbaya zaidi sehemu kubwa ya Jamii ambayo IPO mtaani inadhani kuwa mbingu nihuo mwanga wa jua wa blue tunaouona angani daily ...hata mimi zamani nilikiwa najua kuwa ile ndio mbingu na kwakuwa waislam wanasema kuwa mbingu ziko 7 nami nilikuwa nadhani kuwa baada ya ile Rangi ya blue tuionayo angani ambayo Jamii huwa inadhani kuwa ni mbingu basi juu yake patakuwa na mbingu nyingine 7
Kwani hiyo rangi ya blue ukiienda huko haipo mm sijui naionaga tu
 
Kwani hiyo rangi ya blue ukiienda huko haipo mm sijui naionaga tu
haipo mkuu ...ile nisehemu tu ya mwisho wa upeo wa macho yko pamoja na matokoa ya mwanga wa jua...nikama vile uonavyo maji kwa mbali ukiwa kwenye lami
 
Ungejua mechanism of brain usingesema hivi..vingine hatuwezi kujua..ukifikiria sana unweza kupalalaizi..limity ya brain kutambua vitu inaangukia kwenye faith..
Wapi wapi mwanasayansi hawckings.
Mekanizmu ya ubongo ipoje?
 
Mekanizmu ya ubongo ipoje?
Ni elimu ndefu kidogo ingia google..ila point yangu ni kwamba mengine hatuwezi kuyajua hata tujitahidi vip kwa sababu yapo beyond of our sense..utambuzi wa mwanadamu una ukomo.
 
Ni elimu ndefu kidogo ingia google..ila point yangu ni kwamba mengine hatuwezi kuyajua hata tujitahidi vip kwa sababu yapo beyond of our sense..utambuzi wa mwanadamu una ukomo.
Ni kweli mkuu ila ukipata muda tupatie hiyo elimu mkuu, hata ufungue uzi...
 
Back
Top Bottom